Nawaza siku JF isipokuwepo siasa zetu zitakuwaje!?

Allen Kilewella

JF-Expert Member
Sep 30, 2011
18,300
33,915
Kwa Mbinyo wanaopewa wapinzani wa CCM na wale wana CCM wanaotaka kuwa na mawazo huru na yaliyo tofauti na viongozi wao, nimewaza ikitokea siku Jamiiforums isiwe hivi ilivyo ama isiwepo kabisa, siasa zetu za Tanzania zitakuwaje!

Nawaza nguvu ya Jukwaa hili kwa siasa za nchi yetu iwe kwa vyama vya upinzani ama kwa CCM, itakuwaje lisipokuwepo. Hapa JF ndipo wanasiasa wanapoambiwa bila ya kuhurumiwa wala kuonewa aibu na ama na wafuasi wao waliojificha nyuma ya majina bandia ama na wapinzani wao kuhusu udhaifu wao na ujinga walio nao.

Unaposikia wanasiasa wanahanikiza kwamba mitandao ya kijamii ni hatari kwa "amani na utulivu" wa nchi yetu, ujue hapo inatajwa JF kwa jina la uficho. Kuna watu leo hii kwa jinsi wanavyoichukia JF wakipewa nafasi ya kuchagua kati ya kuishi na mwanawe na JF ama kuishi bila mwanawe na bila ya JF atachagua kuishi bila mwanawe na kuishi bila ya JF pia.Ataona ni bora mwanawe afe ili na JF nayo ife. Lakini baada ya hapo siasa zetu zitakuwaje?

Kwa mbali kinasikika kishindo cha zimwi lenge minyonyoro na kufuli la shaba likiinyemelea JF. Kuna kauli kama kuashiria "Bora JF isiwepo tupumzike na makelele yao". Lakini bila Jf siasa zetu Tanzania zitakuwaje?
 
Chini ya mfalme na prince Bashite, hakuna siasa mpaka 2020...
Haya umeyaandika JF ambako kina Maxence Mello wanalinda uhuru wako huo wa kujieleza na kulindwa kwa faragha ya anwani yako. Fikiria kama JF isingekuwepo ungeandika ulichoandika!!??
 
People who make the law are flawed

They don't have best intentions when people are concerned.

Hawa ndiyo wale....give them inch will take a yard give them yard will take a mile.

Jambo ovu sana kujifanya unalinda amani kwa malengo ya kuminya uhuru wa watu kujieleza...yes kujieleza vyovyote vile.

Ndiyo uhuru wenyewe huo.
 
JF imepungua makali sana. Tangu mamluki wajazane humu, mijadala imekuwa dhaifu sana na mingi ni ya hovyo. Analyses are not well grounded. Ni ushabiki tu. Na jukwaa hili linadharaulika sana sasa. Ni washauri wachache tu wa Mkuu wa Nchi wasio na maono ndio wanafikiri JF ni tishio. Sisemi JF ifungwe. La hasha. Hoja yangu ni kwamba JF itabidi kubadilika sana kurudia makali yake ili iweze kutekeleza jukumu lake la kuibinya serikali na wanasiasa uchwara.
 
Zungu Pule nakubaliana na wewe kwamba makali ya JF yamepungua kwa mtizamo wa wengi. lakini kuna msemo kwamba katikati ya lundo ya uchafu jalala huwa kuna vitu vya thamani.

Hii JF inayoonekana imepungua makali ndiyo hiyo hiyo wakurungenzi wake wapo mahakamani wakishitakiwa kwa "Kukataa kushirikiana na Polisi". Nyie mnaona imepungua makali wenzenu wanataka hata hayo mnayoona ni makali butu yasiwepo kabisa!
 
Zungu Pule nakubaliana na wewe kwamba makali ya JF yamepungua kwa mtizamo wa wengi. lakini kuna msemo kwamba katikati ya lundo ya uchafu jalala huwa kuna vitu vya thamani.

Hii JF inayoonekana imepungua makali ndiyo hiyo hiyo wakurungenzi wake wapo mahakamani wakishitakiwa kwa "Kukataa kushirikiana na Polisi". Nyie mnaona imepungua makali wenzenu wanataka hata hayo mnayoona ni makali butu yasiwepo kabisa!

Tatizo kubwa la JF ni partisanship.

Kama nilivyosema, Wakurugenzi wa JF wapo mahakamani kwa sababu tu ya "ignorance" ya baadhi ya washauri wa Mkuu wa Nchi. Au pengine Mkuu mwenyewe anashindwa kuchambua na kutambua "threats" kwa utawala wake. Uhuru wa kutoa maoni hauwezi kuwa threat kwa kiongozi mwenye nia njema. JF inapaswa kuwa chachu, si threat kwa watawala, kama wana nia njema. Censorship ni sera ya utawala wa sasa. Tatizo kubwa ni kwamba wananchi tunaonekana kuruhusu hilo kutokea. Watu wengi wanafikiri wanaokamatwa kwa kutoa maoni yao kwenye mitandao wametukana, hivyo wanastahili adhabu. Wengi wanashindwa kuelewa faida za uhuru wa kutoa maoni. Madhara ya censorship ni makubwa. Ukisharuhusu serikali ikupangie aina ya maoni unayopaswa kutoa, you are no longer living. You are dead. Nguli Ai Weiwei anaeleza madhara ya censorship, akitumia mfano wa nchi yake ya Uchina: https://www.nytimes.com/2017/05/06/opinion/sunday/ai-weiwei-how-censorship-works.html
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom