Duble Chris
JF-Expert Member
- May 28, 2011
- 3,481
- 564
i
- huku wanadai katiba mpya
- maandalizi ya kula bata kwa kisingizio cha miaka 50 ya uhuru
- Z'bar wanapanga maandamo ijumma hii hawaupendi kabisa muungano wetu
- CDM hawaingii bungeni wanasambaza sumu mbaya nje ya bunge juu ya katiba
- Wanaharakati wameegesha mtego wa kuandamana nchi nzima kupinga namna ya kuitafuta katiba ya ukweli
- Wabunge wamehama hoja wanajadili chama na mbunge badala ya hoja ya katiba
- Majembe imara yamelazwa INDIA ambayo yangesaidia kupunguza ghasia hizi japo kwa ushauri tu
- machinga nao hawaambiliki hata wakipigwa mabomu kiasi gani na wanasababisha gharama zisizo za lazima kuwatuliza
- wanafunzi wana dai mikopo/fedha kana kwamba hawajui yanayo ikabili hii nchi kwa wakati mmoja