Nchi yenye nguvu zaidi kiteknolojia duniani inawezaje kujishusha hadi kuzikandamiza kampuni za nchi nyingine?

ldleo

JF-Expert Member
Jan 9, 2010
1,003
1,024
VCG211287007538.jpg

Katika siku ambayo Bunge la Marekani liliidhinisha uteuzi wa balozi mpya nchini China, serikali ya nchi hiyo kama kawaida yake ilitangaza kuziwekea vikwazo kampuni 34 za teknolojia za China kwa kisingizio cha “kutishia usalama wa taifa”, na kuziweka kampuni nyingine 8 za China kwenye “orodha hasi ya uwekezaji” kwa kushukiwa kuhusika na sekta ya jeshi.

Hii ni mara ya tatu kwa serikali ya Marekani kuchukua hatua kama hizi dhidi ya kampuni za teknolojia za China ndani ya miezi miwili. Mwezi Septemba mwaka huu, waziri wa biashara wa Marekani Gina Raimondo alisema nchi hiyo itaizuia China kupata teknolojia mpya ili kukwamisha maendeleo yake katika uvumbuzi. Ikifuata ahadi kwa makini, kama nchi yenye nguvu zaidi kiteknolojia duniani, Marekani inawezaje kujishusha hadi kuzikandamiza kampuni za nchi nyingine? Je, Marekani sasa inaogopa nini?

Hivi karibuni, Kituo cha Sayansi na Masuala ya Kimataifa cha Belfer cha Shule ya Harvard Kennedy, Marekani kilitoa ripoti yenye kichwa cha habari “ushindani mkuu kati ya China na Marekani katika karne ya 21”, ikisema China imechukua nafasi ya Marekani kama nchi namba moja duniani katika uzalishaji wa bidhaa za teknolojia, na tayari imeishinda Marekani katika teknolojia kama akili bandia, mtandao wa 5G, na nishati mpya na pengine itaipiku katika sekta nyingine katika muongo ujao.

Baada ya Vita Vikuu vya Pili vya Dunia, Marekani iliimarisha nafasi yake kama nchi yenye nguvu zaidi ya kimagharibi na kuvutia vipaji kutoka kote duniani kuhamia na kuishi nchini humo, ambao walichangia sana maendeleo ya teknolojia ya nchi hiyo. Baada ya kuzuka kwa mapinduzi ya tatu ya kiteknolojia, sekta mpya inayohusu teknolojia ya habari ililipuka nchini Marekani. Takwimu zimeonyesha kuwa kutoka mwaka 1970 hadi mwaka 2008, kiwango cha ukuaji wa uchumi wa Marekani kilikuwa zaidi ya 3% kwa muda mrefu, ambapo mapinduzi ya kiteknolojia yamechangia sana ukuaji huo wa uchumi.

Hata hivyo, katika miaka kumi iliyopita, Marekani imeachana na nafasi yake ya kutawala kiviwanda na kuelekeza mkazo wake wa kiuchumi kwenye sekta kama mambo ya fedha na huduma, na hivyo kusababisha kuporomoka kwa viwanda na kukwama kwa maendeleo ya matumizi ya teknolojia. Na baada ya kuchukua nafasi ya Marekani kama kiwanda cha dunia, China imeanza kuongeza uwekezaji katika sayansi na tekonolojia, na pengo la kiteknolojia kati yake na Marekani likapungua.

Mwaka 2020, uwekezaji wa jumla wa China kwenye Utafiti na Maendeleo R&D ulishika nafasi ya pili duniani kwa kufikia karibu dola za Kimarekani bilioni 375. Ripoti ya Viashiria vya Uvumbuzi Duniani ya mwaka 2021 iliyotolewa na Shirika la Haki Miliki Duniani WIPO inaonyesha kuwa nafasi ya China imepanda kwa miaka 9 mfululizo, kutoka nafasi ya 14 ya mwaka 2020 hadi 12 duniani, na kuwa nchi pekee yenye kipato cha kati miongoni mwa nchi 30 bora. Wakati huo huo, kwa mujibu wa Shirika hilo, mwaka jana, China ilishika nafasi ya kwanza duniani kwa kuchangia asilimia 45.7 ya maombi ya hataza duniani. Miongoni mwao, idadi ya maombi ya hataza yaliyotolewa na kampuni ya teknolojia ya Huawei, ambayo inachukuliwa na Marekani kuwa adui namba moja ilifikia 5,464, na kushika nafasi ya kwanza duniani kwa miaka 4 mfululizo.

Kama tunavyojua, matunda ya kiteknolojia yanapaswa kufaidisha binadamu wote, na yasiwe njia ya kuzuia au kudhibiti maendeleo ya nchi nyingine. Katika zama za utandawazi na mwelekeo wa kihistoria, China na Marekani zinapaswa kuwa na uhusiano wa kunufaishana. Maendeleo ya teknolojia ya China yanaweza kusaidia kutoa bidhaa na huduma za teknolojia ya hali ya juu kwa nchi nyingine, ikiwemo Marekani. Ukizingatia faida za kiuchumi, "kutochagua China" ni jambo lisilo la kiuchumi na pia ni vigumu sana.

Ni kweli kwamba mnyororo wa ugavi ukikatika ghafla, kampuni yoyote itakumbwa na matatizo. Lakini hatua hizi za serikali ya Marekani zitachochea tu kampuni za China kujitafutia maendeleo katika sekta zinazokaba shingo, na matokeo yatakuwa China kupata maendeleo zaidi ya teknolojia, huku kampuni za Marekani zikipoteza soko kubwa la sasa. Muhimu zaidi, kuichukulia China kama "adui wa kufikirika" hakuwezi kuongeza ushindani wa kiteknolojia wa Marekani.
 

