Nchimbi kupata PhD

Nchimbi J

Senior Member
Jun 16, 2008
132
20
Wana JF,

Kwa mujibu wa habari tulizopata muda huu, ni kuwa hatimaye Mh. Emmanuel Nchimbi amefanikiwa kumaliza PHD yake aliyoianza mwaka 2004.
Katika PHD hiyo ambayo alikuwa akifanya utafiti wa uhusiano wa umasikini na mikopo midogo midogo katika mazingira ya wajasiliamali wa Tanzania wanaoukutana na vikwazo kadha wa kadha kama vile umeme, kushuka kwa thamani ya shilling, mzunguko mdogo wa hela na nguvu ya soko ya nje wanavyoweza kutoka kwenye lindi hioli la umasikini.

PHD paper yake ilipelekwa na kusahihishwa taasisi ya Development Studies ya UDSM kama external na walimpa alama ya A nilivyoambiwa.

Nakaribisha maoni yenu kama ifuatavyo: -
1. Mzumbe haina status,
2. Kaandikiwa ni kilaza,
3. Anajisafisha baada ya kuona anaandamwa,
4. Tuletewe tuipitie hapo jamvini (anaedai tena ni std 7),
5. Hatuitambui kabisa,
6. Huu ni uzushi,
7. Hata masters hana mbona,
8. Ni ya kisiasa hiyo,
9. Mimi hata sisomi hii thread
11. Huyu alietuma ni mpuuzi, mjinga, analeta utoto hapa,
12. Nae anataka urais,
13. Kumbe ni rahisi sana,
14. Tupe source ya taarifa,
15. Lini alipata muda wa kufanya huo utafiti,
16. Kapendelewa na walimu wa mzumbe na udsm pia
17. Nimeambiwa utafiti wenyewe ni shallow sana,
18. Mwalimu mmoja wa mzumbe kaniambia kuwa wameamua kumwachia tu,
19. Shule za bongo ni za ajabu kweli hivi mzumbe wanaweza kutoa PHD kweli,Mzumbe walimu wote wana PHD fake likewise na wanafunzi pia,
20. Nampongeza kama ni kweli.

Graduation itakuwa mwanzoni mwa December. Kama una maoni yafananayo na naapo juu yani namba 1-20 , changia kwa kuweka namba inayowiana namchango wako tu inatosha kama ni tofauti basi karibu.

Nov 30, 2011

WAZIRI wa Waziri wa Habari, Utamaduni, Vijana na Michezo, Dk Emmanuel Nchimbi, kesho atatunukiwa Shahada ya Uzamivu katika mahafali ya Chuo Kikuu cha Mzumbe, mkoani Morogoro.

Katika taarifa yake kwa vyombo vya habari jana, Mkurugenzi wa Mawasiliano wa chuo hicho, Rainfrida Ngatunga, alisema Dk Nchimbi ni miongoni mwa wahitimu saba wa shahada ya uzamivu watakaotunikiwa shahada hiyo kesho.Wahitimu wengine ni Gustav Kunkuta, Simon Lushakuzi, Sunday Makama wa Nigeria, George Makoma, Anarabbi Nangawe na Fred Rwechengula.

Ngatunga alimtaja mgeni rasmi katika mahafali hayo kuwa ni Jaji Mkuu mstaafu, Barnabas Samatta.Kwa mujibu wa mkurugenzi huyo, wahitimu 2,220 watatunukiwa shahada mbalimbali katika mahafali hayo ya kumi ya chuo hicho.

"Sisi kama chuo tunajivunia sana kuona uwiano wa jinsia kwa wahitimu unavyoshabihiana kwa sababu katika wahitimu hao 1,282 ni wanaume na 938 ni wanawake," alisema Ngatunga.Alisema mahafali hayo yatatanguliwa na warsha itakayofanyika leo katika chuo hicho.

Alisema miongoni mwa mambo yatakayofanyika katika warsha hiyo ni kutambua michango mbalimbali ya wanazuoni waliofanya vizuri katika masomo na tafiti."Chuo chetu kitachukua fursa hiyo pia kutambua mchango wa Bima ya Afya ya Taifa (NHIF) katika ujenzi wa bweni la wanafunzi wa kike katika Kampasi Kuu ya Morogoro," alisema.

