Nawapongeza na kuwashukuru wanasheria wa CHADEMA, ni mfano

Nicholas

JF-Expert Member
Mar 7, 2006
25,260
7,195
Bila kupepesa macho salamu na shukrani zangu za mwaka mpya naelekeza ktk timu ya wanasheria wa CHADEMA. Kwa weledi, tenacity na mioyo yao mikubwa. Itakuwa mbaya kama siasa, itikadi au chuki binafsi zitatupeleka kumkufuru Muumba, kwa kuacha mshukuru na kuwapongeza hawa Wataalamu. Hawa jamaa ni mfano mzuri hadi kwa wanasheria wa serikali.

Sasa hivi kuna kila dalili kwamba wanasheria wa serikali wakiamka lazima waangalie ni jinsi gani watajipima au kujikumbusha mengi kutoka katika hii timu ambayo ipo busy sana, hawana kivuli cha dola ila wana jina baya la kuhalishwa nao kuhitajai tetea na roho zao.

Nawaheshimu, nawakubali, natangaza hadharani na kwa sauti kubwa hawa jamaa wametukuka. Asiyetukuka hayopo nao na alipo anapigania roho yake kiweledi na kisiasa.

Kwanini basi basi nawashukuru na kuwapongeza na kumshukuru Mungu kwa hawa jamaa?

1.Hawa jamaa hawana woga wa kucheza mechi katika un equal grounds. Hawa jamaa wanacheza mechi katika viwanja idara zote hazipo huru.

2. Hawa jamaa wana lundo la kesi za kupambana: zao binafsi, dhidi ya chama chao, dhidi ya viongozi wao, dhidi ya wanachama wao, dhidi ya waandishi, wachapishaji, raia wasiokuwa na itikadi etc. Kesi nyingine hata walio ansisha hawakumbuki kwanini walianzisha,ila kwa vile wapo katika dola, basi wanabadili gia angani kila wapendavyo, kesi nyingine zimefunguliwa na watu wanaogoopa kujiona katika kioo au kuambiwa taswira zao, kesi nyingine ni watu hawataki kukubali uzee kisiasa. Wengine hawataki kubali kwamba wameshindwa kwa haki, hata kama mechi haikuwa ya haki (kama obama na clinton wanavyohangaika).

3. Uendeshaji wa kesi nyingi umekuwa kama mizaha.Wanasheria wa upande wa walalamikaji kwa vile wapo chini ya nguvu za nje ya uwanja wanaamua tuu kufanya vitu vya kujaribu jionesha kwamba wanaweza.Yote haya hayajawakwaza hawa jamaa.

4. Wanasheria wa CHADEMA kupitia bunge wameweza onyesha watanzania kwamba sasa ni wakati wa kuamka. Si kuamini amini tuu kila office kwa vile ina jina zuri na imepigiwa upatu mkubwa. Hata office ya mwanasheria mkuu imekimbizwa mchaka mchaka katika bunge. Tumeshughudia hadi ikibidi speaker wa bunge aiokoe office. Wanasheria wengine wa ni nai wasijfunze hapa?

5. Wanasheria wa CHADEMA hawajapewa haki sawa katika vyombo vya habari na masikio ya wananchi. Wamepewa majina mabaya (Mpe mbwa jina baya ili umuue), hii imewaongezea mileage kila mara lazima wajithibitishe kabla ya kufanya ndipo waaminike walichofanya na mara nyingine hata wasipotendewa haki, inakuwa kazi kuuambia umma haki haikutendeka. Na asiyetoa haki kuondaka bila hatia yake.


6. Wanasheria ya wa CHADEMA ni mfano hata kwa wanasheria maarufu waliotangulia. Kwamba unaweza shinda kesi dhidi ya dola, unaweza shida kesi bila kuhonga hata km mazingira yote yanakwenda nje ya sheria. Hawa jamaa ni mfano.

8. Wanasheria wa CHADEMA wameonyesha busara, wamonyesha utulivu hata pale kila kitu kinafanywa kuonekana km mzaha.

9.Wanasheria wa CHADEMA, wamenifanya nijulize hawa jamaa ni wajapani au.Muda gani wanajiandaa kama mashauri yaliyopo mahakamani ni bandika bandua. Na yapo nchi nzima? Hawa jamaa PAMOJA NA KWAMBA WENGINE ,DHAMAN ZAO NI MTEGO MWINGINE KWAMBA WASITOKE NJE YA MAENEO FULANI.ILA HAWA JAMAA NI UNDETERRED UN STOPPABLE.

NAPENDA WASHUKURU, NAPENDA WAPONGEZA. NAWAOMBA WASIFE MOYO.NAWAOMBA WAJUE KAZI YAO NI NOBLE NA HATA WAO WAKIZEEKA AU KUPOTEZWA WALISHOFANYA HAKITOFUTIKA.

NAWAOMBA WAJUE ADUI NI MWOGA, NA JINSI ANAVYOKARIBIA KUSHINDWA KWA UKOSEFU WA MAADILI YUPO TAYARI KUFANYA KILA UOVU AKIDHANI ANAOKOA ROHO YAKE KUMBE ANAONGEZA KOSA ZAIDI ILI ATAKAPOSHINDWA APATE ADHABU KUBWA ZAIDI.

NAWAOMBA WAJUE KUNA WATANZANIA WAMESHAATHIRIKA NA MTESI WAO KWA KIASI HAWAWEZI TENA HATA OTA KM SIO KUFIKIRI KWAMBA KUNA MAISHA NJE YA MATESO, NA HAYO MAISHA YAPO VIPI ILI HAA WAWEZE LINGANISHA NA MATESO. WARUSI WALIMKA SIKU MOJA WAKAJIKUTA UKOMMUNIST UMETOWEKA. HAWAKUAMINI KWA JINSI ULIVYOKUWA UKITISHA NA KUHOFIWA KULIKO MUNGU.

