Lord Delamere in Kenya
JF-Expert Member
- Nov 26, 2018
- 2,898
- 5,988
Kuna watu wamekuwa wakinong'ona kuwa Taifa letu limelogwa na hivyo tutahangaika sana kama taifa kujiletea maendeleo. Nilikuwa siamini ila sasa nimeanza kuamini. Kwanini?
Kuna mambo fulani yanayoendelea kwenye siasa,uchumi,jamii yanavunja moyo sana.Lakini huku kwenye soka ni kabisaaa..!
Kabla sijaenda mbali nikupe sifa moja kati ya nyingi za wachawi: huwa hawapendi maendeleo na mafanikio.Kama ndugu zako ni wachawi,utawagundua utakapoanza kufanikiwa,sasa hivi huwezi kuwaelewa.
Ni hivi: Simba Sports Club imeonyesha mafanikio makubwa sana kwenye soka kwa miaka ya hivi karibuni na inaonekana ina nia ya kuelekea kwenye mafanikio makubwa zaidi. Ila cha ajabu kuna viongozi serikalini wenye dhamana ya soka letu wametokea kuichukia sana Simba SC.Si kwamba zamani waliwahi kuipenda,No! ila chuki zao dhidi ya Simba wameanza kuzidhihirisha baada ya Simba kuingia kwenye take-off stage ya mafanikio.
Nasema hivyo kwasababu;
1.Inakuwaje Simba SC ambayo imeliletea Taifa letu heshima kubwa ichukiwe na inyanyaswe huku serikali yote ikiwa kimya? (rejea suala la N-Cards). Nchi yetu isingekuwa na mindset ya kichawi Simba ilipaswa ipongezwe na ipewe support siyo kunyanyaswa.
2.Iweje Serikali na Media takribani zote wawe Pro-Yanga na kuiweka kando Simba? Kila kukicha ni kuipigia chapuo Yanga hii hii inayolidhalilisha taifa kwa 'kupigwa nao' na akina Kapumbu,Isaac Shamtompa na wenzake. Juzi tena ikafanyiziwa na Rivers United nyumbani kwetu na kuiaibisha nchi ila bado Media Houses zinawapa Yanga airtime ya kutosha kuliko Simba .Kama si kulogwa ni nini?
3.Ni Simba SC ndio imesababisha leo tuna vilabu 4 vinavyotuwakilisha kwenye michuano ya kimataifa.Haijawahi kutokea hii. Lakini watu wako kimya kana kwamba Simba haijafanya lolote katika hilo na bado wanaenda mbele kuinyanyasa Simba.
Simba ina bahati mbaya kuwepo Tanzania.Ni sawa na mtoto mwenye nyota ya mafanikio kuzaliwa katika familia ya kichawi...atafanikiwa kwa mbinde sana. Kuna wakati nimewaza:Simba nayo ikikata tamaa na hatimaye iachane na mipango mingine ya maendeleo iliyojiwekea (kwa sababu ya chuki dhidi yake) ndo tutapata maendeleo ya soka?
Kuishi ndani ya taifa lenye watu wenye roho za kichawi ni tatizo kubwa.KAMA WE UNAJIFANYA HUAMINI KAMA UCHAWI UPO NA UNAATHIRI MAENDELEO,UTAFIKIRI ULIZALIWA AMSTERDAM BADALA YA MSAMVU,HUWEZI KUNIELEWA. Ila nakushauri upatapo mafanikio usijifanye una huruma sana kwa ndugu zako kwa kuwapa misaada,utakufa mapema. Kama wazazi wake wanasemwa semwa ni 'wazee wa busara' usijaribu kuwajengea nyumba nzuri na kuhakikisha wanakula vizuri UTAKUFA MAPEMA uwaache ndugu zako wasio na mbele wala nyuma wakiishi maisha marefu.Uchawi haupendi mafanikio na Simba SC ina bahati mbaya kuwepo Tanzania.
Kuna mambo fulani yanayoendelea kwenye siasa,uchumi,jamii yanavunja moyo sana.Lakini huku kwenye soka ni kabisaaa..!
Kabla sijaenda mbali nikupe sifa moja kati ya nyingi za wachawi: huwa hawapendi maendeleo na mafanikio.Kama ndugu zako ni wachawi,utawagundua utakapoanza kufanikiwa,sasa hivi huwezi kuwaelewa.
Ni hivi: Simba Sports Club imeonyesha mafanikio makubwa sana kwenye soka kwa miaka ya hivi karibuni na inaonekana ina nia ya kuelekea kwenye mafanikio makubwa zaidi. Ila cha ajabu kuna viongozi serikalini wenye dhamana ya soka letu wametokea kuichukia sana Simba SC.Si kwamba zamani waliwahi kuipenda,No! ila chuki zao dhidi ya Simba wameanza kuzidhihirisha baada ya Simba kuingia kwenye take-off stage ya mafanikio.
Nasema hivyo kwasababu;
1.Inakuwaje Simba SC ambayo imeliletea Taifa letu heshima kubwa ichukiwe na inyanyaswe huku serikali yote ikiwa kimya? (rejea suala la N-Cards). Nchi yetu isingekuwa na mindset ya kichawi Simba ilipaswa ipongezwe na ipewe support siyo kunyanyaswa.
2.Iweje Serikali na Media takribani zote wawe Pro-Yanga na kuiweka kando Simba? Kila kukicha ni kuipigia chapuo Yanga hii hii inayolidhalilisha taifa kwa 'kupigwa nao' na akina Kapumbu,Isaac Shamtompa na wenzake. Juzi tena ikafanyiziwa na Rivers United nyumbani kwetu na kuiaibisha nchi ila bado Media Houses zinawapa Yanga airtime ya kutosha kuliko Simba .Kama si kulogwa ni nini?
3.Ni Simba SC ndio imesababisha leo tuna vilabu 4 vinavyotuwakilisha kwenye michuano ya kimataifa.Haijawahi kutokea hii. Lakini watu wako kimya kana kwamba Simba haijafanya lolote katika hilo na bado wanaenda mbele kuinyanyasa Simba.
Simba ina bahati mbaya kuwepo Tanzania.Ni sawa na mtoto mwenye nyota ya mafanikio kuzaliwa katika familia ya kichawi...atafanikiwa kwa mbinde sana. Kuna wakati nimewaza:Simba nayo ikikata tamaa na hatimaye iachane na mipango mingine ya maendeleo iliyojiwekea (kwa sababu ya chuki dhidi yake) ndo tutapata maendeleo ya soka?
Kuishi ndani ya taifa lenye watu wenye roho za kichawi ni tatizo kubwa.KAMA WE UNAJIFANYA HUAMINI KAMA UCHAWI UPO NA UNAATHIRI MAENDELEO,UTAFIKIRI ULIZALIWA AMSTERDAM BADALA YA MSAMVU,HUWEZI KUNIELEWA. Ila nakushauri upatapo mafanikio usijifanye una huruma sana kwa ndugu zako kwa kuwapa misaada,utakufa mapema. Kama wazazi wake wanasemwa semwa ni 'wazee wa busara' usijaribu kuwajengea nyumba nzuri na kuhakikisha wanakula vizuri UTAKUFA MAPEMA uwaache ndugu zako wasio na mbele wala nyuma wakiishi maisha marefu.Uchawi haupendi mafanikio na Simba SC ina bahati mbaya kuwepo Tanzania.