Katika siku ambayo Bunge la Marekani liliidhinisha uteuzi wa balozi mpya nchini China, serikali ya nchi hiyo kama kawaida yake ilitangaza kuziwekea vikwazo kampuni 34 za teknolojia za China kwa kisingizio cha “kutishia usalama wa taifa”, na kuziweka kampuni nyingine 8 za China kwenye “orodha hasi ya uwekezaji” kwa kushukiwa kuhusika na sekta ya jeshi.

Hii ni mara ya tatu kwa serikali ya Marekani kuchukua hatua kama hizi dhidi ya kampuni za teknolojia za China ndani ya miezi miwili. Mwezi Septemba mwaka huu, waziri wa biashara wa Marekani Gina Raimondo alisema nchi hiyo itaizuia China kupata teknolojia mpya ili kukwamisha maendeleo yake katika uvumbuzi. Ikifuata ahadi kwa makini, kama nchi yenye nguvu zaidi kiteknolojia duniani, Marekani inawezaje kujishusha hadi kuzikandamiza kampuni za nchi nyingine? Je, Marekani sasa inaogopa nini?

Hivi karibuni, Kituo cha Sayansi na Masuala ya Kimataifa cha Belfer cha Shule ya Harvard Kennedy, Marekani kilitoa ripoti yenye kichwa cha habari “ushindani mkuu kati ya China na Marekani katika karne ya 21”, ikisema China imechukua nafasi ya Marekani kama nchi namba moja duniani katika uzalishaji wa bidhaa za teknolojia, na tayari imeishinda Marekani katika teknolojia kama akili bandia, mtandao wa 5G, na nishati mpya na pengine itaipiku katika sekta nyingine katika muongo ujao.

Baada ya Vita Vikuu vya Pili vya Dunia, Marekani iliimarisha nafasi yake kama nchi yenye nguvu zaidi ya kimagharibi na kuvutia vipaji kutoka kote duniani kuhamia na kuishi nchini humo, ambao walichangia sana maendeleo ya teknolojia ya nchi hiyo. Baada ya kuzuka kwa mapinduzi ya tatu ya kiteknolojia, sekta mpya inayohusu teknolojia ya habari ililipuka nchini Marekani. Takwimu zimeonyesha kuwa kutoka mwaka 1970 hadi mwaka 2008, kiwango cha ukuaji wa uchumi wa Marekani kilikuwa zaidi ya 3% kwa muda mrefu, ambapo mapinduzi ya kiteknolojia yamechangia sana ukuaji huo wa uchumi.

Hata hivyo, katika miaka kumi iliyopita, Marekani imeachana na nafasi yake ya kutawala kiviwanda na kuelekeza mkazo wake wa kiuchumi kwenye sekta kama mambo ya fedha na huduma, na hivyo kusababisha kuporomoka kwa viwanda na kukwama kwa maendeleo ya matumizi ya teknolojia. Na baada ya kuchukua nafasi ya Marekani kama kiwanda cha dunia, China imeanza kuongeza uwekezaji katika sayansi na tekonolojia, na pengo la kiteknolojia kati yake na Marekani likapungua.

Mwaka 2020, uwekezaji wa jumla wa China kwenye Utafiti na Maendeleo R&D ulishika nafasi ya pili duniani kwa kufikia karibu dola za Kimarekani bilioni 375. Ripoti ya Viashiria vya Uvumbuzi Duniani ya mwaka 2021 iliyotolewa na Shirika la Haki Miliki Duniani WIPO inaonyesha kuwa nafasi ya China imepanda kwa miaka 9 mfululizo, kutoka nafasi ya 14 ya mwaka 2020 hadi 12 duniani, na kuwa nchi pekee yenye kipato cha kati miongoni mwa nchi 30 bora. Wakati huo huo, kwa mujibu wa Shirika hilo, mwaka jana, China ilishika nafasi ya kwanza duniani kwa kuchangia asilimia 45.7 ya maombi ya hataza duniani. Miongoni mwao, idadi ya maombi ya hataza yaliyotolewa na kampuni ya teknolojia ya Huawei, ambayo inachukuliwa na Marekani kuwa adui namba moja ilifikia 5,464, na kushika nafasi ya kwanza duniani kwa miaka 4 mfululizo.

Kama tunavyojua, matunda ya kiteknolojia yanapaswa kufaidisha binadamu wote, na yasiwe njia ya kuzuia au kudhibiti maendeleo ya nchi nyingine. Katika zama za utandawazi na mwelekeo wa kihistoria, China na Marekani zinapaswa kuwa na uhusiano wa kunufaishana. Maendeleo ya teknolojia ya China yanaweza kusaidia kutoa bidhaa na huduma za teknolojia ya hali ya juu kwa nchi nyingine, ikiwemo Marekani. Ukizingatia faida za kiuchumi, "kutochagua China" ni jambo lisilo la kiuchumi na pia ni vigumu sana.

Ni kweli kwamba mnyororo wa ugavi ukikatika ghafla, kampuni yoyote itakumbwa na matatizo. Lakini hatua hizi za serikali ya Marekani zitachochea tu kampuni za China kujitafutia maendeleo katika sekta zinazokaba shingo, na matokeo yatakuwa China kupata maendeleo zaidi ya teknolojia, huku kampuni za Marekani zikipoteza soko kubwa la sasa. Muhimu zaidi, kuichukulia China kama "adui wa kufikirika" hakuwezi kuongeza ushindani wa kiteknolojia wa Marekani.
We mchina wacha kulia lia. Wawekeni vikwazo na nyie.
 
Back
Top Bottom