Nawasifu Madaktari wanafanya mambo kisomi

Kifuna

JF-Expert Member
Aug 7, 2008
442
116
Moja ya jambo ambalo madaktari hawa wamelifanya na nimeliona ni zuri na la kisomi zaidi ni kumtaalifu mtoto wa mkulima kuwa hawatakuja ukumbini kwenye mazunguzo kisha hawakuishia hapo wakatoa na sababu wanasema kuwa taalifa iliwafikia usiku ikiwa imechelewa sana. Swali la kujiuliza ni kwa nini Waziri mkuu alienda wakati walimwambia kuwa hawatakuwepo? Mimi nafikiri ni kuwa alitaka kuwaonyesha kuwa yeye ni nani! Sasa hawa jamaa hawataki hilo! Ni lazima PM aangalie alama za nyakati.
Jambo lingine nafikiri mtoto wa mkulima alikuwa anawaita kwenye majadiliano na siyo maelekezano sasa kama mtu unamwita kujadiliana nae usimtishie, hapa naona kama vile Mtoto wa mkulima anatishia maiti. Kiasi walichofikia madaktari hawa wamechoka.Abadili mbinu ya kujadiliana wataelewana tu.
Nawasilisha.
 
hawana muda tena,kwakuwa wote wanaoisumbua serikali ni wanafunzi wanafanyakaz kwny ngos za ukimwi sio mhm kama hawataki kurud kwng ngos zao.
 
Huo ukali aliouonyesha mtoto wa mkulima angekuwa ndio anaounyesha kwa mafisadai ,watu wa EPA,na akina Jairo ningemuona mtu wa kazi,huwezi mlazimisha punda anywe maji bana
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom