Nawashangaa Viongozi wa CCM kila linapotajwa kosa au tuhuma na nchi washirika wa maendeleo mnakimbilia kusema vita ya kiuchumi. Jibuni hoja kwa hoja

That is the issue, kama wanaweza kupata kwingine, basi watuache tufanye biashara na wengine ambao kwa standard zao kila kitu kiko sawa. Lakini wanakuja na hoja zao za "haki za binadamu na usawa wa binadamu" kwa viwango na vigezo vyao ambavyo kwao havitumiki ila wanataka vitumike kwetu tu. Tukivikataa, basi nongwa, eti tutawekewa vikwazo vya kiuchumi! Mnadhani ni rahisi namna hiyo? Nchi ngapi zimewekewa hivyo vikwazo au ni mikwara tu ya kutaka tuyumbe, watutoe kwenye RELI wapore utajiri wetu kwa faida yao. Hatuyumbi wala hatutolewi kwenye RELI we are an independent sovereign state na wenye kujua haki na wajibu wetu kwa watu wetu na kwa marafiki zetu wenye adabu na heshima na wanaotutakia mema. Kinyume cha hapo tutapamabana nao tu! Ingawa kwa watu wenye kasumba ya kikoloni, hili ni ajabu kwao/kwenu.
Wewe bila shaka ni kijana wa juzi na haujui hali ilivyokuwa nchini baada ya vita vya Kagera. Hali ile ilitokana na wenye fedha zao kutaka zifanyike structural reforms katika mambo ya uchumi. Haukuweko wakati tunapigiwa muziki London na kwingineko ili kushinikiza mataifa ya magharibi kutusamaa madeni yaliyotokana na fedha tulizokopa wenyewe. Haukuweko wakati watu wanazungusha kibakuli Dovos kumpa Mkapa ili zimsaidie kununua vyandarua.

Wewe na wengine mnadhani hii ni mara ya kwanza sisi kujimwambafai na kusema tusiingiliwe kwenye mambo yetu. Mwaka 1999 tulipotaka kununua Radar kutoka BAE tulionywa sana na mabeberu kuwa tunauziwa kitu ambacho hakitufai na kwa bei isiyoendana na uhalisia. Tukawaambia watukome, tukanunua radar. Wote tunajua hatma ya hii hadithi. Mabeberu waliwafuatilia BAE ( kampuni ya kwao) na kugundua kuwa walitupiga sana kwenye ule mradi na kuwataka waturudishie kiasi kikubwa tu cha fedha.

Kuna mwaka tulitaka kumnunulia Rais wetu ndege. Tukaonywa sana lakini Waziri musikaali wa wakati ule akawaambia mabeberu kuwa tuko tayari kula nyasi ili Rais wetu apate ndege ya saiz yake. Wote tunajua mheshimiwa huyo aliishia wapi!

Waliotutangulia walituasa kuhusu umuhimu wa kuchagua vita tunazopigana. Nyingine, kama hii haina tija na hatuna sababu ya kuishupalia.

Amandla...
 
Kwahiyo utawala bora na haki za binadamu vitawawezesha wao kupora Mali za nchi ?
Ndiyo to them "utawala bora na haki za binadamu"ni za kuwawezesha watu kama akina Lissu, vibaraka wao, kuingia madarakani ili wawape mali zetu na utajiri wetu kama walivyofanya babu zetu, machifu wetu wa kale. Walipewa vioo (looking mirrors) kisha wakasaini mikataba ya kutoa nchi zetu! Lakini utawala bora unaofanya vibaraka wao washindwe uchaguzi kupitia sanduku la kura, na kushindwa kwa KISHINDO, to them huo siyo utawala bora! What a heck! Hebu tuelezeni sasa hicho cha US kwenye uchaguzi wao ni "utawala bora na kuheshimu haki za banadamu (Mmarekani) aliyepiga kura huko au nini? Wambieni waache DOUBLE STANDARD kwani sijamsikia BOB wa Lissu akisema lolote on this!
 
Nimepata jibu hili: .. kahawa inapatikana kwa wingi sana Indonesia, Brazil, na maeneo mengine mengi haina hata walaji wa kuimaliza! Dunia haitasimama kisa eti wamekosa kahawa, korosho, pamba, karafuu, sijui mkonge wa Tanzania. Tunaihitaji sana EU na dunia kuliko EU na dunia wanavyoihitaji Tanzania.
Kama hiyo sentesi yako ya mwisho ni kweli basi kawaulize WANAITAKIA NINi TZ, mbona wapo hapa miaka nenda miaka rudi? Kwani ni lazima wawe na diplomatic relations na TZ? Kwani sisi tuna diplomatic relations na nchi zote duniani!? Jibu ni HAPANA. BASi waende wakachukue hivyo vitu huko kwingine mbona wako hapa! Unajua majibu kama haya hata hao maafisa wa balozi mbalimbali hapa nchini wakiyaona humu JF wanatushangaa namna tulivyo IVA KIKASUMBA NA TUSIVYOJIELEWA kama watu! In fact tunahitajiana sana lakini kwa KUHESHIMIANA NA KUTOKUINGILIANA katika mambo yetu ya ndani kwa kisingizio tu kuwa Lissu kapigwa kipigo cha mbwa koko via the ballot box! Waache hizo, wamshauri tu aje tena 2025 kama atakuwa bado NAO! Si unajua "mabeberu" hawana PERMANENT FRIENDS BALI WANA PERMANENT INTERESTS.
 
Ningekutukana tusi kuuuuubwa ila nahofia ban humu. Naishia kukwambia uwezo wako wa kufikiri na kuchanganua mambo Ni mdogo mno, au haupo.
Hapo ndipo uwezo wako wa kuwaza, kufikiri na kuchambua hoja umeishia! Ukienda kidogo, kweli utatoa matusi kwani that is the level of shallow minds! Kama kweli una hoja njoo, tu TUHOJIANE! Halafu, ni tusi gani jipya leo chini ya jua, hata wakati wa Yesu Kristo, walitukana ila hakukuwa na tusi jipya, leo wewe utalitoa wapi ambalo halijawahi kusikika humu JF!?
 
Kabla ya kujibu huu upoloto uliojibu hapa ugefanya tafiti kidogo kujua viwango vya Imports na Exports vya Tanzania kwa nchi hizo na nchi nyingine pia za Africa hapo ungejua jee sisi nimuhimu sana kwao kiasi cha kuingia eti vita vya uchumi nao?
Unaelewa kuwa Budget support yao kwetu na misaada mingine inazidi exports zetu?
Waambieni hao viongozi wenu waache tabia ya uongo uongo
Nilichojibu, ni kutoka kwenye Economic Journals za WB na za WEF za mwaka 2018/2019! Kasome hizo au nenda kasome ripoti ya EU Bank ya mwaka 2019 uone namna biashara ilivyo kati ya hayo mataifa na TZ. Naku refer huko kwani nikikwambia za humu ndani utaishia kusema ni za kughushi! Majibu mepesi kwa masuala mazito! Kama ukipenda basi pitia pale EPZA au Mamlaka ya Kukuza Biashara upate maarifa kidogo in this area.
 
Tufanye unachosema ni kweli, hebu haya.
1. Kwanini mlipokea pesa ya corona wakati tanzania hakukuwa na corona,je hii ni vita ya kiuchumi?

2. Nchi za wazungu wanategemea malighafi kutoka tanzania tu?
1. Hatukupokea pesa za Corona! Huo ni uzushi na uongo uliosemwa na mbunge mmoja huko Ubelgiji kwa nia na lengo la kumfurahisha "Rafiki" yao. Ngoja nikuambie jambo moja, hawa wabunge mnaowasikiliza kutoka huko Ulaya au US na hatimaye kuwanukuu, mjue ni wabunge tu wa kawaida kama akina Mdee au Godbless Enzi zao. They can saya anything in the Bunge na hakuna hatua zozote dhidi yao, ndivyo walivyo hao pa. Juzi nilimsikia Mwakilishi wa Jimbo la New Jersey pale US akituamrisha sisi, kama nchi tufanya atakavyo yeye! What a heck!
2. Hapana! Wana vyanzo vingi sana, karibu dunia yote kule ambako tentacles zao za uizi na unyonyaji zinafika. N a kwa mantiki hiyo ndiyo maana nimesema mahali fulani humu JF kuwa kama hawahitaji au hawatuhitaji sisi na malighafi zetu, why all that noise. Si waende wakanunue huko kwingine.

