Nchi za dunia ya tatu tuna safari ndefu sana katika kusimamia utawala wa sheria

sammosses

JF-Expert Member
Jan 24, 2011
1,682
1,110
Jana nimefuatilia impeachment abuse of power zikiwakilishwa hoja za kumuondoa rais Trump madarakani, nimekiri bado Waafrika wana Safari ndefu kuishi kwenye utawala wa sheria.

Ushahidi wa matumizi mabaya ya madaraka uliwasilishwa kwa hoja nzito,ukiwepo tuhuma mbali mbali za rushwa.

Pamoja na upinzani mkali wa kihoja kwa pande zote mbili republican na democratic wote wanakiri kuwa rais hayupo juu ya sheria.

Wakati democratic wanaamini kuwa rais anajiona yupo juu ya sheria ndiyo maana anatumia madaraka yake vibaya hali itakayo athiri national security. Republican hawaamini kuwa yupo juu ya sheria kwa kuwa alichokifanya utekelezaji wa majukumu yake.

#Hojayangu

Uwazi huu wa kumkosoa na kutokuwa na imani na Rais kwa kutumia madaraka yake vibaya, waafrika hatuna ubavu huo.

Wenzetu Rais ni mtumishi wa umma ana wajibika kwa maslahi ya umma pia, akienda kinyume wana vyombo vyenye mamlaka ya kumhoji ambavyo huku kwetu ni bunge.

Ukisoma katiba yetu kuna mgawanyo wa madaraka katika mihimili mitatu,ambayo ni Bunge,serikali na mahakama.

Mwingiliano uliopo ni mkubwa sana na mhimili unaonekana kuhodhi mamlaka ya mihimili mingine ni serikali.

Leo Rais anaweza kumuagiza speaker wa bunge kufanya jambo, na bunge likaona sawa.

Serikali inaweza kulidhoofisha bunge kwa kuwa tu rais ambaye ndiye mwenyekiti wa chama kinachoongoza dola ana mamlaka ndani ya chama kumpitisha speaker kuwa mgombea wa ubunge na mgombea wa kiti cha speaker kupitia chama chake kama zawadi ili kukidhi matakwa ya chama na rais bila kudhibitiwa na chombo chochote.

Hali hii imetokea kwa speaker kuwatishia wabunge tena bungeni kuwa wasipopitisha bajeti ya serikali rais atavunja bunge,ana uhakika wabunge wengi hawatarudi hususani wa chama chake.

Haya ni matumizi mabaya ya madaraka, ni rushwa ya kimamlaka kwa wabunge wanao toka ndani ya chama chao wakihofia kulinda ubunge.

Wanao umia ni wananchi kwa kuwa wanapoteza national security yao kwa maslahi ya watu wachache wenye malengo ya kung'ang'ania madaraka na kugawana vyeo.

Rais akiongea na waandishi wa habari mara baada ya kuingia madarakani, akijibu swali la separation of power, alisema serikali ndiyo mhimili mkuu ambao unaweza kuingilia mipaka ya mihimili.

Kwa majibu hayo hata kama rais ni sehemu ya bunge alipaswa kuheshimu na kuilinda katiba aliyoapa kuilinda na kuhifadhi.

Kilicho fanyika kwenye kikao cha Congress hapo jana kinapaswa kuwa fundisho kwa nchi zetu za dunia ya tatu.

Ili viongozi wa Afrika wasimamie maslahi ya wananchi, lazima tuwe na vyombo madhubuti visivyo hofia nguvu ya dola kwa maslahi ya wananchi.

Tuna bezwa sana kuwa tuna tumia mamlaka tuliyopewa na wananchi kubadili katiba zetu kwa maslahi binafsi.

Tupo kwenye karne ya 21 bado tawala zetu hazina mwelekeo tunaongozwa kwa mujibu wa nini. Tuamke saa ya mabadiliko ni sasa.
 
