Nawashukuru Watanzania-Waasia hawa; historia itawakumbuka

Mzee Mwanakijiji kwanza nikushukuru kwa kutukumbusha habari hiyo. Hata mie nilikuwa na copy ya hiyo taarifa ambayo niliipata kwenye mtandao. Lakini mpaka leo sijui ni watu gani walio itayarisha. Kama ni Watanzania waasia basi nawapa hongera sana kwa kazi nzuri waliofanya ya kumwaga "mboga".
Nahisi watanzania wenye uwezo wa kumwaga "ugali" ni wachache sana. Kumbuka asilimia si chini ya 70 ya watanzania wapo vijijini na hii ripoti sidhani kama wameisikia.
 
Nahisi watanzania wenye uwezo wa kumwaga "ugali" ni wachache sana. Kumbuka asilimia si chini ya 70 ya watanzania wapo vijijini na hii ripoti sidhani kama wameisikia.


Usijali Mungu si Athumani kama walivyo mwaga mboga hao ambao hawakutegemewa ndivyo itakavyo kuwa kwa watakao mwaga ugali. Hakuna mfumo wa kibinadamu wa kidhalimu utakao dumu milele....time is a gudi furendi...
 
Uzushi mtupu, gari moshi lilianzia stesheni namba moja, chanzo cha matatizo yote ya Tanzania ya leo ni Nyerere, Ujamaa ulikuwa ni chanzo cha matatizo na hilo halipingiki.
"[FONT=Verdana,Arial,Helvetica]But the Tanzanian experiment offers good evidence that saints do not really make very good presidents"[/FONT]


Kaka/Dada hebu pitia kidogo JF Doctor ukapate ushauri maana lazima utakuwa unaumwa "something"..........
 
WABAKAJI WA UCHUMI DUNIANI WANAJUA NAMNA YA KUWATUMIA HAWA WAZEE VILAZA MA-MBUMBUMBUU WASIO NA UWEZO WA KUFIKIRI UREFU WA PUA YAO...

WANAJUA KUWA UCHAGUZI FEKI = RAIS FEKI + MAWAZIRI FEKI + WABUNGE FEKI + MAJAJI FEKI + MAJESHI FEKI + MABENKI FEKI + KILIMO FEKI + UVUVI FEKI + UFUGAJI FEKI + SEKTA YA MADINI FEKI + MIPANGO FEKI + VIWANDA FEKI + MASHIRIKA FEKI + VYUO FEKI + HOSPITALI FEKI + MIUNDO MBINU FEKI + MAKANISA FEKI + MISIKITI FEKI + WAUMINI FEKI + WANANCHI FEKI + FIKRA FEKI + MISHAHARA FEKI + WAZALENDO FEKI
progress.gif
= WATAWALIWA MILELE !!! KUDOS MWANAKIJIJI THO KAZI ZA MIKONO YAKO ITAKUJA KUONEKANA KWA VIZAZI VIJAVYO!!!
 
The evidence has been gathered from official
Bank of Tanzania documents, government agencies and authorities.

Kama tungo hii ni kweli basi,
1. Hata Watanzania wenye asili ya Afrika wanaweza kuwa ndio wengi wamehusika kuzinyofoa hizo 'primary' data na kuwakabidhi hao waliozikusanya (gather) na kuziwasilisha maana ndio watumishi wengi walioko kwenye Mabenki na Asasi / Wakala wa Serikali.
2. Hata UWT nao wanaweza kuwa wamehusika maana nao ni sehemu ya Asasi / Mamlaka za Serikali na hata humo wahusika wanaweza kuwa wenye asili ya Kiafrika na Kiasia au asili nyinginezo (nani anasema UWT haina maajenti wenye asili tofauti na ya Kiafrika?).

