NCCR Mageuzi yamfukuza uanachama Kafulila na wenzake!

Ingawaje siungi mkono kuvuliwa uanachama kwa baadhi ya wanachama na viongozi wa chama cha NCCR,lakini nimefurahishwa na ule uthubutu wa kuchukua maamuzi magumu ambayo ndugu zangu wa CCM wamekua wagumu kuyachukua.
Kuchuka maamuzi magumu kunaleta nidhamu katika kazi.Watendaji wa serikali pamoja na vyama vyote vya siasa,kama kila mmoja angekua anatimiza wajibu wake,na wale wenye mamlaka wakawawajibisha wanaoenda kinyume na taratibu,nina uhakika kuwa Tanzania ya leo ingekua ni ile nchi ya asali na maziwa tunayoitamani.
Naomba tuichukulie NCCR kama mfano na tuanze kubadilika tuchukue maamuzi magumu katika kuwajibishana.

maamuzi haya ccm wanayochombeza katika vyama vya upinzani wanapaswa kuyafanya wao katika kusukuma mbele gurudumu la taifa!!otherwisw watanzania wote tuna laana!!!
 
Majina mengine bwana, eti Kafulila.
mnakmkumbuka Masumbuko Lamwai alivyosumbuka?
huyu jamaa atafulia mpaka basi.
 
nccr nazani uchaguzi ujao wanaweza wawe na mmbunge mmoja au wakase kabisa,hawana tofauti na kaf
 
ya ngoswe mwachie ngoswe! CHADEMA mkimpokea hapatatosha.! kigoma kuna wanachama wengi hilo jimbo tulimwachia kwasababu alionekana kuwa anaweza kumbe kweli hawezi. mtu ambae hawezi kutumia vikao kukosoa wenzake badala yake anakimbilia magazeti na tv. Acha ile kwake ajifunze.
 
0digg
clip_image001.jpg
ALISULUBIWA NA WAJUMBE 38, ALIANGUA KILIO ZAIDI YA DAKIKA 40, KINA MBATIA KUMUONA RAIS KIKWETE
Fidelis Butahe
DAVID Kafulila mbunge kijana kutoka Jimbo la Kigoma Kusini juzi aliingia kwenye ukumbi wa mkutano akiwa na nguvu na matumaini ya kumsimamisha uongozi mwenyekiti wa chama chake cha NCCR Mageuzi, James Mbatia, lakini mwisho, upepo ulivuma vibaya kuelekea upande wake na hatimaye akajikuta anasulubiwa na kisha kuvuliwa uanachama.

Kafulila ambaye alitokea Chadema na kujiunga NCCR- Mageuzi mwishoni mwa mwaka juzi na mwaka jana akafanikiwa kuingia bungeni baada ya kumwaga mgombea wa CCM, Kifu Gullamhussein , ni mwanasiasa kijana ambaye alianza kung’ara katika medani za siasa nchini kutokana na kusimamia hoja zenye maslahi ya umma kama Katiba Mpya, kupinga nyongeza ya posho za wabunge na kutaka wale ambao walisababisha hadi Dowans kupata tuzo ya zaidi ya Sh100 kuchukuliwa hatua.

Safari ya kumshughulikia Kafulila ilianzia Desemba 8 mwaka huu baada ya kuvuliwa wadhifa wa Katibu Mwenezi wa chama hicho na juzi, ilihitimishwa katika Ukumbi wa Proin ambako mkutano wa Halmashauri Kuu (NEC) ya chama hicho ulifanyika kuanzia saa mbili asubuhi hadi karibu saa tano usiku.

Gazeti hili liliwashuhudia wajumbe 64 wa mkutano huo wakifika katika ukumbi huo huku wakionekana kuwa na shauku ya kutaka kujua hatma ya chama hicho baada ya kuibuka kwa mvutano baina ya Kafulila, Mwenyekiti wa chama hicho, James Mbatia na Katibu wake Samwel Ruhuza.

Kuwasili wa Kafulila
Kafulila alifika katika ukumbi huo saa 2:00 asubuhi akiwa kwenye gari yake aina ya Toyota Altezza na moja kwa moja aliingia ndani baada ya mabaunsa zaidi ya 10 waliokuwa katika geti la kuingilia kumruhusu.

Kuanza kwa mkutano
Mkutano huo ulianza rasmi mnamo saa 3:00 huku ukiongozwa na Dk Sengondo Mvungi, akisaidiwa na Ruhuza na Makamu mwenyekiti wa chama hicho Zanzibar, Haji Ambari Khamis.

Katika mkutano huo, Mbatia alikuwa mmoja wa watuhumiwa ambao alipaswa kujibu tuhuma zake za kukifanya chama kama CCM B huku Kafulila akituhumiwa kuvujisha siri za chama nje ya utaratibu wa vikao. Moja ya tuhuma za Kafulila ni kueleza vyombo vya habari kwamba ameondolewa katika nafasi ya uenezi.

Baadhi ya wajumbe wadaiwa si halali
Lakini, hali ya mambo katika chumba cha mikutano ilianza kuvurugika ilipofika saa 8:00 mchana wakati wa kupigakura ya za kutokuwa na imani na Mbatia baadhi ya wajumbe walitoka nje ya ukumbi kwa maelezo kuwa baadhi ya wapiga kura hawakuwa wajumbe halali wa mkutano huo.

Habari hizo zilieleza kwamba, waliotoka nje walikuwa saba huku wakiongozwa na aliyekuwa mgombea urais wa chama hicho katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka jana na Mjumbe wa Baraza la Wadhamini la chama hicho, Hashim Rungwe.

Kwa mujibu wavyanzo hivyo, baada ya hali kuwa shwari wajumbe hao walipokea na kujadili utetezi wa Mbatia. Tuhuma dhidi ya Mbatia zilitolewa na Kamishna wa chama hicho Mkoa wa Tanga, Mbwana Hassan pamoja na wengine 26 waliosaini hati ya kutokuwa na imani naye kwa madai kuwa ni CCM B.

‘’Katika kupiga kura haki haikutendeka, wajumbe tulipiga kura kwa kunyoosha mikono na sio kura ya siri, pamoja na hayo Mbatia alionekana kuwa safi’’ alieleza mmoja wa wajumbe wa NEC wa chama hicho.

Hata hivyo, akizijibu shutuma hizo mbele ya waandishi wa habari jana, Ruhuza alisema kuwa mkutano huo ulitoa maazimio kwamba Mbatia yuko safi, hodari na shujaa wa chama.
‘’Wajumbe wote waliotoa malalamiko walijiondoa na Mbatia akawa safi hiyo ikiwa ni pamoja na hao waliokuwa wakimpinga awali,’’ alisema Ruhuza.
Hoja ya kumjadili Kafulila
Baada ya kumalizika hoja ya Mbatia na kufanikiwa kuzima kile alichokuwa akikiita uasi dhidi yake, jioni ndipo ilipokuja hoja ya Kafulila.

Zamu hiyo ya Kafulila ilipokuja upepo ulionekana kubadlika ghafla ndipo alipopewa nafasi ya kujitetea kuhusu tuhuma zinazomkabili.

Alivyojitetea
Habari hizo zilieleza kuwa Kafulila alipopewa nafasi ya kujieleza, alisema kama kweli kuna mvutano baina yake na Mbatia kinachotakiwa ni kukutana na kuzungumza chini ya usimamizi wa wazee wenye busara wa chama hicho.
Habari hizo zilelieza zaidi kuwa Dk Mvungi wakati akitoa maelezo yake alisema kuwa wajumbe wanatakiwa kutumia busara katika uamuzi yao.

Hata hivyo, hali iliharibika zaidi kwani licha ya utetezi huo wa Kafulila, wanachama ndani ya ukumbi huo baada ya kuanza kupiga kura za kuwafuta uanachama makada wa chama hicho akiwemo Kafulila.