Check and balance of our three pillars hatuna.Mfumo wa uongozi wa Tanzania ni wa safeguard mfumo wa chama kimoja,ndio maana hawapendi kugusa katiba inayowapa madaraka ya kifalme ibadirishwe.Wakati ndio utaongea.Maana hata Mwalimu Nyerere alikuwa anakwenda na wakati alikuwa anapenda siasa za ujamaa zinazojikita mfumo chama kimoja .Lakini aliona mbali kuwa siasa ubadilika akaweka mfumo wa vyama vingi wenye uwezo wa kumudu check and balance system.
 
Yaani kwa sasa kila wanachofanya kwenu kipo sahihi mnataka kulinganisha na huku....Hivi hii kasumba ya kuji- undermine ss waafrika itaisha lini..? Kwa nn msichukulie mfano kwa nchi za Africa zilizo vizuri kama Africa kusini.....?
Yaani mara marekani cjui uingereza.... Hii inferiority haita isha kwetu wallahi
 
Kuna watanzania wengine utawasikia wanalinganisha US na Tz.......wakati ni opposite
 
Ukileta hayo kwetu rais atakuwa anaondoshwa kila mara maana tuna wivu. Ona jinsi kila kitu afanyacho Magufuli kinavyopingwa na Chadema. Hapa kuna atoke niingie mie nile
 
Kwani hatuwezi kuzungumzia mustakabali wa jambo bila ushabiki wa kisiasa.hukuzaliwa na chama but ulizaliwa Tanzania
 
Yaani kwa sasa kila wanachofanya kwenu kipo sahihi mnataka kulinganisha na huku....Hivi hii kasumba ya kuji- undermine ss waafrika itaisha lini..? Kwa nn msichukulie mfano kwa nchi za Africa zilizo vizuri kama Africa kusini.....?
Yaani mara marekani cjui uingereza.... Hii inferiority haita isha kwetu wallahi
Kwa utawala usio zingatia sheria ndiyo sahihi! Tatizo we are thinking out of the box. Soma contents za mada
 
Kwa utawala usio zingatia sheria ndiyo sahihi! Tatizo we are thinking out of the box. Soma contents za mada
Tatizo reference zenu ndugu....Daily humu ni marekani,uingereza to tz...kuna nchi za kiafrika zipo vizuri kwenye hili....mfano bunge la S.A si juzi tu walimjadiri rais aliyekuwepo madarakani Zouma... Sometimes chukueni references huku huku kwetu... Kwanza haya mambo yanategemea na katiba ya nchi husika.... Hivyo kamwe Tanzania haitafanana na USA ...hakuna cha safari ndefu,hiyo safari yenyewe haipo.... Hata hao wazungu wenyewe wao kwa wao hawatafanana kamwe...
 
Tatizo reference zenu ndugu....Daily humu ni marekani,uingereza to tz...kuna nchi za kiafrika zipo vizuri kwenye hili....mfano bunge la S.A si juzi tu walimjadiri rais aliyekuwepo madarakani Zouma... Sometimes chukueni references huku huku kwetu... Kwanza haya mambo yanategemea na katiba ya nchi husika.... Hivyo kamwe Tanzania haitafanana na USA ...hakuna cha safari ndefu,hiyo safari yenyewe haipo.... Hata hao wazungu wenyewe wao kwa wao hawatafanana kamwe...
Mbona hata katiba zetu hatuzifuati, kwa kuwa hazina meno
 
Haha mkuu pointi yangu ni kwenye reference countries tu mkuu.... Hata hivyo ni vipengele gan vya katiba havifuatwi.....?
Katiba inafatwa.

Kama alivyoeleza hapo juu mleta mada, mambo aliyoeleza yote ndo katiba inayataka yafanyike na viongozi wanatimiza hiyo katiba.

Nakuongezea mfano, Kwa hizo nchi usizotaka kujilinganisha nazo kwa sababu i/complex Rais anaweza kukaa miaka 5 bila kuongeza wafanyakazi mshahara ambao upo kimkataba? hiyo sio matumizi ya mabaya ya madaraka? je, hii ni mbaya kuifanya rejea kwenye hayo mataifa usiyotaka kuyasikia kwa sababu sio mataifa toka Africa?
 