BTW.
Mwanakijiji, waliokusanya (gather) data unasema ni wa asili ya Asia, je waliozipanga, kuzichambua na kuzitafsiri (organise, analyze & interpret) walikuwa wenye asili gani maana hao nao ni muhimu sana.
Aidha binafsi nina swali juu ya hiyo organogram ya Umafia wao; kwamba ni kwa nini JayantKumar Patel (Alias Jeetu Patel) ndiye aitwe Head of Crime Family? Je ni kwa sababu ndiye aliyefaidika sana na mfumo, au ndiye kweli kiongozi mfawidi wa ufisadi 'wooote' huo yaani anayetengeneza sera na au kutoa amri nini kifanyike kote huko au ni kwa sababu ndiye mwenye makosa ya jinai kibao katika nchi yetu na nje kuliko hao wengine. Je kweli muundo (organisation structure) wa Umafia wao ni wa msoge kama unavyoonekana au ni wa style ya mtando wa buibui. Na je yeye mwenyewe huko juu kabisa ANAWAJIBIKA KWA NANI? (yaani uki- extrapolate lines of authorities juu ya Jeetu Patel kuna nani au kuna asasi gani au yeye ndiyo mwanzo na mwisho kama Mungu?

Zaidi ya pongezi kwa KUKUSANYA (GATHERING), mimi natoa pongezi za dhati za ukabla (in advance) kwa wote wenye asili yeyote WATAKAOZITUMIA (UTILIZATION) takwimu au taarifa za kweli na zilizo kamili kwa ajili ya maendeleo ya nchi na dunia kwa ujumla.

Mwalimu wangu alisema, ' Data are like bikinis. What they reveal is suggestive, but what they conceal is vital'
 
Umenikumbusha maneno ya mzee ruksa...zamani zilee alisema: kosa la pateli ni la pateli peke yake na si la wahindi wote...na kosa la masanja ni la masanja pekee si la wasukuma wote...hii imethibitisha kuwa kumbe kuna waasia wengine si magabachori. mzee mwanakijiji ahsante sana kwa kutufungua macho.
 
Mzee Mwanakijiji kwanza nikushukuru kwa kutukumbusha habari hiyo. Hata mie nilikuwa na copy ya hiyo taarifa ambayo niliipata kwenye mtandao. Lakini mpaka leo sijui ni watu gani walio itayarisha. Kama ni Watanzania waasia basi nawapa hongera sana kwa kazi nzuri waliofanya ya kumwaga "mboga".

Lakini tukumbuke kwamba hawa waasia walimwaga mboga baada ya wao kukosa "mnuso" hapo BoT. Nia hasa ilikuwa ni kukomoana. Ndio maana hata Rais alipohutubia Bunge Agosti 2008 huko Dodoma alisema "bila ugonvi wa wafanyabiashara sakata la EPA lisingejulikana kwa umma". Binafsi namshukuru IBILISI aliyewafanya hawa waasia wagombane wao kwa wao. Wangechotewa EPA wasingetoboa siri hata kidogo. Ndio mana hata Gavana Bilali alivyopewa hiyo ripoti kwa mara ya kwanza na kuisoma alijisahau na kubwatuka mbele ya msaidizi wake akasema "huyu ni ......". Alimjua kwa vile alijua kwamba alimkatalia ombi lake la kuchota EPA.

Waasia ni waasia tu. wana mwili (makazi) wao Tanzania, roho yao iko India na Pesa yao Canada au Ulaya.
 
Kwa niaba ya kijiji changu na wale wote ambao wanasimama leo kama majemedari dhidi ya vita hii ninawashukuru sana na ninaisubiria kwa hamu ripoti yao ijayo kabla ya uchaguzi mkuu. Kwani kwa mara nyingine tena, kuta za vyumba vya wanasiasa wetu na wale waliojinyanyua juu yetu zitatikisika na wale tuliowadhania siyo kumbe ndio hao hao!

Nimeona utangulizi wake, nimeipenda.
Kazi ipo. Naisubiri kama wewe, Mama Sophia S na wengine tele ambao either majuzi, juzi au jana na pengine leo wameamua kuwa wapiganaji tunavyoisubiri
Project X-201
0
In initiating stage...
"Change is coming; be part of it, don't wait for it"!

Well, kwa wale ambao hawajui ninazungumzia nini, nimeiambatanisha.[/QUOTE]
 
Yawezekana tumeshasahau au kama tunakumbuka basi tunakumbuka walichokifanya lakini hatukumbuki ni nani walifanya kitu hicho. Wengi wetu letu tumedandia garimoshi la vita dhidi ya ufisadi na kuwataja watu kwa majina lakini hatujui gari moshi hilo lilitiwa funguo na kina nani. .

Sidhani kama hawa jamaa ndio waliotia funguo gari moshi.... noo hapana! Unamkumbuka mwandishi Stan katabalo na kashfa ya Loliondo?

Nawashukuru Watanzania-Waasia hawa; historia itawakumbuka

Kwa hili moja nimejikuta leo nikiamua kuonesha shukrani za dhati kwa mchango wao mkubwa katika vita ya ufisadi kwani pasipo ripoti ile kali, labda leo tungeendelea kuchezeshwa "tiari bado" huku tukikimbizwa mchaka mchaka wa "Chinja". Leo hii tungeendelea kuwa na Benki Kuu ile ile ikifanya kazi zake kwa mtindo ule ule.

Mwizi aliyesalitiwa na wenziwe akaamua kuwachoma leo hii tumshukuru na kumuona shujaa mpaka historia imkumbuke kweli...!!!!?
 
kitu cha kushangaza ni mfano serikali ilitahadhalishwa mapema kuhusu RITES ya India lakini waziri akang'ang'ana kwamba lazima waingie mkataba na hiyo kampuni. Je sasa hivi kwa nini aliye saini mkataba asifungwe??

Hapo ndo mimi sina imani na JK kabisa.
 
Lakini tukumbuke kwamba hawa waasia walimwaga mboga baada ya wao kukosa "mnuso" hapo BoT. Nia hasa ilikuwa ni kukomoana. Ndio maana hata Rais alipohutubia Bunge Agosti 2008 huko Dodoma alisema "bila ugonvi wa wafanyabiashara sakata la EPA lisingejulikana kwa umma". Binafsi namshukuru IBILISI aliyewafanya hawa waasia wagombane wao kwa wao. Wangechotewa EPA wasingetoboa siri hata kidogo. Ndio mana hata Gavana Bilali alivyopewa hiyo ripoti kwa mara ya kwanza na kuisoma alijisahau na kubwatuka mbele ya msaidizi wake akasema "huyu ni ......". Alimjua kwa vile alijua kwamba alimkatalia ombi lake la kuchota EPA.

Waasia ni waasia tu. wana mwili (makazi) wao Tanzania, roho yao iko India na Pesa yao Canada au Ulaya.

Mkuu Byasel,
Nakubaliana na maoni yako 100% kwa ufahamu nilio nao. Na pia ili tusifanye dhambi kama yupo ambaye kweli alifanya hayo kwa kuwa mzalendo wa kweli basi anastahili sifa na hizo asante, I really doubt there is.... but that space should be provided and be there!
Kinachonishangaza baadhi ya watajwa kwenye hizi scandle bado wanafanya biashara kubwa tu hapo dar na watu hawana habari tunakwenda kutaka kufanya nao bishara kubwa tu!! Thkis has truly shocked me, sasa hii serikali hata haijali inawaachia wazidi kutumaliza nini? Kuna jamaa yangu alitaka kununua nyumba kwa mmoja wao ya thamani ya zaidi ya Tshs.130mln watu wa benki ndiyo walimshangaza walipokataa kupeleka fedha kwenye akaunti ya hiyo kampuni. Hii si ni hatari sana? Kwanini serikali imekaa pembeni inaangalia?? Aggrrrrr!
 