Ngatunga alisema chuo pia kinatambua mchango mkubwa na uungaji mkono wa Benki ya CRDB katika mchakato wa kuandaa kongamano la wadau wa elimu la chuo hicho lililofanyika Mei mwaka huu.

Kuhusu mahafali hayo, alisema wahitimu hao 1,365 watatunukiwa katika Kampasi Kuu ya Morogoro kesho,wakati 472 watatunukia shahada za uzamili katika Shule ya Biashara ya Mzumbe ya Dar es Salaam Desemba 16 na 383 watatunukiwa shahada zao kwenye Kampasi ya Mbeya Desemba 10, mwaka huu.

"Kwa mara ya kwanza katika historia ya chuo chetu wahitimu watatunukiwa shahada ya elimu katika Lugha na Uongozi ( Bachelor Education in Language Management),Shahada ya Elimu katika Biashara na Uhasibu (Bachelor of Education in Commerce and Accounting) na Shahada ya Elimu katika Uchumi na Uongozi (Bachelor of Education in Economics and Management)," aliongeza.
 
Kama sikosei 2004 NDO alikuwa anamaliza MBA pale mzumbe ngoja nicheki kwa mafile yangu vyema ntarudi!
Sasa kama alimaliza na kuunga PHD kwa kutumia 8 years amengangana vya kutosha
 
Tell him
gun.gif
 
Bora nae angeomba tu apewe ya bure kwa kufunga michuano ya kagame kwa mwanga wa ambulance
 
Nov 30, 2011

WAZIRI wa Waziri wa Habari, Utamaduni, Vijana na Michezo, Dk Emmanuel Nchimbi, kesho atatunukiwa Shahada ya Uzamivu katika mahafali ya Chuo Kikuu cha Mzumbe, mkoani Morogoro.

Katika taarifa yake kwa vyombo vya habari jana, Mkurugenzi wa Mawasiliano wa chuo hicho, Rainfrida Ngatunga, alisema Dk Nchimbi ni miongoni mwa wahitimu saba wa shahada ya uzamivu watakaotunikiwa shahada hiyo kesho.Wahitimu wengine ni Gustav Kunkuta, Simon Lushakuzi, Sunday Makama wa Nigeria, George Makoma, Anarabbi Nangawe na Fred Rwechengula.

Ngatunga alimtaja mgeni rasmi katika mahafali hayo kuwa ni Jaji Mkuu mstaafu, Barnabas Samatta.Kwa mujibu wa mkurugenzi huyo, wahitimu 2,220 watatunukiwa shahada mbalimbali katika mahafali hayo ya kumi ya chuo hicho.

"Sisi kama chuo tunajivunia sana kuona uwiano wa jinsia kwa wahitimu unavyoshabihiana kwa sababu katika wahitimu hao 1,282 ni wanaume na 938 ni wanawake," alisema Ngatunga.Alisema mahafali hayo yatatanguliwa na warsha itakayofanyika leo katika chuo hicho.

Alisema miongoni mwa mambo yatakayofanyika katika warsha hiyo ni kutambua michango mbalimbali ya wanazuoni waliofanya vizuri katika masomo na tafiti."Chuo chetu kitachukua fursa hiyo pia kutambua mchango wa Bima ya Afya ya Taifa (NHIF) katika ujenzi wa bweni la wanafunzi wa kike katika Kampasi Kuu ya Morogoro," alisema.

Ngatunga alisema chuo pia kinatambua mchango mkubwa na uungaji mkono wa Benki ya CRDB katika mchakato wa kuandaa kongamano la wadau wa elimu la chuo hicho lililofanyika Mei mwaka huu.

Kuhusu mahafali hayo, alisema wahitimu hao 1,365 watatunukiwa katika Kampasi Kuu ya Morogoro kesho,wakati 472 watatunukia shahada za uzamili katika Shule ya Biashara ya Mzumbe ya Dar es Salaam Desemba 16 na 383 watatunukiwa shahada zao kwenye Kampasi ya Mbeya Desemba 10, mwaka huu.

"Kwa mara ya kwanza katika historia ya chuo chetu wahitimu watatunukiwa shahada ya elimu katika Lugha na Uongozi ( Bachelor Education in Language Management),Shahada ya Elimu katika Biashara na Uhasibu (Bachelor of Education in Commerce and Accounting) na Shahada ya Elimu katika Uchumi na Uongozi (Bachelor of Education in Economics and Management)," aliongeza.
 