Habari zilieleza kuwa baada ya kuthibitisha upepo unavuma vibaya kwake na hakuna njia ya kutokea, Kafulila alikwenda kumwomba msamaha Mbatia huku akiwa amepiga magoti jambo ambalo liliwakera wajumbe ambao walimwita msaliti.

Lakini, wajumbe walipiga kelele, ‘’Anaigiza huyo muda wote alikuwa wapi? Hata kujitetea kashindwa na amekuwa akijibu majibu ya mkato sasa ndio anakumbuka kuomba msahama, muongo huyo’’.

Kafulila alia kwa uchungu
Kilio cha kwikwi kilimtoka Kafulila kuanzia saa 4:48, usiku baada ya mkutano huo kumvua uanachama Kafulila. Mwananchi lilifanikiwa kujipenyeza hadi ndani ya geti la ukumbi na kumkuta Kafulila akilia kwa sauti huku akiwa amepiga magoti na kumshika mmoja wa wajumbe miguuni.

‘’Nisameheni jamani..., naomba mnisamehe jamani nimekosa nitakwenda wapi?,’’ alisikika akilia.

Mbunge huyo alionekana kushindwa kujizuia na kuangua kilio kilicholeta huzuni kwa baadhi ya wajumbe wa mkutano huo ambao baadhi yao walionekana kumwonea huruma

Kutokana na hali hiyo, Mbatia alijaribu kumwombea msamaha kwa wajumbe, lakini walishikilia msimamo wao kwa maelezo kwamba kama Kafulila akisamehewa, wao watarudisha kadi za chama.

Katika wakati fulani Kafulila aliyekuwa amevaa suti nyeusi alikuwa alisimama nje ya mlango wa kuingilia katika ukumbi huo huku akiwa amekunja mikono yake, mfano wa mtu anayemwomba Mwenyezi Mungu
Wajumbe waliokuwa wakitoka katika ukumbi huo walionekana kutomjali na walimpita na kuingia katika magari yao na kuondoka jambo, lililozidi kumwongezea uchungu na kuonekana akizidi kulia mpaka alipokuja kutolewa eneo hilo na Mkuu wa Idara ya Oganaizesheni, Kampeni na Uchaguzi wa chama hicho, Faustine Sungura.

Walimtoa eneo hilo na kumpeleka katika gari lake na kuondoka eneo hilo wakati huo ilikuwa saa 5:37 usiku.
Wafuasi wa Kafulila washikwa huzuni

Hayo yakiendelea ndani nje kulikuwa na baadhi ya makada wa chama hicho waliokuwa kundi moja na Kafulila ambao walionekana kuwa na huzuni kubwa baada ya kupata habari hizo.
‘’Wamemfukuza..., wameshakiua chama ndio maana mimi nakuelezeni kila siku hiki sio chama, hakina demokrasia ya kweli, ni bora kwenda CCM tu kuliko hiki chama,’’ alisikika akisema mmoja wa makada hao.

Polisi na mamluki
Awali, wakati zikipigwa kura za kutokuwa na imani na Mbatia ulizuka mtafaruku baada ya wajumbe kushangazwa na kitendo cha kuwepo kwa wajumbe zaidi ya 60 wakati mkutano huo huwa na wajumbe wasiozidi 40.

Baadhi ya wajumbe waliibua hoja ya kutaka baadhi ya watu ambao hawafahamiki kujieleza na taratibu zitumike kuwatambua au kutowatambua.

Kutokana na hali hiyo kuibua mgogoro katika kikao hicho Rungwe pamoja na baadhi ya wajumbe walitoka nje ya mkutano huo, wakionyesha kutoridhishwa na maamuzi yaliyotolewa katika upigaji wa kura.

Habari hizo zilieleza kuwa Rungwe pia alijieleza sababu za yeye kuiandikia barua ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa nchini kuiarifu kuwa kikao hicho hakikuwa halali

Awali, wakati mkutano ukiendelea habari za ndani kutoka katika mkutano huo zilieleza kuwa wakati ajenda mbalimbali zikijadiliwa Kafulila aliwasiliana na polisi na kuwaeleza kuwa katika mkutano huo kulikuwa na vurugu.
Mwananchi lilishuhudia polisi tisa wakiwa katika gari aina ya Landcruser wakifika katika Ukumbi huo saa 6:05 mchana na kuingia ndani ya ukumbi, ambao walielezwa hakukuwa na vurugu yoyote na wakatoka nje na kuondoka.

