Black Mirror
JF-Expert Member
- Oct 17, 2019
- 833
- 1,041
Salaam wana JF,
Poleni kwa msiba wa Mh Mkapa, mbali ya kwamba CCM imeendeleza kuimarisha ufukara kwa Watanzania, lakini kwa Jimbo la Nkenge(Missenyi) nawapongeza sana tena sana wajumbe wa CCM kwa kazi kubwa mlioifanya ya kuwabwaga chini hawa vigogo yaani Dr Deodorus Kamala Buberwa na Huyu mama Asumputa Nshunju Mshama, hawa wote wamekuwa wabunge wa jimbo la Nkenge kwa vipindi tofauti lakini ukweli ni kwamba hakuna la maana lolote walilo lifanya, aidha obovu wao ulitegemeana.
Asumputa kwa miaka mitano ya nyuma alipokuwa Mbunge hakufanya jambo lolote la kuwatetea wana Nkenge, yeye aliishia kugawa mipira ya miguu, jezi kwa vijana pia na kanga kofia na visenti kidogo kwenye vikoba kwa akina mama, akaenda zake bungeni kula bata. Muda ulipoisha akapigwa chini na Dr Kamala, huyu ndiye hakufanya chochote na hakuweza hata kumfikia Asumputa walau kugawa jezi alishindwa.
Kamala ni mbunge pekee ambaye baada ya kuchaguliwa alianza kuwatukana wananchi wake kila walipojaribu kumueleza changamoto zao alisema wazi kuwa yeye hakupewa kura bali pesa yake ndiyo ilimpa kura. Alitoa majibu ya kejeli sana, mfno huko kwao kiziba waliwahi kumueleza juu ya uwepo wa kundi la ngedere kwenye mashamba yao aliwajibu hivi...."...ngedere wangekuwa wanaliwa wasingekuwepo..." lakini alisahau wananchi wa Nkenge wanapaswa kutetewa na kupiganiwa juu ya masula ya maji, umeme, barabara, hospitali, masoko na miradi mbalimbali.
Nawashukuru tena kwa kuwapiga chini hawa watu. Mh Kyombo mbunge mteule najua kwenye kamati kuu bado unaweza kuinuka kidedea, kama utaweza kuingia Bungeni hebu jaribu kwanza kurekebisha taswira ya Halmashauri ya Missenyi, ingia vijijini huko watu hawana maji, umeme, barabara nk.
Poleni kwa msiba wa Mh Mkapa, mbali ya kwamba CCM imeendeleza kuimarisha ufukara kwa Watanzania, lakini kwa Jimbo la Nkenge(Missenyi) nawapongeza sana tena sana wajumbe wa CCM kwa kazi kubwa mlioifanya ya kuwabwaga chini hawa vigogo yaani Dr Deodorus Kamala Buberwa na Huyu mama Asumputa Nshunju Mshama, hawa wote wamekuwa wabunge wa jimbo la Nkenge kwa vipindi tofauti lakini ukweli ni kwamba hakuna la maana lolote walilo lifanya, aidha obovu wao ulitegemeana.
Asumputa kwa miaka mitano ya nyuma alipokuwa Mbunge hakufanya jambo lolote la kuwatetea wana Nkenge, yeye aliishia kugawa mipira ya miguu, jezi kwa vijana pia na kanga kofia na visenti kidogo kwenye vikoba kwa akina mama, akaenda zake bungeni kula bata. Muda ulipoisha akapigwa chini na Dr Kamala, huyu ndiye hakufanya chochote na hakuweza hata kumfikia Asumputa walau kugawa jezi alishindwa.
Kamala ni mbunge pekee ambaye baada ya kuchaguliwa alianza kuwatukana wananchi wake kila walipojaribu kumueleza changamoto zao alisema wazi kuwa yeye hakupewa kura bali pesa yake ndiyo ilimpa kura. Alitoa majibu ya kejeli sana, mfno huko kwao kiziba waliwahi kumueleza juu ya uwepo wa kundi la ngedere kwenye mashamba yao aliwajibu hivi...."...ngedere wangekuwa wanaliwa wasingekuwepo..." lakini alisahau wananchi wa Nkenge wanapaswa kutetewa na kupiganiwa juu ya masula ya maji, umeme, barabara, hospitali, masoko na miradi mbalimbali.
Nawashukuru tena kwa kuwapiga chini hawa watu. Mh Kyombo mbunge mteule najua kwenye kamati kuu bado unaweza kuinuka kidedea, kama utaweza kuingia Bungeni hebu jaribu kwanza kurekebisha taswira ya Halmashauri ya Missenyi, ingia vijijini huko watu hawana maji, umeme, barabara nk.