Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,470
- 911,172
Jumla ya mawaziri 14 hivi hadi sasa yasadikiwa wamepoteza viti vyao lakini kila mahali wakubwa hao wanakataa matokeo na kutaka kura zihesabiwe upya!!!!!!!!!!!!!!......
Katika sheria ya uchaguzi ni kwa amri ya mahakama tu ndiyo unaweza kupita kibali cha kurudia kuzihesabu kura tena lakini viongozi wa CCM serikalini wanatumia madaraka yao kushinikiza wasimamizi wa majimbo ya chaguzi ambao ni wadogo wao kiajira kurudia kuzihesabu kura kinyume na sheria.............
Swali la kujiuliza hivi ni kwa nini CCM wanaamini mwaka huu kura zimekosewa kuhesabiwa na kwa nini hawasubiri matokeo yatangazwe kama sehemu nyingine ambazo wamefanya vizuri?
Yaelekea NEC inapoona CCM imeshindwa ipo tayari kurudia kuhesabu kura ili kuyachakachua matokeo ya ridhaa ya wananchi na hili huenda likaielekeza nchi kwenye vita vya wenyewe kwa wenyewe........Ni lazima wasiwasi uwepo wa usalama wa maboksi vinginevyo CCM wasingeshupalia kura zihesabiwe tena yaani hata mawakala wao waliowaweka wenyewe hata hawaamini tena...........
Wapo wanaona ya kuwa kama majemedari wa JK wataonekana wameanguka itakuwa vigumu kwa serikali ya CCM kumtangaza Jk kibabe kuwa ameshinda na hivyo ni lazima watumie nguvu ya dola kuhakikisha ya kuwa majemedari wake ambao ni mawaziri wanakubalika na jamii jambo ambalo siyo kweli hata kidogo ...........
Kukosekana kwa NEC kuwa na waajiriwa wa kudumu kumechangia katika serikali ya CCM kuvuruga riidhaa ya wananchi kwa kuwatumia watendaji wa serikali za mitaa hususani Ma-DED.....katika kuchakachua ridhaa ya wapigakura
Katika sheria ya uchaguzi ni kwa amri ya mahakama tu ndiyo unaweza kupita kibali cha kurudia kuzihesabu kura tena lakini viongozi wa CCM serikalini wanatumia madaraka yao kushinikiza wasimamizi wa majimbo ya chaguzi ambao ni wadogo wao kiajira kurudia kuzihesabu kura kinyume na sheria.............
Swali la kujiuliza hivi ni kwa nini CCM wanaamini mwaka huu kura zimekosewa kuhesabiwa na kwa nini hawasubiri matokeo yatangazwe kama sehemu nyingine ambazo wamefanya vizuri?
Yaelekea NEC inapoona CCM imeshindwa ipo tayari kurudia kuhesabu kura ili kuyachakachua matokeo ya ridhaa ya wananchi na hili huenda likaielekeza nchi kwenye vita vya wenyewe kwa wenyewe........Ni lazima wasiwasi uwepo wa usalama wa maboksi vinginevyo CCM wasingeshupalia kura zihesabiwe tena yaani hata mawakala wao waliowaweka wenyewe hata hawaamini tena...........
Wapo wanaona ya kuwa kama majemedari wa JK wataonekana wameanguka itakuwa vigumu kwa serikali ya CCM kumtangaza Jk kibabe kuwa ameshinda na hivyo ni lazima watumie nguvu ya dola kuhakikisha ya kuwa majemedari wake ambao ni mawaziri wanakubalika na jamii jambo ambalo siyo kweli hata kidogo ...........
Kukosekana kwa NEC kuwa na waajiriwa wa kudumu kumechangia katika serikali ya CCM kuvuruga riidhaa ya wananchi kwa kuwatumia watendaji wa serikali za mitaa hususani Ma-DED.....katika kuchakachua ridhaa ya wapigakura