MFIZIGO
JF-Expert Member
- Sep 30, 2014
- 374
- 232
Nasema tena nchi hii kuna uwezekano mkubwa haina wazee au ambao waliopo hawaelewi majukumu yao. Katika nchi au eneo lenye wazee mambo huwa hayaaribiki, hata yakiharibika huwa ni kwa muda tu.
Sasa ona hapa kwetu wazee wao wameamua kuwa kimya, nao wamekuwa waoga kama sisi vijana ambao hatujui lolote, wao ndiyo waliokuwa wakemeaji wa mambo haya yanayokwenda mrama sasa.
Au huenda wazee hawajapendezwa na suala la huyu mkuu wa kaya mpya? Kwa hiyo wanaona bora aharibu tu. Kweli katika nchi yenye wazee, uvunjwaji wa katiba unakaliwa kimya kiasi hiki?
Kweli katika nchi yenye wazee, watu wa nchi hiyo wanaishi huku hawaijui kesho yao? Kweli katika nchi yenye wazee, kila mtu ni mchochezi madamu tu unamkosoa 'sizonje'? Ona sasa wazee! Wawekezaji wanakimbia kwa sababu ya misimamo ya hovyo ya 'Sizonje' na hili nalo mmelikalia kimya?
Mnasubiri mpaka atangaze kukiuza chama chenu ndiyo muibuke mlipo na misuli yenu viunoni? Sisi vijana tunashindwa kumshauri kwa kuwa 'hatujui kitu', nyinyi mnajua kwa kuwa mlishapita huko aliko Sizonje.
Tusaidieni kuinusuru.
Sasa ona hapa kwetu wazee wao wameamua kuwa kimya, nao wamekuwa waoga kama sisi vijana ambao hatujui lolote, wao ndiyo waliokuwa wakemeaji wa mambo haya yanayokwenda mrama sasa.
Au huenda wazee hawajapendezwa na suala la huyu mkuu wa kaya mpya? Kwa hiyo wanaona bora aharibu tu. Kweli katika nchi yenye wazee, uvunjwaji wa katiba unakaliwa kimya kiasi hiki?
Kweli katika nchi yenye wazee, watu wa nchi hiyo wanaishi huku hawaijui kesho yao? Kweli katika nchi yenye wazee, kila mtu ni mchochezi madamu tu unamkosoa 'sizonje'? Ona sasa wazee! Wawekezaji wanakimbia kwa sababu ya misimamo ya hovyo ya 'Sizonje' na hili nalo mmelikalia kimya?
Mnasubiri mpaka atangaze kukiuza chama chenu ndiyo muibuke mlipo na misuli yenu viunoni? Sisi vijana tunashindwa kumshauri kwa kuwa 'hatujui kitu', nyinyi mnajua kwa kuwa mlishapita huko aliko Sizonje.
Tusaidieni kuinusuru.