Halafu ni nyinyi Watanzania wachache mlioiva kwa kasumba ya mabeberu ndio mnasema eti hawahitaji malighafi zetu! Sasa mbona wapo hapa na kla kukicha wanafungua balozi zao hapa na sisi wanaturuhusu tufungue balozi zetu huko kwao? Hiki ni kipimo kuwa TUNAHITAJIANA ila kuwe ni kwa heshima na adabu kama diplomasia ya kimataifa inavyotaka. Siyo ya kusikiliza kelele za akina BOB na Lissu wake hasa baada ya kushindwa MISEREBLY IN THE BALLOT BOX!
 
Mbona mnapenda mno kuwatukana wenzenu? Hivi kuna mali ghafi ipi ambayo Ulaya haiwezi kupata kwengine kuliko Tanzania? Nadhani hauelewi kuwa sehemu kubwa ya Ulaya imetoka katika uchumi wa viwanda. Viwanda vya nguo viko Bangladesh, Cambodia n.k. kahawa inayopendwa na wengi ni ya Ethiopia na Columbia, chai ni kutoka Kenya na India, maua ni kutoka Kenya na Ethiopia, machungwa kutoka Spain na Misri, ndizi zinatoka Latin America, gas wanatoa Urusi na Qatar, korosho wananunua kutoka Vietnam na India ambao nao wananunua kutoka kwetu, msumbiji na Afrika Magharibi. Madini yapi ambayo tunazalisha yanachangia katika uchumi wao? Almasi wanatoa Botswana, dhahabu inazalishwa zaidi na Ghana na Afrika Kusini kuliko sisi. Msijidanganye, mpaka sasa ni sisi ndio tunaowategemea zaidi kuliko wao wanavyotutegemea. Au unadhani hizo ndege tumenunua ili sisi twende tukatalii Ulaya na sio wao waje kwetu kutalii?

Amanda...
Ujobile (Umeongea)
 
Taja hizo malighafi wanazozitegemea sana kutoka Tanzania.Hatuna uzalishaji wowote mkubwa kiasi chakutufanya tuwe hatarishi kwao.Hizi porojo zilitakiwa kutolewa miaka ya nyerere sio sasa.Hao watu wangekua tegemezi kwa kila kitu afrika usidhani wangetuacha tukae kienyeji hivi.Kilichopo ni sisi kuangaika kuuza rasilimali zetu kwao ili zitunufaishe nasio vinginevyo.Hayo makampuni yanayokuja uku kufanya lobbyng kuhusu rasilimali zetu zisikupe jeuri ukajiona una cha muhimu sana.
Sasa wewe ndio unayasemea hayo makampuni, mbona yako hapa siku nyingi na yanazidi kuja kununua, kuzalisha na kuchakata malighafi zetu kwa misingi ya usawa wa on win - win scenario. Wewe waza mambo ya zamani wakati nchi inafaidika na mahusiano ya kibiashara na hayo makampuni unayosema hayaangaiki na malighafi zetu! Nenda kaone uzalishaji kwenye EPZA ndiyo utajua hali halisi badala ya kuishia kumeza propaganda za Lissu na BOB!
 
We zwazwa kweli kweli, ina maana izo raw materials zinapatikana Tanzania pekee?? Assume zisingekuwepo TZ wasingekuwa na pa kuzipata??
We zwazwa pia fara sana
Haya ona huyu mwingine hapa, hana hoja yoyote ya maana ila matusi tu. Hongera for your dirty mouth!
 
Ile ilikuwa ni kamati ya bunge la EU inayodeal na nchi za Atrika, kwa hiyo ni sehemu ndogo mno ya bunge la EU lenye wabumge takribani 700, kamati hiyo ina wajumbe 70 unaweza kuona wajumbe waliochangia Jana hawafiki hata 10 na yale yalikuwa ni mawazo ya wajumbe hao ambao pia hawakufikia consesus. Kwa hiyo maamuzi ya kusitishwa misaada kwa Tanzania hayawezi kufanywa na kamati peke yake tena yenye uwakilishi mdogo kiasi hicho.
Kwa hiyo, vip hizo fedha za Corona ni kweli? Kama za Rambo rambi zilipigwa na hizi za Corona zimefanya nini?
 
