Richard
JF-Expert Member
- Oct 23, 2006
- 14,939
- 20,399
Nchi za Tanzania, Angola na Congo DRC ni nchi muhimu katika mstakabali mapinduzi ya viwanda barani Ulaya na Marekani.
Mwaka 2020 Uingereza walitangaza kuachana na magari yatumiayo mafuta ya diseli na petroli kufikia mwaka 2030 na wameazimia kuanza kutengeneza magari zaidi yatumiayo betri.
Hata hivyo tayari magari yatumiayo betri tayari yanatengenezwa katika nchi mbalimbali barani Ulaya.
Nchi za kibeberu au maadui wa maendeleo hawawezi kuiruhusu Tanzania iendelee kwa kuwa na viwanda vyake .
Pia Tanzania ina malighafi zote kutengeneza hata seti za televisheni, vioo vya madirisha na balbu.
Kuna mambo matatu makuu ambayo sisi binadamu twapaswa kufahamu.
Mambo hayo ni technical know what, technical know how and technical know why.
Darasani mwalimu hutufundisha kuhusu somo la jiografia, kisha kuingia ndani kufanya tathmini kutumia kifaa maalum cha Compass kwa kutumia ramani na hiyo ni technical how.
Pale uanzapo kujiuliza hii Compas imetengezwa vipi ndipo unapoingia kwenye technical know why.
Mabeberu wanakuambia kuwa Afrika kuna dhahabu tatu ambazo ni Tanzania, Angola na Congo DRC.
Mabeberu wanaendelea kuziangalia nchi tatu ambazo nchi za Tanzania, Angola na Congo DRC ambazo wana malengo ya muda mrefu hadi miaka 50.
Katika nchi hizo ni Tanzania ambayo wao mabeberu wana uwezo wa kuingia na kujichotea maliasili watakavyo.
Kutokea bandari ya Lobito iliopo Benguela kupitia Lusaka, Lubumbashi ni ukanda maalum ulojaa madini, mafuta na madini ya uranium ambavyo ni malighafi muhimu kwa utengenezaji wa betri za magari, simu za mkononi na mabomu ya nyuklia na mitambo yake.
Lango kuu la kuingia kwenda huko ndani au (interior) na kutokea ni Bagamoyo na ni njia rahisi kuliko kuzunguka Cape Town.
Ila mabeberu hao wakadai kuwa watakuja kwa mazungumzo na ikiwa mazungumzo yatashindikana basi watatumia mbinu zozote kuhakikisha wanafanikiwa azma yao.
Wazungu hao wanasema kuwa Tanzania ni nchi ya kuingia na kutokea Afrika kupitia Bagamoyo. Pia wanasema kuwa asilimia 60 ya biashara ya meli kuanzia mwaka 2050 itakuwa ndani ya bahari ya Hindi na hiyo ndio itakuwa Ocean of the future.
Hivyo, meli yaweza kutoka bandari ya Lobito kupitia Dar-es-Salaam hadi mfereji wa Suez bila shida na kwa uharaka zaidi.
Na hivyo ndivyo mfalme Leopold wa pili wa Belgium alivyokubaliana na wakoloni wa kijerumani kujenga reli ya kati ambayo ingesafirisha bidhaa zote za malighafi kutoka katikati ya Tanzania na Afrika kuelekea bahari ya Hindi.
Mfalme huyo alikuwa akivuna zao la mpira na kulisafirisha kwenda Ulaya kutengeneza bidhaa mbalimbali kama matairi ya magari, baiskeli na zingine yaani alikuwa "supplier" mkubwa.
Moja ya viwanda vikubwa ambavyo mfalme huyo alikuwa akiviuzia malighafi ya mpira ni kiwanda kinachotengeneza bidhaa za Dunlop.
Waafrika wengi sana raia wa Congo walikufa wakivuna zao hilo na wengine kukatwa mikono kwa kushindwa kufanya hivyo.
Bahari ya Hindi ni bahari ilojaaliwa kila aina ya maliasili kuanzia mafuta, gesi asilia na uranium. Leo hii twashuhudia jinsi magaidi wa kupandikizwa nchini Msumbiji wakitumika kama kivuli cha wizi wa maliasili hizi zinazoibwa usiku na mchana.
Mwandishi Robert Kaplan katika kitabu chake cha Monsoon - "The India Ocean and Future of American Power" anaitaja bahari ya Hindi kama New Great Game kama ndo njia ya China ikitumia meli zake kubwa za mafuta kusaka maliasili hiyo ndani ya bahari ya Hindi.