Hivi ka-inzi kana rangi au kabila?
Alaa mkuu huna bahari kuna nzi wa rangi ya blu makazi yao ktk chimoni, hawajishughulishi na mabaki ya embe ..wao wanajua fika kwamba uchafu wa binadamu huishia shimoni ambako ndiko kuna ulaji wa kupumzika na sii mabaki ya mifupa wanayokimbilia walalahoi (nzi wa kijivu) ambao kila siku wanaepa mikono ya binadamu..
 
Alaa mkuu huna bahari kuna nzi wa rangi ya blu makazi yao ktk chimoni, hawajishughulishi na mabaki ya embe ..wao wanajua fika kwamba uchafu wa binadamu huishia shimoni ambako ndiko kuna ulaji wa kupumzika na sii mabaki ya mifupa wanayokimbilia walalahoi (nzi wa kijivu) ambao kila siku wanaepa mikono ya binadamu..

...duuh.....Mkuu unaweza kutupa tafsiri yake kwa Kikerewe?
 
Ogah,
Haaa! haaa! haaa! Kikerewe kipi - Kisilanga au Kiruhu?..
Ni hivi hawa wadosti sii wenzetu, yaani sii nzi wa kijivu (kama sisi) ambao utawaona wakizengea zengea wakisha nusa harufu ya chakula..
hawa hupenda harufu (Ufisadi) sehemu ambazo wewe na mimi hatuwezi kwenda wala kujaribu kuvuta mnuso wa BoT.
Hivyo, tuwape sifa zao kama alivyosema Mwanakijiji, Ni watanzania na bila shaka hilo neno waasia kaliweka makusudi kutofautisha na wengine ambao hawatoki msalani wanazengea ukija chuchumaa tu wanaanza makamuzi...
Haaa! haaa! haaa!
 
Yawezekana tumeshasahau au kama tunakumbuka basi tunakumbuka walichokifanya lakini hatukumbuki ni nani walifanya kitu hicho. Wengi wetu letu tumedandia garimoshi la vita dhidi ya ufisadi na kuwataja watu kwa majina lakini hatujui gari moshi hilo lilitiwa funguo na kina nani.

Wengine tumesahau pia kuwa JF ilipata umaarufu mkubwa na kuwa kero na kikwazo kwa baadhi ya wanasiasa ambao leo wamegeuka na kuwa upande wetu (Sitta alibeza nyaraka za kwenye mitandao!) lakini tumewasahau wale ambao walianzisha moto huu.

Sijawasahau.

Ni kundi la Watanzania wenye asili ya Kiasia ambao walikusanya taarifa mbalimbali juu ya "wenzao" na watu wengine ambao walihusika na mtandao wa ufisadi wa kimataifa wenye mfanano wa kundi la Kimafia la Sisilia kule Italia.

Aidha kwa kuzidiana kete, wivu, kisasi au chochote kile kilichokuwa nyuma ya malengo yao ukweli ni kuwa walichokifanya kimebadilisha kabisa mjadala wa mahusiano kati ya watawala na watawaliwa, walao na waliwa, wanasiasa na wapiga kura, wananchi na wageni. Walitoa kile kinachojulikana kama taarifa ya mtandao wa ufisadi iliyopewa jina la "Tanzania Mafia". Hii ililikuwa ni kabla ya sakata la Mwembe Yanga.

Ilikuwa kama utani na majungu lakini data walizomwaga, kuunganisha majina ya watu na makampuni, na kutuonesha mtandao huu ulivyofanya kazi ulisababisha aliyekuwa Gavana wa Benki Kuu Ballali, atimke na asirudi milele; ulisababisha mtikisiko wa aina yake huku walioatajwa humo ndani wakitafuta kila namna ya maelezo ya kufafanua vitendo vyao.