Wewe bila shaka ni kijana wa juzi na haujui hali ilivyokuwa nchini baada ya vita vya Kagera. Hali ile ilitokana na wenye fedha zao kutaka zifanyike structural reforms katika mambo ya uchumi. Haukuweko wakati tunapigiwa muziki London na kwingineko ili kushinikiza mataifa ya magharibi kutusamaa madeni yaliyotokana na fedha tulizokopa wenyewe. Haukuweko wakati watu wanazungusha kibakuli Dovos kumpa Mkapa ili zimsaidie kununua vyandarua.

Wewe na wengine mnadhani hii ni mara ya kwanza sisi kujimwambafai na kusema tusiingiliwe kwenye mambo yetu. Mwaka 1999 tulipotaka kununua Radar kutoka BAE tulionywa sana na mabeberu kuwa tunauziwa kitu ambacho hakitufai na kwa bei isiyoendana na uhalisia. Tukawaambia watukome, tukanunua radar. Wote tunajua hatma ya hii hadithi. Mabeberu waliwafuatilia BAE ( kampuni ya kwao) na kugundua kuwa walitupiga sana kwenye ule mradi na kuwataka waturudishie kiasi kikubwa tu cha fedha.

Kuna mwaka tulitaka kumnunulia Rais wetu ndege. Tukaonywa sana lakini Waziri musikaali wa wakati ule akawaambia mabeberu kuwa tuko tayari kula nyasi ili Rais wetu apate ndege ya saiz yake. Wote tunajua mheshimiwa huyo aliishia wapi!

Waliotutangulia walituasa kuhusu umuhimu wa kuchagua vita tunazopigana. Nyingine, kama hii haina tija na hatuna sababu ya kuishupalia.

Amandla...
Wewe ndio haukuwepo WAKATI MWALIMU JULIUS K. NYERERE ALIPOWATIMUA WAJERUMANI NA MISAADA YAO. Akawafurusha na kuwaambia waondoke na wachukue hata makarai na masepeto yao. Nadhani ulikuwa bado kijijini, hivyo kusikia lugha na maneno kama hayo asemayo Rais Magufuli na Prof. Kabudi, kwako ni maneno mapya, ambayo kwa kweli hujayasikia tangu miaka ya enzi za RUKSA. Tumeanza kuyasikia SASA, yaani kuanzia 2015! Hivyo unaposema hayo usemayo, binafsi sishangai kwani kizazi cha leo kimezoea na kimeaminishwa kuwa bila EU au US au UK hakuna maendeleo! This is BULL S***! Kama nikim - quote djt (if you what Imean)!
 
Ile ilikuwa ni kamati ya bunge la EU inayodeal na nchi za Atrika, kwa hiyo ni sehemu ndogo mno ya bunge la EU lenye wabumge takribani 700, kamati hiyo ina wajumbe 70 unaweza kuona wajumbe waliochangia Jana hawafiki hata 10 na yale yalikuwa ni mawazo ya wajumbe hao ambao pia hawakufikia consesus. Kwa hiyo maamuzi ya kusitishwa misaada kwa Tanzania hayawezi kufanywa na kamati peke yake tena yenye uwakilishi mdogo kiasi hicho.
Kwa hiyo kama uchache wa wajumbe wa hiyo kamati ni hoja kwamba walichozungumza hakina maana, je ile kamati kuu ya ccm haina maamuzi yoyote? Hoja zijibiwe ipasavyo. Kutafuta vichaka vya kujificha hakutusaidii chochote kama taifa.
 
Ujobile (Umeongea)
Inawezekana kweli "ameongea", lakini tuelezeni basi wanatafuta nini hapa TZ kama wanaweza kupata hivyo mnavyo taja huko kwingine!? Mbona hata takwimu zao za kiuchumi na kibiashara wanaonyesha hizo malighafi na mazao ya TZ?! Hivi hayo majarida ya WEF, ITO, EU Economic Bank, WB na mengine mengi yanajidanganya yenyewe? Au ndio wale wanajikuna na kisha kucheka wenyewe? Kama msemo wetu wa Kiswahili usemavyo!?
 
