nngu007
JF-Expert Member
- Aug 2, 2010
- 15,862
- 5,797
[h=2][/h]JUMANNE, MEI 22, 2012 05:42 NA ABDALLAH AMIRI, NZEGA
KATIBU wa Fedha na Uchumi wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Mwigulu Nchemba, amesema CCM ni chama kikubwa hakiwezi kutetereka na kutegemea walimu ili kishinde chaguzi.
Nchemba aliyasema hayo jana wakati akitoa ushahidi wa upande wa mdaiwa katika kesi ya kupinga matokeo ya ubunge wa Mbunge wa Igunga, Dk. Dalaly Kafumu (CCM). Kesi hiyo ilifunguliwa na Mgombea wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Joseph Kashindye.
Akitoa ushahidi katika Mahakama Kuu, Kanda ya Tabora, Mjini Nzega, Nchemba ambaye pia Mbunge wa Iramba Magharibi (CCM), alikanusha tuhuma za kutoa rushwa kwa walimu katika eneo la Nkinga pamoja na kutoa lugha ya matusi katika baadhi ya mikutano ya kampeni.
Nchemba ambaye alikuwa Kiongozi Mkuu wa Kampeni za CCM, aliieleza Mahakama hiyo, kuwa chama hicho kilitenga Sh milioni 402 kwa ajili ya shughuli nzima ya kampeni.
Awali, Wakili wa Mlalamikaji, Profesa Abdallah Safari, alieleza Mahakama kuwa, September 16 mwaka jana, Nchemba alikutana na walimu na kuwashawishi waipigie kura CCM ili kukinusuru kisianguke pamoja na kuwagawia fedha walimu 70 katika eneo la Shule ya Msingi Nkinga iliyoko Igunga.
Akijibu hoja hiyo, Nchemba alikana kuhusika na utoaji wa pesa ndogo ndogo, kwa walimu hao na kusema kuwa yeye husaini hundi katika chama hicho.
Mimi sihusiki na viji-petty cash, nahusika na kusaini akaunti kubwa, hivyo vijipetty cash vina wenyewe kama nilivyotaja hapo mwanzo,alisema Nchemba.
Kwa mujibu wa Nchemba, chama hicho hakiwezi kunusuliwa na kikundi cha walimu bali kinanusuliwa na wanachama wa CCM waliopo sehemu mbalimbali nchini wakiwamo wa Igunga.
Huwezi kumpatia shetani neno la Mungu akahubiri, ni jambo ambalo ni gumu sana, alisema Nchemba akiwalenga walimu kulingana na swali aliloulizwa na Profesa Safari.
Mwanzoni, Nchemba wakati akijitambulisha, alidai CCM ina fedha nyingi na yeye ni Bwana Fedha wa chama hicho, kauli ambayo ilisababisha wananchi waliofurika mahakamni hapo kuguna.
Hata hivyo, Jaji Mery Shangali anayesikiliza shauri hilo, alimtaka mbunge huyo kuheshimu Mahakama kwa kutotumia lugha zisizostahili.
Wakati huo huo Mahakama hiyo ilikataa ushahidi wa shahidi wa 18 ambaye ni Ofisa Mtendaji, Kata ya Igunga, Fedrick Magaka kutokana na shahidi huyo kuhudhuria baadhi ya vikao vya kesi hiyo. Kesi hiyo itaendelea leo.
KATIBU wa Fedha na Uchumi wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Mwigulu Nchemba, amesema CCM ni chama kikubwa hakiwezi kutetereka na kutegemea walimu ili kishinde chaguzi.
Nchemba aliyasema hayo jana wakati akitoa ushahidi wa upande wa mdaiwa katika kesi ya kupinga matokeo ya ubunge wa Mbunge wa Igunga, Dk. Dalaly Kafumu (CCM). Kesi hiyo ilifunguliwa na Mgombea wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Joseph Kashindye.
Akitoa ushahidi katika Mahakama Kuu, Kanda ya Tabora, Mjini Nzega, Nchemba ambaye pia Mbunge wa Iramba Magharibi (CCM), alikanusha tuhuma za kutoa rushwa kwa walimu katika eneo la Nkinga pamoja na kutoa lugha ya matusi katika baadhi ya mikutano ya kampeni.
Nchemba ambaye alikuwa Kiongozi Mkuu wa Kampeni za CCM, aliieleza Mahakama hiyo, kuwa chama hicho kilitenga Sh milioni 402 kwa ajili ya shughuli nzima ya kampeni.
Awali, Wakili wa Mlalamikaji, Profesa Abdallah Safari, alieleza Mahakama kuwa, September 16 mwaka jana, Nchemba alikutana na walimu na kuwashawishi waipigie kura CCM ili kukinusuru kisianguke pamoja na kuwagawia fedha walimu 70 katika eneo la Shule ya Msingi Nkinga iliyoko Igunga.
Akijibu hoja hiyo, Nchemba alikana kuhusika na utoaji wa pesa ndogo ndogo, kwa walimu hao na kusema kuwa yeye husaini hundi katika chama hicho.
Mimi sihusiki na viji-petty cash, nahusika na kusaini akaunti kubwa, hivyo vijipetty cash vina wenyewe kama nilivyotaja hapo mwanzo,alisema Nchemba.
Kwa mujibu wa Nchemba, chama hicho hakiwezi kunusuliwa na kikundi cha walimu bali kinanusuliwa na wanachama wa CCM waliopo sehemu mbalimbali nchini wakiwamo wa Igunga.
Huwezi kumpatia shetani neno la Mungu akahubiri, ni jambo ambalo ni gumu sana, alisema Nchemba akiwalenga walimu kulingana na swali aliloulizwa na Profesa Safari.
Mwanzoni, Nchemba wakati akijitambulisha, alidai CCM ina fedha nyingi na yeye ni Bwana Fedha wa chama hicho, kauli ambayo ilisababisha wananchi waliofurika mahakamni hapo kuguna.
Hata hivyo, Jaji Mery Shangali anayesikiliza shauri hilo, alimtaka mbunge huyo kuheshimu Mahakama kwa kutotumia lugha zisizostahili.
Wakati huo huo Mahakama hiyo ilikataa ushahidi wa shahidi wa 18 ambaye ni Ofisa Mtendaji, Kata ya Igunga, Fedrick Magaka kutokana na shahidi huyo kuhudhuria baadhi ya vikao vya kesi hiyo. Kesi hiyo itaendelea leo.