Ilipofika saa 6:45 polisi hao walirudi tena na kueleza kwamba, walipigiwa simu nyingine kwamba katika mkutano huo hali si shwari na safari hii walimhoji dereva wa Kafulila, Denis Kalikisha.

Wakati huo huo, chama hicho kimeomba kukutana na Rais Jakaya Kikwete kwa nia ya kutoa mawazo yake kuhusu mchakato wa kutungwa kwa Katibu Mpya ya Tanzania, kama ilivyoahidiwa kwa wananchi na mkuu huyo wa nchi.
Kafulila aliwahi kupinga kukutana na Rais Ikulu kwa madai suala zima la mchakato wa Katiba Mpya umekiukwa.

Lakini, taarifa ya Kurugenzi ya Mawasiliano Ikulu jana ilisema Rais sasa amekubali ombi hilo la NCCR-Mageuzi.

Mbali ya NCCR, Rais pia amekubali kukutana na Baraza la Taifa la Taasisi Zisizokuwa za Kiserikali (NGO’s), ambalo limeomba kukutana na kuzungumza nye.


 
Alimpigia magoti Meku Mbatia, maana alishaona projections zake za cashflow pale mjengoni zitatiliwa mchanga. Kama alikuwa sahihi ktk anachokisimamia kwanini alirudi tena kulamba matapishi, zis cantri bana inatawalaiwa na watu wajinga sana wasio na msimamo.
 
  • Thanks
Reactions: ral
Hii imenifanya nifikiri kuwa jamaa alikuwa analilia posho au ile gari!

"Kafulila alia kwa uchungu
Kilio cha kwikwi kilimtoka Kafulila kuanzia saa 4:48, usiku baada ya mkutano huo kumvua uanachama Kafulila. Mwananchi lilifanikiwa kujipenyeza hadi ndani ya geti la ukumbi na kumkuta Kafulila akilia kwa sauti huku akiwa amepiga magoti na kumshika mmoja wa wajumbe miguuni."
 
Alimpigia magoti Meku Mbatia, maana alishaona projections zake za cashflow pale mjengoni zitatiliwa mchanga. Kama alikuwa sahihi ktk anachokisimamia kwanini alirudi tena kulamba matapishi, zis cantri bana inatawalaiwa na watu wajinga sana wasio na msimamo.


Kama angejua yangefika huko, Kafulila angemuendea Mbatia na jani la msale siku moja kabla ya mkutano.

On a serious note, NCCR wamefanya kosa kubwa sana kumfukuza Kafulila. Kwa namna fulani wamedhirihisha kabisa kuwa NCCR ni CCM-C kwa sababu hata wakati wa mgogoro wa sheria ya katiba, ni Kafulila peke yake NCCR aliyeonesha msimamo thabiti wa kuupinga muswada.
 
Huu ni ujumbe wa kukufariji kama kijana mpambanaji usiekubali kutumiwa na wababaishaji waliopo kwa Maslahi binafsi.

Unajua zaidi fitna ilipochochewa ili utimuliwe.

Unajua vema magazeti yaliyoripoti kukuhusisha na Zitto kwamba unataka kumuengua Mbatia ili Zitto achukuwe nafasi yake na kugombea Urais 2015.

Bado unakumbu kumbu ya Jinsi ulivyoondoka Chadema.

Unachohitaji kufanya sasa hivi ni maamuzi sahihi.

Sisemi ukate Rufaa popote. Sisemi uende CCM ni kinyume na dhamira yako. Usile matapishi yako kwa kurudi Chadema ulikoitwa Sisimizi. You know very well about anti-Chadema sentiment kule Kigoma; Zitto is elected as Zitto not as Chadema.

