Nchi bado ina uozo mwingi. SUA nako walamba Bilioni moja bila maelezo

Zygot

JF-Expert Member
Apr 14, 2016
2,238
2,866
Hivi karibuni kulikuwa na matangazo ya wizi wa pesa kupitia wanafunzi hewa wa vyuo vikuu. yaonekana hilo ni tone ktk tabia mbaya iliyoko vyuoni.

Maelezo yafuatayo, yametolewa kwenye mtandao wa chuo kikuu cha kilimo, SUA. Bahati mbaya kabisa wahusika ni wakuu wenyewe, sijui nani anapewa jukumu la kulinda mali ya umma chuoni.

Soma na kama kuna vyombo vinavyohusika fuatilieni ili nchi iende inavyotakiwa.

------------------------------------------------
Wale munaofuatilia yanayotokea hapa chuoni, munafahamu sekeseke linalotokea kwa sasa hadi watu wamepigiwa simu za vitisho ili waache kulizungumzia tatizo hilo. Kwa ujumla ni wizi mkubwa wa pesa za mradi wa NORAD uliokuwa kwenye ujenzi wa jengo la kitivo cha sayansi kule Mazimbu.

Takribani bilioni 1 imeliwa na watawala wetu. Jengo hili limekuwa likijengwa kwa miaka zaidi ya mitatu sasa. Ni jengo dogo lililopangwa liwe la gorofa tatu. Baada ya kupatikana pesa, likapunguzwa kuwa ni la gorofa mbili na mwishoni sasa limekuwa ni jengo la gorofa moja, lakini gharama yake imebaki kuwa ni ile ile!

Ni muendelezo wa miradi ya wizi pamoja na ile ya ujenzi wa kumbi mbili za mihadhara iliyochota zaidi ya bilioni 1.3, maktaba ya mazimbu iliyobomoka tangu siku ya kwanza, maabara ya zoolojia inayovuja hadi leo bila kutumika, chanzo pekee cha maji kilichotumia mabilioni wakati hadi leo watu wanakunywa tope, huku kukiwa na tenda feki za madawa kila mwaka, pia jengo la kilimo biashara ambalo leo hii limechakaa hata kabla ya miaka 4!

Pesa kama hizo kwa vyuo vingine linajengwa jengo kubwa na la maana sana.

Wakati Naibu katibu mkuu alipotembelea chuo hiki cha SUA, mwezi wa nne alielezwa ujenzi huo ulikuwa unaendelea vizuri na kufikia mwezi wa 6 jengo lingekamilika.

Leo hii Disemba jengo bado halijamalizika na pesa hazitoshi kwa kusingizia mabadiliko ya ujenzi ambayo hata hayastahili kutumia milioni 100, sasa chuo kinatafuta mabilioni kwa kisingizio kwamba ni kwa ajili ya kumalizia ujenzi wa jengo hili. Huu ndio mgogoro tulionao sasa hivi hapa chuoni tunaomba wote wanaousikia, waelewe.

Yaonekana nguvu ya Mh. Magufuli haijasikika vizuri hapa chuoni maana kwa taarifa tulizonazo toka ndani ya idara ya uhasibu SUA, pesa za jengo hili, viongozi wetu wamezigawana na zimeliwa kwa pamoja. Bila aibu naomba niwataje kama nilivyosimuliwa kwamba wafuatao ndiyo wamegawana pesa hizo.

Ikiwezekana wajitokeze kueleza sababu ya kuleta vitisho kwa wale wanaouliza upotevu huo wa pesa:

1. Mkuu wa chuo (VC) Prof. Monela amebeba sehemu ya pesa hizo, mlinzi mkuu wa mali ya chuo asiyefanya kazi yake

2. Naibu makamu mkuu wa chuo taaluma (DVC acad), Prof Gillah kila dili kwake ni safi tu

3. Msarifu (Barsar), ndg. Raphael na staf yake hadi kwa cashier wetu hawa ni walinzi wasiotaka kulinda pesa

4. Ofisi ya ugavi ilipewa mgao wa jumla Yaani Zumo na watu wake ambao ni wazoefu ktk dili

5. Afisa mipango, Masawe na watu wake ambao ni wazoefu kwa dili kama hizi

6. Ukaguzi wa mahesabu kwa akina Mulyomi pamoja na watu wake walipitisha kuwa ni malipo halali

7. Kurugenzi ya utafiti, pale Muhikambele alipewa na watu wake na hata messenger alipata.

8. Mkuu wa kitivo cha sayansi. Prof. Mwangingo ambaye amejitafuna mwenyewe jengo lake

Kuna watu wengine wawili ambao wanaonekana kufahamu dili hili na wanafahamu jinsi gani pesa hizo zimeliwa.