WENGINE HAWAKUWA WAMEJIANDAA KUWA HURU KIFIKRA,NA ILICHUKUA MUDA KUKUBALIANA NA HALI. WENGINE WALISHANGAA EXPERIENCE MPYA KM YUE KIPOFU ALIYEPEWA KUONA NA YESU.YOTE HAYO NI SEHEMU YA EXPERIENCE YA WATANZANIA.

KATIKA HAO WATANZANIA WENGINE WATAKUWA KIKWAZO KAMA WATU WANAOZAMA,WANAVYOJARIBU KUWA WABINAFSI ILI WAOKOLEWE WAO KWANZA HATA MWOKOAJI AKIFA SIO SHIDA, KWA VILE HAWAJUI MWOKOAJI AKIFA NAO NA WENGINE WATAKUFA. NAOMBA MSIWAOGOPE HAO.

MUNGU IBARIKI TANZANIA, MUNGU UTOKOMEZE UJAMAA NA MIZIZI YAKE YA KISHETANI. NA AKILI ZA ZA KISHETANI KTK VICHWA VYA WAJAMAA WANAOUA KILA AINA YA UHURU WA RAIA ULIOWAUMBA NAO WATU. WOTE WANAOPINGA NJIA ZA KIUCHUMI ZINAZOWAFAIDISHA WACHAPA KAZI NA WENYE KUTUMIA AKILI NA MAADILI VYEMA.
 
Wanasheria wa chadema wanafanya kazi ya Mungu hawawezi kushindwa na shetani .
Sio muda mrefu ushetani ktk hii nchi utatoweka ghafla kama UKOMUNIST, au km waliokuwa wakiendesha kampeni kule arusha kipindi tulichoshuhudia mashambulizi soweto, Kabla kura kuhesabiwa walishahama mji.
 
Sio muda mrefu ushetani ktk hii nchi utatoweka ghafla kama UKOMUNIST, au km waliokuwa wakiendesha kampeni kule arusha kipindi tulichoshuhudia mashambulizi soweto, abla kura kuhesabiwa walishahama mji.
Very true .
 
Wanasheria pande zote wapo vizuri upstairs,mimi wakija mahakamani naona wako safi ,labda kama kuna ka uzembe flani,you know?
 
Wanasheria pande zote wapo vizuri upstairs,mimi wakija mahakamani naona wako safi ,labda kama kuna ka uzembe flani,you know?
mkuu kaite kauzembe, kaite kukosa maadili.lakini akili huathirika na maadili ad vise versa. Critical decision haziamuliwi na matomaso.Ukishakuwa ktk wrong place na una option ya kutoka na kuna wengine wametoka na wamethibitishe kuna life upande wa pili no matter how tough it appears.HUwezi jisfu un akitu upstairs.Ni kwamba hawajitambui ndio maana wanapigana vita ya kujikuza tuu.
 
Mtoa mada elewa kwamba huwezi elewa ubora au udhaifu wa learned brothers or sister kama ww n layman

Kwa hyo naamn hata ulichokiandka hukielew
 
Hao ni wanasheria au wanasiasa, kimsingi mimi sio kama ni wanasheria bali nawaona ni wanasiasa kwa jinsi wanafanya kazi zao.
 
Wambie basi hao watetezi wa wanyonge wasaidie kumuuliza Mbowe alipo Ben
 
Mtoa mada elewa kwamba huwezi elewa ubora au udhaifu wa learned brothers or sister kama ww n layman

Kwa hyo naamn hata ulichokiandka hukielew
Acha akili za kukariri wewe,sasa unamwelewaje Mungu kuwa ni mzuri wakati hata kumwona humwoni na Elimu za mbingu hata ktk internet hazipo?Unajuaje mvua zinakuja wakati hujasomea hayo mambo na kuwa na hizo degree. Matendo yao mengine hayahitaji degree kujua.Na kuna vitu vingine havijawekewa mipaka wao tuu ndo wajue ndio maana kuna vitabu,kuna material kibao kwa kila mtu kuyapata.Hata katiba na sheria zetu zipo .Sasa katiba na sheria nyingine ziliandikiwa wasomi tuu?
 
Wambie basi hao watetezi wa wanyonge wasaidie kumuuliza Mbowe alipo Ben
Kwanini wewe usianze ,au wewe ndio mpanga majukumu?Your very horrible mkuu, unajipa kibarua cha kupangia kazi watu, huku ukiwahukumu wakati wanazofanya huwezi fanya,wala hupendi kwa vile unadhani unajipenda sana kuliko wao na njia nyepesi ni kujibanza na uovu.Kamulize wassira km hata kuna miezi 12 keshasahaulika na jeuri yake yote.
 
Hao ni wanasheria au wanasiasa, kimsingi mimi sio kama ni wanasheria bali nawaona ni wanasiasa kwa jinsi wanafanya kazi zao.
Wakati ubongo unakuwa disconnected na utu.Hata usome degree ngapi utabaki kuwa km kitabu kilichoandikwa vitu vingi ila hayo yote hayana connection na vitabu wala kitabu hakiwezi jisifu kwamba kinajua mambo mengi. Hao jamaa sio practically sio wanasheria wala wanasiasa, ni watu wanajibamiza ktk matukio ya sheria na siasa.
 
Back
Top Bottom