Lakini safari hii upo uwezekano mkubwa wa vita ndani ya bahari hiyo baina ya nch iza kibeberu yaani Marekani na China.
Kaplan anaelezea muungano wa nchi za Marekani, China na India katika bahari ya Hindi katika kufanya biashara, kuzuia vitendo vya utekaji meli yaani Piracy, kulinda njia za usafiri wa meli na kuitikia wito wa majanga ndani ya bahari hiyo.
Bila shaka kelele za ujenzi wa bandari ya Bagamoyo ni moja ya vielelezo vya mpango wa nchi za kibeberu.
Mkataba wa ujenzi wa bandari ya Bagamoyo ulofumuliwa na hayati John Magufuli haukuwa mkataba uloweka maslahi ya taifa mbele na ulikuwa ni wa miaka 99.
Mkataba huo pia haukuwa unaruhusu maendelezo yoyote ya bandari zingine kama bandari ya Dar-es-Salaaam, Tanga, Zanzibar.
Hiyo ni kwasababu Bagamoyo ndo lango kuu la kuingiza na kutoa rasilimali zote zinatoka ndani ya Tanzania na maliasili zingine zinazotoka ndani ya Congo DRC na Angola.
Kwa vile nchi za kibeberu tayari wana ramani ya Afrika na sehemu zilipo maliasili basi Tanzania pamoja na Angola na Congo DRC na wanafahamu kuwa sasa hivi ujazo wa Uranium na madini mengine umefikia kiwango cha juu kiasi cha kuweza kuvunwa, basi sisi hatuna ujanja.
Tanzania tunapaswa kueleza wazi msimamo wetu na pia kueleza ni nini tunataka kwani mali tunayo.
Tanzania haina budi kulinda ukanda wa bahari ya Hindi hadi Msumbiji kuhakikisha usalama wake hauingiliwi kirahisi. Serikali pia inawajibika kueleza msimamo wake kuhusiana na mkataba wa ujenzi wa bandari ya Bagamoyo.
Lakini si kuanza kuzunguka mbali na kuanza mijadala ya kupoteza muda huku tayari wenzetu wachache wamekaa tayari na mabeberu na wamepanga nini kinachofuata.
La sivyo tunakubali kuwa sie ni waangalizi tu wa rasilimali tulozikalia na tupo tayari kuzigawa bure au kwa ujira kiduchu.
Mwaka 2020 Uingereza walitangaza kuachana na magari yatumiayo mafuta ya diseli na petroli kufikia mwaka 2030 na wameazimia kuanza kutengeneza magari zaidi yatumiayo betri.
Hata hivyo tayari magari yatumiayo betri tayari yanatengenezwa katika nchi mbalimbali barani Ulaya.
Nchi za kibeberu au maadui wa maendeleo hawawezi kuiruhusu Tanzania iendelee kwa kuwa na viwanda vyake .
Pia Tanzania ina malighafi zote kutengeneza hata seti za televisheni, vioo vya madirisha na balbu.
Kuna mambo matatu makuu ambayo sisi binadamu twapaswa kufahamu.
Mambo hayo ni technical know what, technical know how and technical know why.
Darasani mwalimu hutufundisha kuhusu somo la jiografia, kisha kuingia ndani kufanya tathmini kutumia kifaa maalum cha Compass kwa kutumia ramani na hiyo ni technical how.
Pale uanzapo kujiuliza hii Compas imetengezwa vipi ndipo unapoingia kwenye technical know why.
Mabeberu wanakuambia kuwa Afrika kuna dhahabu tatu ambazo ni Tanzania, Angola na Congo DRC.
Mabeberu wanaendelea kuziangalia nchi tatu ambazo nchi za Tanzania, Angola na Congo DRC ambazo wana malengo ya muda mrefu hadi miaka 50.
Katika nchi hizo ni Tanzania ambayo wao mabeberu wana uwezo wa kuingia na kujichotea maliasili watakavyo.
Kutokea bandari ya Lobito iliopo Benguela kupitia Lusaka, Lubumbashi ni ukanda maalum ulojaa madini, mafuta na madini ya uranium ambavyo ni malighafi muhimu kwa utengenezaji wa betri za magari, simu za mkononi na mabomu ya nyuklia na mitambo yake.
Lango kuu la kuingia kwenda huko ndani au (interior) na kutokea ni Bagamoyo na ni njia rahisi kuliko kuzunguka Cape Town.