Tuna wasiwasi kwamba hata wao walipewa mgao. Hao ni:
1. Prof. Ishengoma
2. Prof. Kulwijila

Wawili hawa ni wahusika ktk mradi huo na hakika wanastahili kufahamu pesa ilivyochotwa.

Ndugu zangu hawa ndiyo viongozi wa chuo chetu cha SUA tunaodhani wanaendeleza chuo. Tunapohangaika kuongeza mapato ya chuo tuelewe viongozi wanaongeza wizi pia.

Sasa hivi juhudi zinazofanywa ni kuzuia mambo haya yasiende nje ya chuo na bahati mbaya wanatumia vitisho vya simu na kuna sehemu wamesikika wakitafuta pesa za kuhonga wale wanaodhani wanaweza kulitoa nje ya chuo.

Sisi wanajumuiya ya chuo tunasemaje? Waalimu tunasukumwa kufundisha kwa nguvu bila hata motisha wakati wenzetu wakichota pesa na kujenga mahoteli yasiyolingana na kipato chao. Ombi langu kwa watu hawa, warudishe pesa za jengo hili kwa gharama yoyote ile hata kama ni kuuza hoteli wanazojenga.

Habari hizi tunazifikisha TAKURU tukiomba watusaidie kueleza jinsi gani pesa imepotea kwa kisingizio kwamba zilirudishwa kwa wafadhili. Maana jengo la gorofa moja haliwezi kuwa na thamani ya bilioni 3. Hatutakubali kuwalea wezi. Bahati mbaya kabisa hata wastaafu tunaohitaji uzoefu wao mzuri kumbe wao wamezoea mengine kabisaa!

Haya ni maelezo ya wazi kwenu wahusika. Jitokezeni mueleze kwa nini jengo halijaisha na kwa nini gorofa moja itumie zaidi ya bilioni mbili kwa kisingizio cha maabara.

Magereza watajenga nyumba kibao za kuishi kwa bilioni 10 tu za Mh. Rais!
 
Mimi nasubiri majina ya wadaiwa mokopo maana kuna wale toka idara ya uvuvi walilipiwa na mradi Wa MACEMP na sua wakala dili na bodi ya mikopo wakachukuwa hela toka hesleb. Baada ya kuisha miaka 4 kuna wanafunzi waligundua wamebambikiwa mikopo na sijui kama nao majina yako yatatolewa kwamba ni wadaiwa. Nasubiri kwa hamu niwaumbue bodi. Jifanyeni mnatisha watu kuna wengine wali disco mkala hela zao miaka 5. Ndo maana tunataka muandike na kiwango wanachodaiwa.
 
Ndiyo maana malaika asiyejaribiwa anataka kuifungia JF kwa sababu hataki apewe habari kama hizi kupitia vyombo vya habari, anataka apewa Taarifa kama hizi kimyakimya ili afanye ziara ya kushitukiza akiwa na vyombo vya habari ili apate sifa yeye peke yake kwa kutumbua watu
 
Kosa linalofanyika ni kushirikisha hawa parrots/lecturers kwenye shughuli zinazohitaji accountability. Ninawafahamu baadhi they are crooks for sure na walichonacho ni uwezo wa kukramu tu na kutoa kama parrots.

Wizi ni wa siku nyingi hapo hata wakiandika miradi ikipata fedha wanafanyaga mali yao.

Yuko mmoja mstaafu alishaingia siasa hata kwa sangomba anaendaga mchawi!!

Tz profs! PCCB pls. The whistle has been blowed.
 
Ndiyo maana malaika asiyejaribiwa anataka kuifungia JF kwa sababu hataki apewe habari kama hizi kupitia vyombo vya habari, anataka apewa Taarifa kama hizi kimyakimya ili afanye ziara ya kushitukiza akiwa na vyombo vya habari ili apate sifa yeye peke yake kwa kutumbua watu
Kweli kabisa Mkuu...
Sifa za kijinga.
 
Kosa linalofanyika ni kushirikisha hawa parrots/lecturers kwenye shughuli zinazohitaji accountability. Ninawafahamu baadhi they are crooks for sure@@ na walichonacho ni uwezo wa kukramu tu na kutoa kama parrots.
Wizi ni wa siku nyingi hapo hata wakiandika miradi ikipata fedha wanafanyaga mali yao.
Yuko mmoja mstaafu alishaingia siasa hata kwa sangomba anaendaga@ mchawi!! Tz profs! PCCB pls. The whistle has been blowed.
Very correct!
SUA na UD vina watu ambao wamekuwa ni emperors. Wanadhani pesa ya chuo ni yao na wao ni chuo! Mobutu-style.