Jana nimefuatilia impeachment abuse of power zikiwakilishwa hoja za kumuondoa rais Trump madarakani, nimekiri bado Waafrika wana Safari ndefu kuishi kwenye utawala wa sheria.

Ushahidi wa matumizi mabaya ya madaraka uliwasilishwa kwa hoja nzito,ukiwepo tuhuma mbali mbali za rushwa.

Pamoja na upinzani mkali wa kihoja kwa pande zote mbili republican na democratic wote wanakiri kuwa rais hayupo juu ya sheria.

Wakati democratic wanaamini kuwa rais anajiona yupo juu ya sheria ndiyo maana anatumia madaraka yake vibaya hali itakayo athiri national security. Republican hawaamini kuwa yupo juu ya sheria kwa kuwa alichokifanya utekelezaji wa majukumu yake.

#Hojayangu

Uwazi huu wa kumkosoa na kutokuwa na imani na Rais kwa kutumia madaraka yake vibaya, waafrika hatuna ubavu huo.

Wenzetu Rais ni mtumishi wa umma ana wajibika kwa maslahi ya umma pia, akienda kinyume wana vyombo vyenye mamlaka ya kumhoji ambavyo huku kwetu ni bunge.

Ukisoma katiba yetu kuna mgawanyo wa madaraka katika mihimili mitatu,ambayo ni Bunge,serikali na mahakama.

Mwingiliano uliopo ni mkubwa sana na mhimili unaonekana kuhodhi mamlaka ya mihimili mingine ni serikali.

Leo Rais anaweza kumuagiza speaker wa bunge kufanya jambo, na bunge likaona sawa.

Serikali inaweza kulidhoofisha bunge kwa kuwa tu rais ambaye ndiye mwenyekiti wa chama kinachoongoza dola ana mamlaka ndani ya chama kumpitisha speaker kuwa mgombea wa ubunge na mgombea wa kiti cha speaker kupitia chama chake kama zawadi ili kukidhi matakwa ya chama na rais bila kudhibitiwa na chombo chochote.

Hali hii imetokea kwa speaker kuwatishia wabunge tena bungeni kuwa wasipopitisha bajeti ya serikali rais atavunja bunge,ana uhakika wabunge wengi hawatarudi hususani wa chama chake.

Haya ni matumizi mabaya ya madaraka, ni rushwa ya kimamlaka kwa wabunge wanao toka ndani ya chama chao wakihofia kulinda ubunge.

Wanao umia ni wananchi kwa kuwa wanapoteza national security yao kwa maslahi ya watu wachache wenye malengo ya kung'ang'ania madaraka na kugawana vyeo.

Rais akiongea na waandishi wa habari mara baada ya kuingia madarakani, akijibu swali la separation of power, alisema serikali ndiyo mhimili mkuu ambao unaweza kuingilia mipaka ya mihimili.

Kwa majibu hayo hata kama rais ni sehemu ya bunge alipaswa kuheshimu na kuilinda katiba aliyoapa kuilinda na kuhifadhi.

Kilicho fanyika kwenye kikao cha Congress hapo jana kinapaswa kuwa fundisho kwa nchi zetu za dunia ya tatu.

Ili viongozi wa Afrika wasimamie maslahi ya wananchi, lazima tuwe na vyombo madhubuti visivyo hofia nguvu ya dola kwa maslahi ya wananchi.

Tuna bezwa sana kuwa tuna tumia mamlaka tuliyopewa na wananchi kubadili katiba zetu kwa maslahi binafsi.

Tupo kwenye karne ya 21 bado tawala zetu hazina mwelekeo tunaongozwa kwa mujibu wa nini. Tuamke saa ya mabadiliko ni sasa.
Umeandika vizuri sana, ila demokrasia ipo Ulaya tu, Waafrika nature yetu ya ulafi na ubabe hakuta kaa kuwe na democracy kabisa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Katiba inafatwa.

