Phillipo Bukililo
JF-Expert Member
- Dec 29, 2015
- 18,489
- 13,608
Jana taarifa ya habari ya ITV imeonyesha hasara waliyopata wamiliki wa shamba la miwa huko Mtibwa. Kwa mujibu wa aliyehojiwa ambaye inaonekana ni msimamizi wa shamba hilo, hasara waliyopata ni ya shilingi milioni 800.
Wingi wa miwa ambayo ingevunwa na kuingizwa kwenye mchakato wa upatikanaji wa sukari, kwa namna moja au nyingine ungesababisha kushuka kwa bei ya bidhaa hiyo muhimu.
Hapa tunaongelea hasara waliyopata Mtibwa, hatujaongelea mateso wanayopata wakulima wengine wengi tu wenye kutumia nguvu nyingi katika kulima na kupanda mazao halafu ghafla tu ng'ombe wanaingia na kuharibu kila kitu.
Haipendezi hata kidogo kuona nchi nzima inageuzwa kuwa mali ya wafugaji na mifugo yao. Natambua ukame wa baadhi ya maeneo ya wafugaji. Kwa kukatiza tu na gari pale Monduli mtu anauona ukame halisi, hapo bado haujatembea katika maeneo mengine yenye shida kubwa sana ya maji na nyasi.
Waziri wa kilimo na wasaidizi wako, tunakoelekea kwenye nchi ya viwanda, tunakwenda kwenye maisha ambayo wawekezaji wa ndani ya wa nje hawatakubaliana na hasara zitakazotokana na uholela wa uchungaji ambao umekuwa na mateso makubwa kwa wakulima wasio na hatia.
Lifanyike jambo na lifanyike mapema iwezekanavyo. Leo Mtibwa wanadai kuingia hasara ya milioni 800, kesho atakuja muwekezaji na kudai kupata hasara ya mabilioni ya shilingi na hatakubaliana na majibu yoyote ya kutaka kumridhisha ili suala liweze kumalizika kwa amani.
Wingi wa miwa ambayo ingevunwa na kuingizwa kwenye mchakato wa upatikanaji wa sukari, kwa namna moja au nyingine ungesababisha kushuka kwa bei ya bidhaa hiyo muhimu.
Hapa tunaongelea hasara waliyopata Mtibwa, hatujaongelea mateso wanayopata wakulima wengine wengi tu wenye kutumia nguvu nyingi katika kulima na kupanda mazao halafu ghafla tu ng'ombe wanaingia na kuharibu kila kitu.
Haipendezi hata kidogo kuona nchi nzima inageuzwa kuwa mali ya wafugaji na mifugo yao. Natambua ukame wa baadhi ya maeneo ya wafugaji. Kwa kukatiza tu na gari pale Monduli mtu anauona ukame halisi, hapo bado haujatembea katika maeneo mengine yenye shida kubwa sana ya maji na nyasi.
Waziri wa kilimo na wasaidizi wako, tunakoelekea kwenye nchi ya viwanda, tunakwenda kwenye maisha ambayo wawekezaji wa ndani ya wa nje hawatakubaliana na hasara zitakazotokana na uholela wa uchungaji ambao umekuwa na mateso makubwa kwa wakulima wasio na hatia.
Lifanyike jambo na lifanyike mapema iwezekanavyo. Leo Mtibwa wanadai kuingia hasara ya milioni 800, kesho atakuja muwekezaji na kudai kupata hasara ya mabilioni ya shilingi na hatakubaliana na majibu yoyote ya kutaka kumridhisha ili suala liweze kumalizika kwa amani.