You can choose one of the two:
1. Subiri mabadiliko ya Katiba urudi kama mgombe binafsi 2015............utashinda tu.
2. Kama unapenda ushiriki uchaguzi mdogo go to CUF or UDP.............utapokelewa na utashinda tu.

But by all means possible endapo hautagombea kwenye uchaguzi mdogo CCM italichukua Jimbo hilo. Its either Msambya or Kifu.
Usikate tamaa kijana...........soma historia za wapambanaji wakubwa; walikutana na mikasa kama hiyo yako na mikubwa zaidi lakini wakaishinda.

Kwa sasa pumzika kidogo ukifanya tafakari kwa kina wakati unajipanga kwa mustakbali wako.


Unamtafutia fursa ya mahali pakutokea ,huyu mtu asiyejali taratibu za chama
Maringo na kibuli vimemzidi hana miaka miwili tangu ajiunge na NCCR alipata wapi ujasiri wa kuingia pupa badala ya kusoma mazingira
Magazeti yaliandika alichokuwa akikifanya kudhoofisha upinzani,na kudhani yu mwelewa juu ya kila mtu
Kauli za jeuri na dharau kwa uongozi zinaonyesha Taswira ya mtu alivyo huwezi kumdhalilisha mwenyekiti wako kwenye vyombo vya habari namna hiyo naye ni binadamu unaposema ubunge ni zaidi ya unyekiti ni jeuri kuliko kawaida
Asome somo aombe msamaha NCCR akate rufaa kwenye ngazi za juu za uamuzi kama amekiri kweli toka moyoni watamsamehe
Lakini CDM aliondoka kwa mbwembwe mno Kama aliwatuhumu kwa ubadhirifu,ukabila,udini , ukoo,ukosefu wa dira sidhani kama hayo yameisha kwa mtazamo wake nadhani anngalie chama kingine kisafi manake huko yatakuwa maumivu ya kichwa
Sielewi kwa namna gani vijana wanaingia kwenye siasa wanalelewa na kuiva na kuwa matumaini ya taifa wananshindwa kitu kidogo tu cha mawasiliano angeweza kuwa mwenyekiti wa NCCR kama angetumia right approach
 
Watanzania tujenge utamaduni wa kuangalia vitu kwa kupitia different prisms bila itikadi za kisiasa au kidini.Kama haki haijatendeka kwenye chama ambacho si chako na bila kuathiri mambo ya ndani ya chama kingine ni lazima tulaani vitendo kama hivyo.Vitendo vinavyofanyika ndani ya vyama hivi vya siasa ni pigo kwa watanzania.Wanasiasa vijana pamoja na mapungufu tuliyo nayo lakini kuna tatizo ndani ya mifumo ndani ya vyama vyetu vya siasa hasa utayari wa viongozi wa juu kupokea changamoto zinazokinzana na interest binafsi.Kafulila sasa anatakiwa akae chini ajipange,Naamini ideas na itikadi zake nyingi zimeelemea chadema.

Chadema na sisi tusirithi maadui za watu bali turithi kile alicho nacho na kile anchoweza kuwafanyia watanzania kulingana na jinsi tunavyoamini. NCCR-Mageuzi ina sera nzuri sana,lakini hakijawahi kuwa chama cha siasa kinachowakilisha interest za watanzania at large.Ni muda muafaka sasa wa sisi wanachama wa vyama vingine na wanasiasa kujitathmini upya na ku-reshape system na objectives zetu kwa watanzania ili kwa pamoja tuijenge Tanzania tuitakayo

The party needs to sort itself out, from having a well defined political ideology, to the means with which they select who their leaders are, its necessary that they observe due process.

I bet u if you individually interview the different CCM and even other parties chairmen from over 28 regions of Tanzania on their views on Economic reform, you are bound to get more than 28 different answers.



