Elections 2010 Nchi iko mikononi mwenu wenye hekima na jaji lewis makame.

Mtaka Haki

JF-Expert Member
Oct 1, 2010
492
149
Hiki ni kipindi kigumu katika nchi yetu wakati tunapoendelea kusubiri matokeo ya kura.
Inahitajika wenye hekima kuitumia hekima na busara yao katika kuepusha utata na hisia zisizo na lazima.
Nawaomba viongozi wa dini na wenye hekima katika nchi hii msiendelee kusubiri dakika nyingine moja bila ya kuchukua hatua.

Namsihi mwenyekiti wa tume ya Taifa ya Uchaguzi, pamoja na ugumu mkubwa wa jukumu liloko mbele yake basi aingilie kati na kujaribu pale inapowezekana kuingilia kati mahali ambao sio lazima matokeo kuendelea kusubiriwa.
Kama kila mtu anavyojua matokeo yanapobandikwa ni rahisi wananchi kuyajumlisha na kupata matokeo yasiyo rasmi.

NI KWELI NCHI HII IKO MIKONONI MWA WENYE HEKIMA.
MAAMUZI YATAKAYOCHUKULIWA YATALIPONYA TAIFA AU KULIWEKEA DOA LISILOFUTIKA.
 
Back
Top Bottom