Wewe ndio haukuwepo WAKATI MWALIMU JULIUS K. NYERERE ALIPOWATIMUA WAJERUMANI NA MISAADA YAO. Akawafurusha na kuwaambia waondoke na wachukue hata makarai na masepeto yao. Nadhani ulikuwa bado kijijini, hivyo kusikia lugha na maneno kama hayo asemayo Rais Magufuli na Prof. Kabudi, kwako ni maneno mapya, ambayo kwa kweli hujayasikia tangu miaka ya enzi za RUKSA. Tumeanza kuyasikia SASA, yaani kuanzia 2015! Hivyo unaposema hayo usemayo, binafsi sishangai kwani kizazi cha leo kimezoea na kimeaminishwa kuwa bila EU au US au UK hakuna maendeleo! This is BULL S***! Kama nikim - quote djt (if you what Imean)!
Na ulivyokuwa mpuuzi ukisikia hivyo unadhani inayozungumziwa ni hii ujerumani ya sasa. Ni kweli kabisa bila kushirikiana na nchi za magharibi hamna maendeleo.

Siwezi kuendelea kujadiliana na mtu anaesema " if you what I mean". Na anaedhani Donald J Trump ndie aliyebuni neno Bull s***.

Kama wewe ndio mfano wa watu walioelimika na ndio tunaowategemea katika mpambano na mabeberu, bora nibakie kijijini.

Amandla...
 
Naweza kusema kwa uhakika kabisa BILA KUJING'ATA ULIMI kuwa this can be the shallowest bandiko humu JF kwa 2020! Kwa nini nasema hivyo? Ni kwa sababu haingii akilini mtu kusema kuwa hizo nchi tajwa hazina shida na uchumi wa TZ! Kweli? Hata wao wakisoma hili bandiko watakushangaa. Wanahitaji malighafi karibu zote kutoka nchi zetu, ikiwemo TZ.

Wanahitaji madini yote, wanahitaji pamba yote, wanahitaji chochote atakachofikiria mtu makini humu JF. Nadhani mara ya mwisho ulipokwenda Ulaya au US au UK hukutembea na kuona how dependent they are on our raw materials and ALL CHEAP GOODS from our countries including TZ. Kama hawahitaji kitu, sasa wanahitaji nini - UTAWALA BORA NA HAKI ZA BINADAMU - for what kama siyo kutengeneza njia rahisi za kuiba malighafi zetu!?
Majizi yasituingize kwenye wizi na dhulma yao! Majibu yanahitajika ziko wapi 27m Euro? Si maombi ya siku tatu yalitosha? Hela ya watu irudi wasituhusishe hawa viwavi walafi! Eti
Hela yetu mlifanyia nini? Mbona hamkufuata vigezo vya WHO?
Majibu:
Sisi hatujawahi kushindwa vita yoyote!!
Ohh vita ya kiuchumi!!!
Ohh tutachagua dignity badala ya utajiri!!!
Mafi pumbafu "macho kumchuzi" rudisha hela ya watu kha!
 
Inawezekana kweli "ameongea", lakini tuelezeni basi wanatafuta nini hapa TZ kama wanaweza kupata hivyo mnavyo taja huko kwingine!? Mbona hata takwimu zao za kiuchumi na kibiashara wanaonyesha hizo malighafi na mazao ya TZ?! Hivi hayo majarida ya WEF, ITO, EU Economic Bank, WB na mengine mengi yanajidanganya yenyewe? Au ndio wale wanajikuna na kisha kucheka wenyewe? Kama msemo wetu wa Kiswahili usemavyo!?
Labda tungerudi kwenye kiini cha mjadala huu ambao umemwagiwa 'petroli' na majibu ya Waziri wetu Kabudi.
1. Je ni kweli kuwa Tz tuliomba na kupokea fedha kutoka EU kwa ajili ya kupambana na COVID 19?
2. Majibu na tambo za Waziri wetu vinahusianaje na swala hilo?
 
Back
Top Bottom