Kama alivyoeleza hapo juu mleta mada, mambo aliyoeleza yote ndo katiba inayataka yafanyike na viongozi wanatimiza hiyo katiba.

Nakuongezea mfano, Kwa hizo nchi usizotaka kujilinganisha nazo kwa sababu i/complex Rais anaweza kukaa miaka 5 bila kuongeza wafanyakazi mshahara ambao upo kimkataba? hiyo sio matumizi ya mabaya ya madaraka? je, hii ni mbaya kuifanya rejea kwenye hayo mataifa usiyotaka kuyasikia kwa sababu sio mataifa toka Africa?
Swala ni moja...., tz ni tz,urusi ni urusi,us ni us, s.a ni s.a.....Vp leo warusi wakisema wamulike mwenendo wa nchi yao kwa kuchukulia reference ya marekani.... Hapo watapata vitu vingi tofauti sababu ni nchi mbili tofauti,background haziendani,ideology tofauti yaani haziendani hata kidogo.....Cha kufanya ni kugeukia katiba yetu inataka nn...kama kuna makosa madogomadogo yafanywayo na wakubwa tutumie njia sahihi according to our constitution.... On my side,there's no problem as well as the walfare of the people is concerned...
 
Tatizo reference zenu ndugu....Daily humu ni marekani,uingereza to tz...kuna nchi za kiafrika zipo vizuri kwenye hili....mfano bunge la S.A si juzi tu walimjadiri rais aliyekuwepo madarakani Zouma... Sometimes chukueni references huku huku kwetu... Kwanza haya mambo yanategemea na katiba ya nchi husika.... Hivyo kamwe Tanzania haitafanana na USA ...hakuna cha safari ndefu,hiyo safari yenyewe haipo.... Hata hao wazungu wenyewe wao kwa wao hawatafanana kamwe...
Botwasana nasikia pia wao wana demokrasia nzuri kiasi chake, japo rais wa sasa ni hayawani

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Unarahisisha sana mambo, kuna kiini macho kikubwa sana kinafanywa na hao Wazungu sema hauoni tu.

Usiamini mainstream media hats siku moja, ziko kwa ajili ya kukudanganya na kukupambaza ili uwaone wao ni Miungu.

Demokrasia ya Muzungu ni kiini macho hata kwa wao wenyewe kama ukielewa nini kinafanywa na Banksters!
 
Swala ni moja...., tz ni tz,urusi ni urusi,us ni us, s.a ni s.a.....Vp leo warusi wakisema wamulike mwenendo wa nchi yao kwa kuchukulia reference ya marekani.... Hapo watapata vitu vingi tofauti sababu ni nchi mbili tofauti,background haziendani,ideology tofauti yaani haziendani hata kidogo.....Cha kufanya ni kugeukia katiba yetu inataka nn...kama kuna makosa madogomadogo yafanywayo na wakubwa tutumie njia sahihi according to our constitution.... On my side,there's no problem as well as the walfare of the people is concerned...
Nahisi ukirudi kusoma uzi na ukaelewa muktadha wa mleta mada wala hutakaa ulalame juu ya rejea ya nchi.

Kilichojadiliwa kwenye uzi ni jinsi katiba ya hizo nchi usuzotaka kusikia zinavyolindwa zaidi ya kitu chochote wala cheo/madaraka ya mtu yeyote, kitu ambacho Tz tunalinda chama na vyeo vya watu kuliko katiba ya nchi inayotoa masirahi kwa wananchi wote.

Hii mada ukiisoma bila kukumbuka wewe ni chama fulani au unawapenda watawala fulani utaelewa mleta mada aliwaza nini hasa.
 
Botwasana nasikia pia wao wana demokrasia nzuri kiasi chake, japo rais wa sasa ni hayawani

Sent using Jamii Forums mobile app
Yah there are some African countries which practice well the so called democracy..... Why can't we use them as our reference?.... The problem comes when the American culture is admired by most people especially we Africans that sometime we highlight our countries under the US shadow.... And trust me,this inferiority will never end unless we decide to strongly change our minds.....
 
Back
Top Bottom