Kwa nini usishangae Dr. Remmy (hayati), professor Maji marefu, unamshangaa DR. NCHIMBI!!!!

Way back walisema alipata Ph.D baada ya kuondoka Umoja wa Vijana...

Kwahiyo hana ni Ph.D za kununua na CCM inaamua kumpa ya Mzumbe labda wanataka aje awe Rais
 
Sasa kwanini alikuwa anaitwa Dr. Nchimbi miaka yote hiyo?

Labda anapewa ya pili. Labda amekuja kunote kuwa Ph.D yake ya kwanza was from unaccredited entity, i.e CommonWealth Open University (tofautisha na Commonwealth Institute) na ingekuja kumsumbua wakati wa kugombea Urais. Hata Wikipedia wamelist hiki chuo kama unacredited (List of unaccredited institutions of higher education - Wikipedia, the free encyclopedia). Lakini Waziri wetu alipiga shule ya Masters na Ph.D hapo.

CommonWealth Open UniversityPhD (Management)20012003PHD
CommonWealth Open UniversityMSc. (Management)19992001MASTERS DEGREE
Mzumbe UniversityMBA (Finance & Banking)20012003MASTERS DEGREE
Institute of Development Management - MzumbeAdvanced Diploma in Administration19941997ADV DIPLOMA

And last year, the Tanzania Commission for Universities (TCU) informed that they have no legal right to punish or have the authority to force people to get their educational documents verified. The Senior Public Relations Officer, Mr Edward Mkaku said “The law that governs us (TCU) do not allow us to forcefully make someone produce certificates for verification; we have to wait for either the employer or the person to bring them to us.”

The report mentioned the institutions which issued the doubtful qualifications to include the Washington International University based in Hawaii, Commonwealth Open University (where Dr Nchimbi claims to have studies his masters and Ph.D)based in Caicos Virgin Island, Free States University, Ambala University in India and Almeda University, USA.

Kaazi kwelikweli.
 
Watanzania kwa kupenda title za uchwara....Ukiotoa Mzumbe hivyo vyuo vya mheshimiwa Nchimbi ni vya online, tena haviko accredited!!
Newt Gangrich ni kichwa (PhD), lakini hata siku moja hujasikia sijui DR/PROF./ENGINEER. NEWT GINGRICH
 
Watanzania kwa kupenda title za uchwara....Ukiotoa Mzumbe hivyo vyuo vya mheshimiwa Nchimbi ni vya online, tena haviko accredited!!
Newt Gangrich ni kichwa (PhD), lakini hata siku moja hujasikia sijui DR/PROF./ENGINEER. NEWT GINGRICH

Ndo hapo sasa....
 
hii ni aibu hii!!

CommonWealth Open UniversityPhD (Management)20012003PHD
CommonWealth Open UniversityMSc. (Management)19992001MASTERS DEGREE
Mzumbe UniversityMBA (Finance & Banking)20012003MASTERS DEGREE
Institute of Development Management - MzumbeAdvanced Diploma in Administration19941997ADV DIPLOMA
 
hii ni aibu hii!!

CommonWealth Open UniversityPhD (Management)20012003PHD
CommonWealth Open UniversityMSc. (Management)19992001MASTERS DEGREE
Mzumbe UniversityMBA (Finance & Banking)20012003MASTERS DEGREE
Institute of Development Management - MzumbeAdvanced Diploma in Administration19941997ADV DIPLOMA

Mkuu kwa mujibu wa signature yako amestuka, ndio kaenda kuchukua ya Mzumbe. Hivi kwa nini kuitwa Dk ni dili sana kwa Watanzania?
 
  • Thanks
Reactions: Nzi
Walau huyu bwana ameonesha umakini kwa kupambana na kubeba U-daktari wa Falsafa wa ukweli hapa hapa bongo baada ya kukosea "mlango wa choo" katika attempt ya kwanza. Sielewi sana huu upondaji wa Mzumbe unaanzia wapi, ikumbukwe kwamba Thesis ya PhD hupelekwa kwa External Examiner aliyebobea na inaporudi candidate lazima afaulu "Viva Voce" examination.

Anastahili Hongera bila kujali hayo meengi yanayosemwa.
 
Back
Top Bottom