Wana JF,
Kwa mujibu wa habari tulizopata muda huu, ni kuwa hatimaye Mh. Emmanuel Nchimbi amefanikiwa kumaliza PHD yake aliyoianza mwaka 2004.
Katika PHD hiyo ambayo alikuwa akifanya utafiti wa uhusiano wa umasikini na mikopo midogo midogo katika mazingira ya wajasiliamali wa Tanzania wanaoukutana na vikwazo kadha wa kadha kama vile umeme, kushuka kwa thamani ya shilling, mzunguko mdogo wa hela na nguvu ya soko ya nje wanavyoweza kutoka kwenye lindi hioli la umasikini.
PHD paper yake ilipelekwa na kusahihishwa taasisi ya Development Studies ya UDSM kama external na walimpa alama ya A nilivyoambiwa.
Nakaribisha maoni yenu kama ifuatavyo: -
1. Mzumbe haina status,
2. Kaandikiwa ni kilaza,
3. Anajisafisha baada ya kuona anaandamwa,
4. Tuletewe tuipitie hapo jamvini (anaedai tena ni std 7),
5. Hatuitambui kabisa,
6. Huu ni uzushi,
7. Hata masters hana mbona,
8. Ni ya kisiasa hiyo,
9. Mimi hata sisomi hii thread
11. Huyu alietuma ni mpuuzi, mjinga, analeta utoto hapa,
12. Nae anataka urais,
13. Kumbe ni rahisi sana,
14. Tupe source ya taarifa,
15. Lini alipata muda wa kufanya huo utafiti,
16. Kapendelewa na walimu wa mzumbe na udsm pia
17. Nimeambiwa utafiti wenyewe ni shallow sana,
18. Mwalimu mmoja wa mzumbe kaniambia kuwa wameamua kumwachia tu,
19. Shule za bongo ni za ajabu kweli hivi mzumbe wanaweza kutoa PHD kweli,Mzumbe walimu wote wana PHD fake likewise na wanafunzi pia,
20. Nampongeza kama ni kweli.
Graduation itakuwa mwanzoni mwa December. Kama una maoni yafananayo na naapo juu yani namba 1-20 , changia kwa kuweka namba inayowiana namchango wako tu inatosha kama ni tofauti basi karibu.
Kwa mujibu wa habari tulizopata muda huu, ni kuwa hatimaye Mh. Emmanuel Nchimbi amefanikiwa kumaliza PHD yake aliyoianza mwaka 2004.
Katika PHD hiyo ambayo alikuwa akifanya utafiti wa uhusiano wa umasikini na mikopo midogo midogo katika mazingira ya wajasiliamali wa Tanzania wanaoukutana na vikwazo kadha wa kadha kama vile umeme, kushuka kwa thamani ya shilling, mzunguko mdogo wa hela na nguvu ya soko ya nje wanavyoweza kutoka kwenye lindi hioli la umasikini.
PHD paper yake ilipelekwa na kusahihishwa taasisi ya Development Studies ya UDSM kama external na walimpa alama ya A nilivyoambiwa.
Nakaribisha maoni yenu kama ifuatavyo: -
1. Mzumbe haina status,
2. Kaandikiwa ni kilaza,
3. Anajisafisha baada ya kuona anaandamwa,
4. Tuletewe tuipitie hapo jamvini (anaedai tena ni std 7),
5. Hatuitambui kabisa,
6. Huu ni uzushi,
7. Hata masters hana mbona,
8. Ni ya kisiasa hiyo,
9. Mimi hata sisomi hii thread
11. Huyu alietuma ni mpuuzi, mjinga, analeta utoto hapa,
12. Nae anataka urais,
13. Kumbe ni rahisi sana,
14. Tupe source ya taarifa,
15. Lini alipata muda wa kufanya huo utafiti,
16. Kapendelewa na walimu wa mzumbe na udsm pia
17. Nimeambiwa utafiti wenyewe ni shallow sana,
18. Mwalimu mmoja wa mzumbe kaniambia kuwa wameamua kumwachia tu,
19. Shule za bongo ni za ajabu kweli hivi mzumbe wanaweza kutoa PHD kweli,Mzumbe walimu wote wana PHD fake likewise na wanafunzi pia,
20. Nampongeza kama ni kweli.
Graduation itakuwa mwanzoni mwa December. Kama una maoni yafananayo na naapo juu yani namba 1-20 , changia kwa kuweka namba inayowiana namchango wako tu inatosha kama ni tofauti basi karibu.
Nov 30, 2011
WAZIRI wa Waziri wa Habari, Utamaduni, Vijana na Michezo, Dk Emmanuel Nchimbi, kesho atatunukiwa Shahada ya Uzamivu katika mahafali ya Chuo Kikuu cha Mzumbe, mkoani Morogoro.
Katika taarifa yake kwa vyombo vya habari jana, Mkurugenzi wa Mawasiliano wa chuo hicho, Rainfrida Ngatunga, alisema Dk Nchimbi ni miongoni mwa wahitimu saba wa shahada ya uzamivu watakaotunikiwa shahada hiyo kesho.Wahitimu wengine ni Gustav Kunkuta, Simon Lushakuzi, Sunday Makama wa Nigeria, George Makoma, Anarabbi Nangawe na Fred Rwechengula.
Ngatunga alimtaja mgeni rasmi katika mahafali hayo kuwa ni Jaji Mkuu mstaafu, Barnabas Samatta.Kwa mujibu wa mkurugenzi huyo, wahitimu 2,220 watatunukiwa shahada mbalimbali katika mahafali hayo ya kumi ya chuo hicho.
"Sisi kama chuo tunajivunia sana kuona uwiano wa jinsia kwa wahitimu unavyoshabihiana kwa sababu katika wahitimu hao 1,282 ni wanaume na 938 ni wanawake," alisema Ngatunga.Alisema mahafali hayo yatatanguliwa na warsha itakayofanyika leo katika chuo hicho.
Alisema miongoni mwa mambo yatakayofanyika katika warsha hiyo ni kutambua michango mbalimbali ya wanazuoni waliofanya vizuri katika masomo na tafiti."Chuo chetu kitachukua fursa hiyo pia kutambua mchango wa Bima ya Afya ya Taifa (NHIF) katika ujenzi wa bweni la wanafunzi wa kike katika Kampasi Kuu ya Morogoro," alisema.
Ngatunga alisema chuo pia kinatambua mchango mkubwa na uungaji mkono wa Benki ya CRDB katika mchakato wa kuandaa kongamano la wadau wa elimu la chuo hicho lililofanyika Mei mwaka huu.
Kuhusu mahafali hayo, alisema wahitimu hao 1,365 watatunukiwa katika Kampasi Kuu ya Morogoro kesho,wakati 472 watatunukia shahada za uzamili katika Shule ya Biashara ya Mzumbe ya Dar es Salaam Desemba 16 na 383 watatunukiwa shahada zao kwenye Kampasi ya Mbeya Desemba 10, mwaka huu.
"Kwa mara ya kwanza katika historia ya chuo chetu wahitimu watatunukiwa shahada ya elimu katika Lugha na Uongozi ( Bachelor Education in Language Management),Shahada ya Elimu katika Biashara na Uhasibu (Bachelor of Education in Commerce and Accounting) na Shahada ya Elimu katika Uchumi na Uongozi (Bachelor of Education in Economics and Management)," aliongeza.