Kuna hali nisiyoielewa kwa Mh. Rais. Inaonekana kama anawapa heshima sana viongozi wa vyuo hivi! Hali ilivyo hawastahili kabisa kuheshimika. Kwa uzoefu wangu, kuna wengi wasiokuwa ktk uongozi ktk vyuo hivi ndo watu wema kabisa kuliko walioko kwenye uongozi. Uongozi wa vyuo vingi ulishakuwa ni uhuni tuuu!

Hapo SUA, nasikia mkuu wao hapiti njia moja na wafanyakazi wengine kuingia ofisini akiogopa kulogwa! Huyo akipeleke wapi chuo kikuu? he is just another hunter and gatherer:)
 
Nawasubiri waje waninyang'anye chupa yangu ya bia

Idara ya maji wamemletea kijana wangu eti mdaiwa na wamemwambia kama si mnufaika aandike barua haraka kwa mkurugenzi ya kukunusha. Mbona bodi hawasisitizi maafisa wao waliokula hela za wanafunzi hewa nao watolewe majina na picha?

Nina hamu na hesleb wajichanganye. Mawakili kaeni mkao Wa kula kuna ushahidi Wa kutosha na usio na shaka.
 
...............................................................

Haya ni maelezo ya wazi kwenu wahusika. Jitokezeni mueleze kwa nini jengo halijaisha na kwa nini gorofa moja itumie zaidi ya bilioni mbili kwa kisingizio cha maabara. Magereza watajenga nyumba kibao za kuishi kwa bilioni 10 tu za Mh. Rais!
Haya maelezo ya mwisho yanakera sana juu ya tabia ya wajenzi. Rais ametoa bilioni 10 kwenda UD kwa ujenzi wa hosteli 20 za gorofa 4 kila moja. Iikimaanisha ni milioni 500 kwa kila jengo lenye gorofa 4. Inakuwaje hilo jengo lenu moja lijengwe kwa bilioni zaidi ya 2? Au ni kubwa kama makao ya Papa Francis?

Kuna mtu kanidokezea kwamba vyuo vimekuwa vikiiba kwa mtindo wa double payment. Donor anawapa pesa na wakati huo huo wanaomba pesa kwa donor mwingine au serikalini kwa ujenzi huo huo!!! Rubbish people!
 
Yale Makabila makubwa yote niliyoyategemea yawepo kwenye huu wizi nimeyakuta, Mwangingo, Massawe, Ishengoma, eti wasomi waliostaaribika sisi wengine tunawaonea wivu "wanamaendeleo" hao wa mikoani kawo. MIJIZI MIKUBWA NYIE... yani kila kashfa nyie tu afu mnalilia mpewe nchi Famvafv Thana
 
Daahh SUA hatarii ,pia kuna mradi wa kule Magadu lile bwawa la umwagiliaji yaani , embarkment haiieleweki na watu wameshakula hela
 
Takukuru mfanyie kazi hii taarifa kwa nguvu zote, yaliyosemwa humu hamna la uongo, ni kweli tupu!!
Kuna ile barabara inayotokea new hostel kupitia jengo fake la agribusiness imeishia nusu million 400 zikaishia kusikojulikana
 
Takukuru mfanyie kazi hii taarifa kwa nguvu zote, yaliyosemwa humu hamna la uongo, ni kweli tupu!!
Kuna ile barabara inayotokea new hostel kupitia jengo fake la agribusiness imeishia nusu million 400 zikaishia kusikojulikana
Jamani! hiki ni Chuo au kambi ya wezi? Kwa nini PCCB hawachunguzi mambo kama haya? Au mpaka rais azungumzie mambo haya?
 
Yale Makabila makubwa yote niliyoyategemea yawepo kwenye huu wizi nimeyakuta, Mwangingo, Massawe, Ishengoma, eti wasomi waliostaaribika sisi wengine tunawaonea wivu "wanamaendeleo" hao wa mikoani kawo. MIJIZI MIKUBWA NYIE... yani kila kashfa nyie tu afu mnalilia mpewe nchi Famvafv Thana
"KAZI YA KABILA NI KUTAMBIKA TU".-BY JK.NYERERE.


ANGALIA USIPOTEE KWENYE DHIMA YA HUU UZI.
i think HICHO KIPENGELE CHA MAKABILA UNGEKIKOPI NA KU-paste kwenye uzi wa ukabila kisha ukijadili.
dont forget...innocent till proven guilty.

back to.topic
sua imejaa majambazi hadi hao marais wa chuo wanawaibia wanafunzi pesa zao
 
Takukuru mfanyie kazi hii taarifa kwa nguvu zote, yaliyosemwa humu hamna la uongo, ni kweli tupu!!
Kuna ile barabara inayotokea new hostel kupitia jengo fake la agribusiness imeishia nusu million 400 zikaishia kusikojulikana
Wiki ijayo napita Morogoro. Nitaingia maeneo hayo nijionee vituko vya wasomi wa nchi hii. Si wamesoma?
 
Back
Top Bottom