Ila mabeberu hao wakadai kuwa watakuja kwa mazungumzo na ikiwa mazungumzo yatashindikana basi watatumia mbinu zozote kuhakikisha wanafanikiwa azma yao.
Wazungu hao wanasema kuwa Tanzania ni nchi ya kuingia na kutokea Afrika kupitia Bagamoyo. Pia wanasema kuwa asilimia 60 ya biashara ya meli kuanzia mwaka 2050 itakuwa ndani ya bahari ya Hindi na hiyo ndio itakuwa Ocean of the future.
Hivyo, meli yaweza kutoka bandari ya Lobito kupitia Dar-es-Salaam hadi mfereji wa Suez bila shida na kwa uharaka zaidi.
Na hivyo ndivyo mfalme Leopold wa pili wa Belgium alivyokubaliana na wakoloni wa kijerumani kujenga reli ya kati ambayo ingesafirisha bidhaa zote za malighafi kutoka katikati ya Tanzania na Afrika kuelekea bahari ya Hindi.
Mfalme huyo alikuwa akivuna zao la mpira na kulisafirisha kwenda Ulaya kutengeneza bidhaa mbalimbali kama matairi ya magari, baiskeli na zingine yaani alikuwa "supplier" mkubwa.
Moja ya viwanda vikubwa ambavyo mfalme huyo alikuwa akiviuzia malighafi ya mpira ni kiwanda kinachotengeneza bidhaa za Dunlop.
Waafrika wengi sana raia wa Congo walikufa wakivuna zao hilo na wengine kukatwa mikono kwa kushindwa kufanya hivyo.
Bahari ya Hindi ni bahari ilojaaliwa kila aina ya maliasili kuanzia mafuta, gesi asilia na uranium. Leo hii twashuhudia jinsi magaidi wa kupandikizwa nchini Msumbiji wakitumika kama kivuli cha wizi wa maliasili hizi zinazoibwa usiku na mchana.
Mwandishi Robert Kaplan katika kitabu chake cha Monsoon - "The India Ocean and Future of American Power" anaitaja bahari ya Hindi kama New Great Game kama ndo njia ya China ikitumia meli zake kubwa za mafuta kusaka maliasili hiyo ndani ya bahari ya Hindi.
Lakini safari hii upo uwezekano mkubwa wa vita ndani ya bahari hiyo baina ya nch iza kibeberu yaani Marekani na China.
Kaplan anaelezea muungano wa nchi za Marekani, China na India katika bahari ya Hindi katika kufanya biashara, kuzuia vitendo vya utekaji meli yaani Piracy, kulinda njia za usafiri wa meli na kuitikia wito wa majanga ndani ya bahari hiyo.
Bila shaka kelele za ujenzi wa bandari ya Bagamoyo ni moja ya vielelezo vya mpango wa nchi za kibeberu.
Mkataba wa ujenzi wa bandari ya Bagamoyo ulofumuliwa na hayati John Magufuli haukuwa mkataba uloweka maslahi ya taifa mbele na ulikuwa ni wa miaka 99.
Mkataba huo pia haukuwa unaruhusu maendelezo yoyote ya bandari zingine kama bandari ya Dar-es-Salaaam, Tanga, Zanzibar.
Hiyo ni kwasababu Bagamoyo ndo lango kuu la kuingiza na kutoa rasilimali zote zinatoka ndani ya Tanzania na maliasili zingine zinazotoka ndani ya Congo DRC na Angola.
Kwa vile nchi za kibeberu tayari wana ramani ya Afrika na sehemu zilipo maliasili basi Tanzania pamoja na Angola na Congo DRC na wanafahamu kuwa sasa hivi ujazo wa Uranium na madini mengine umefikia kiwango cha juu kiasi cha kuweza kuvunwa, basi sisi hatuna ujanja.
Tanzania tunapaswa kueleza wazi msimamo wetu na pia kueleza ni nini tunataka kwani mali tunayo.
Tanzania haina budi kulinda ukanda wa bahari ya Hindi hadi Msumbiji kuhakikisha usalama wake hauingiliwi kirahisi. Serikali pia inawajibika kueleza msimamo wake kuhusiana na mkataba wa ujenzi wa bandari ya Bagamoyo.
Lakini si kuanza kuzunguka mbali na kuanza mijadala ya kupoteza muda huku tayari wenzetu wachache wamekaa tayari na mabeberu na wamepanga nini kinachofuata.
La sivyo tunakubali kuwa sie ni waangalizi tu wa rasilimali tulozikalia na tupo tayari kuzigawa bure au kwa ujira kiduchu.