 
Tuache ujinga na tuwe wakweli.Hakuna Chama chochote duniani kinachoongozwa bila taratibu.Hata kama Mbatia ni tatizo lakini ni lazima uwe na busara katika kupambana naye.Kwa nini asingefanya kampeni za chini chini huku akisubiri muda ufike agombee madaraka ili amshinde kidemokrasia? Haiwezekani ujifanye mjanja halafu yakikufika umwage machozi kama bomba la Dawasco

kweli mkuu hata CCM wanasema hivyo hivyo chadema wakiwananga! kuna tume huru ya uchaguzi...hivi vyama kama chadema vikisema vifuate utaratibu kuna mabadiliko?? kamuulzie mpendazoe!
 
Unamtafutia fursa ya mahali pakutokea ,huyu mtu asiyejali taratibu za chama
Maringo na kibuli vimemzidi hana miaka miwili tangu ajiunge na NCCR alipata wapi ujasiri wa kuingia pupa badala ya kusoma mazingira
Magazeti yaliandika alichokuwa akikifanya kudhoofisha upinzani,na kudhani yu mwelewa juu ya kila mtu
Kauli za jeuri na dharau kwa uongozi zinaonyesha Taswira ya mtu alivyo huwezi kumdhalilisha mwenyekiti wako kwenye vyombo vya habari namna hiyo naye ni binadamu unaposema ubunge ni zaidi ya unyekiti ni jeuri kuliko kawaida
Asome somo aombe msamaha NCCR akate rufaa kwenye ngazi za juu za uamuzi kama amekiri kweli toka moyoni watamsamehe
Lakini CDM aliondoka kwa mbwembwe mno Kama aliwatuhumu kwa ubadhirifu,ukabila,udini , ukoo,ukosefu wa dira sidhani kama hayo yameisha kwa mtazamo wake nadhani anngalie chama kingine kisafi manake huko yatakuwa maumivu ya kichwa
Sielewi kwa namna gani vijana wanaingia kwenye siasa wanalelewa na kuiva na kuwa matumaini ya taifa wananshindwa kitu kidogo tu cha mawasiliano angeweza kuwa mwenyekiti wa NCCR kama angetumia right approach

CCM nao wanasema.....chadema, nccr, cuf na TLPni vichanga sana haviwezi kushika uongozi na kubadilisha nchi!! wewe nawe wasema vilevile mwana wangu!

ebu nieleze hwo long does it take to know this is right and this is wrong....and how long requires to make it right??

vyama vya kifamilia havina right approach...kamuulize Zito wa chadema au Hamada wa cuf!!
 
Watanzania tujenge utamaduni wa kuangalia vitu kwa kupitia different prisms bila itikadi za kisiasa au kidini.Kama haki haijatendeka kwenye chama ambacho si chako na bila kuathiri mambo ya ndani ya chama kingine ni lazima tulaani vitendo kama hivyo.Vitendo vinavyofanyika ndani ya vyama hivi vya siasa ni pigo kwa watanzania.Wanasiasa vijana pamoja na mapungufu tuliyo nayo lakini kuna tatizo ndani ya mifumo ndani ya vyama vyetu vya siasa hasa utayari wa viongozi wa juu kupokea changamoto zinazokinzana na interest binafsi.Kafulila sasa anatakiwa akae chini ajipange,Naamini ideas na itikadi zake nyingi zimeelemea chadema.

Chadema na sisi tusirithi maadui za watu bali turithi kile alicho nacho na kile anchoweza kuwafanyia watanzania kulingana na jinsi tunavyoamini. NCCR-Mageuzi ina sera nzuri sana,lakini hakijawahi kuwa chama cha siasa kinachowakilisha interest za watanzania at large.Ni muda muafaka sasa wa sisi wanachama wa vyama vingine na wanasiasa kujitathmini upya na ku-reshape system na objectives zetu kwa watanzania ili kwa pamoja tuijenge Tanzania tuitakayo

The party needs to sort itself out, from having a well defined political ideology, to the means with which they select who their leaders are, its necessary that they observe due process.

I bet u if you individually interview the different CCM and even other parties chairmen from over 28 regions of Tanzania on their views on Economic reform, you are bound to get more than 28 different answers.



Kwa hiyo mmeamua kuibomoa kimya kimya? Toka mafichoni.
 
Back
Top Bottom