Ni katika ripoti hiyo tulifahamishwa kwa undani:

- mahusiano ya Ballali, Jeetu Patel, na Mkapa
- mahusiano ya kina Maregesi na kina Pateli
- Suala la Alex Stewart na kina Basil Mramba
- Kina Lukaza na Bank M
- Kampuni ya Negus ya huko Uswisi (hii hata hatujaanza kuiangalia!)
- Mradi wa Meremeta na wizi wa Benki Kuu
- N.k

Ilikuwa ni ripoti iliyomfichua mfalme kuwa yu uchi; ilikuwa ni ripoti ambayo inasimama kama uthibitisho wa kazi nzuri iliyofanywa na watu wa kawaida huku wanaolipwa kufanya kazi hiyo wakitafuta mbinu na njia ya kuizima. Ndugu zetu waasia hao (pamoja na washirika wengine) waliweza kufanya kile ambacho kimewashinda usalama wa taifa kwa miaka arobaini! Waliweza kufichua kile kilichowashinda kuanzia kina Solomon Liani hadi leo kina Mwema wanahangaika nacho!

Uwezo wao wa kukusanya na kuchambua data na kuziweka katika kurasa chache ulifanywa kwa gharama ya chini kweli kushinda vikao vya kamati mbalimbali za Bunge ambazo hutumia mabilioni kutafuta suluhisho la matatizo ya nishati bila ya mafanikio na kuandika ripoti lukuki zisisofanyiwa kazi zaidi ya kusababisha kuandikwa kwa ripoti nyingine.

Hivyo, ninatambua hisia za watu mbalimbali dhidi ya Watanzania wenye asili ya Asia (Wahindi n.k) na jinsi gani tunawashuku juu ya uzalendo wao na kujitoa kwao kwa ajili ya taifa.

Kwa hili moja nimejikuta leo nikiamua kuonesha shukrani za dhati kwa mchango wao mkubwa katika vita ya ufisadi kwani pasipo ripoti ile kali, labda leo tungeendelea kuchezeshwa "tiari bado" huku tukikimbizwa mchaka mchaka wa "Chinja". Leo hii tungeendelea kuwa na Benki Kuu ile ile ikifanya kazi zake kwa mtindo ule ule.

Ndio siyo kwamba tumefika na siyo kwamba ripoti ile imesababisha mabadiliko katika vichwa vya watawala wetu; hapana! Ripoti ile imetupa nguvu wananchi zaidi kuweza kubisha na kuwakatalia watawala; imetupa nguvu ya kuweza kutambua jinsi tunavyoibiwa kwa jina la "uwekezaji" na imetupa nguvu kuelewa kuwa siyo wote wavaao suti na kujiita wanasiasa na viongozi wanastahili mambo hayo.

Hivyo, kama nilivyofundishwa kushukuru nimejikuta nami nioneshe shukrani kwao. Kwani ni wao pia walituonya kuhusu TRL tukawakatalia na leo tunakiona cha moto. Sina budi kuwashukuru kwa sababu walikuwa na uchaguzi wa kukaa kimya na kufumba macho yao na kumalizana kimya kimya. Waliamua kusema na kutupa nguvu sisi wengine kupiga kelele!

Kwa niaba ya kijiji changu na wale wote ambao wanasimama leo kama majemedari dhidi ya vita hii ninawashukuru sana na ninaisubiria kwa hamu ripoti yao ijayo kabla ya uchaguzi mkuu. Kwani kwa mara nyingine tena, kuta za vyumba vya wanasiasa wetu na wale waliojinyanyua juu yetu zitatikisika na wale tuliowadhania siyo kumbe ndio hao hao!

Nimeona utangulizi wake, nimeipenda.

Project X-2010
In initiating stage...
"Change is coming; be part of it, don't wait for it"!

Well, kwa wale ambao hawajui ninazungumzia nini, nimeiambatanisha.

Mbona umewasahau Chadema?
 
Back
Top Bottom