Nawapenda rafiki zangu kuliko ndugu zangu.

Husninyo

JF-Expert Member
Oct 24, 2010
23,724
9,188
Ndugu wengi ni watu wa lawama, hawana jema jamani. Hawawezi kukufanyia zuri na zuri utakalowafanyia wewe hawana shukrani nalo.
Wengi ni wasiopenda kuona unafanikiwa hata sijui kwanini.
Kuwasiliana au kuonana ni hadi kwenye matukio eg msiba au harusi.
Wale waliofanikiwa huwa ni wenye kujisikia na wale wenye hali za chini hujiona dhaifu.
Jamani mnafanyaje kukabiliana na ndugu wa aina hizo?
 
Hongera. Ukipata rafiki wa kweli umepata tunu. Ndugu wengi kwa hakika wana mauzauza. Wana wivu, husuda, ukiwasaida whawaoni kipya kwani wanaona ni haki yao. Ndugu huumizana (rejea Abeli na Kaini; Yusufu na nduguze = wana wa Isaka, nk katika maandiko matakatifu) na kutendeana kila aina ya uovu.
 
Kweli kabisa uyasemayo. Mi nimefika point ambayo nikiwa na inshu inanitatiza ushauri nitauomba kwa rafiki,ndugu nitamjulisha tu juu ya maamuzi yangu kama itabidi sana. Nashukuru Mungu nina rafiki ambao ni yaidi ya ndugu.
 
Hujatueleza ni ndugu wa vipi! Shangazi, mjomba binam, bibi au wakuzaliwa nao? sikatai kuna wanandugu hawafai. Lakini kumbuka ndugu hasa wa damu hata ukilost hawata kutupa lakini ni bahati sana kupata rafiki wa hivyo. Nina uzoefu na marafiki na ndugu walio fanya mambo ya ajabu na mazuri. Tueleze kategori ya ndugu unao maanisha
 
Ndugu wengi ni watu wa lawama, hawana jema jamani. Hawawezi kukufanyia zuri na zuri utakalowafanyia wewe hawana shukrani nalo.
Wengi ni wasiopenda kuona unafanikiwa hata sijui kwanini.
Kuwasiliana au kuonana ni hadi kwenye matukio eg msiba au harusi.
Wale waliofanikiwa huwa ni wenye kujisikia na wale wenye hali za chini hujiona dhaifu.
Jamani mnafanyaje kukabiliana na ndugu wa aina hizo?

Haya mambo hayana fomula YEYOTE AWEZA KUTOSA ndugu au rafiki
 
Ndugu wengi ni watu wa lawama, hawana jema jamani. Hawawezi kukufanyia zuri na zuri utakalowafanyia wewe hawana shukrani nalo.
Wengi ni wasiopenda kuona unafanikiwa hata sijui kwanini.
Kuwasiliana au kuonana ni hadi kwenye matukio eg msiba au harusi.
Wale waliofanikiwa huwa ni wenye kujisikia na wale wenye hali za chini hujiona dhaifu.
Jamani mnafanyaje kukabiliana na ndugu wa aina hizo?
Let me tell you one thing: Unawependa ndugu zako bali rafiki zako unawafurahia. Mungu ndio anatupenda sisi wanadamu, no matter tunamkosea vipi lakini upendo wake kwetu bad upo. Wengine tunafurahiana tu na si kupendana, unadai unampenda mkeo kwa sababu anakufurahia, anakupikia, anakuliwaza wakati wa huzuni, haya asipoyaonyesha upendo unaisha na unatafuta nyumba ndogo ili uyapate. Upendo hauna kikomo, sie twafurahiana na hatupendani!
 
Hujatueleza ni ndugu wa vipi! Shangazi, mjomba binam, bibi au wakuzaliwa nao? sikatai kuna wanandugu hawafai. Lakini kumbuka ndugu hasa wa damu hata ukilost hawata kutupa lakini ni bahati sana kupata rafiki wa hivyo. Nina uzoefu na marafiki na ndugu walio fanya mambo ya ajabu na mazuri. Tueleze kategori ya ndugu unao maanisha

ndugu wote ukiacha wa kuzaliwa nao tumbo moja.
 
Let me tell you one thing: Unawependa ndugu zako bali rafiki zako unawafurahia. Mungu ndio anatupenda sisi wanadamu, no matter tunamkosea vipi lakini upendo wake kwetu bad upo. Wengine tunafurahiana tu na si kupendana, unadai unampenda mkeo kwa sababu anakufurahia, anakupikia, anakuliwaza wakati wa huzuni, haya asipoyaonyesha upendo unaisha na unatafuta nyumba ndogo ili uyapate. Upendo hauna kikomo, sie twafurahiana na hatupendani!

mi nafikiri kupenda na kufurahia vinaendana pamoja.
Hivi unaweza ukakifurahia kitu wakati hukipendi?
Au unaweza ukakipenda kitu huku haukifurahii?
Labda unieleweshe zaidi juu ya hilo.
 
mi nafikiri kupenda na kufurahia vinaendana pamoja.
Hivi unaweza ukakifurahia kitu wakati hukipendi?
Au unaweza ukakipenda kitu huku haukifurahii?
Labda unieleweshe zaidi juu ya hilo.

Upendo hauna kikomo
Furaha na upendo ni vitu tofauti
Mvuta sigara anapenda kuvuta sigara au anafurahia tendo la kuvuta sigara?
 
ndugu wote ukiacha wa kuzaliwa nao tumbo moja.

Kwa hilo lisikuu mize kichwa hapo nakuunga mkono 61% Unachotakiwa
1. Ishinao kimjini mjini
2. Watu wapo busy na kuonana ni kwenye matukia ni sawa
3. Kama upo Dsm foleni inasababisha watu wasitembeleane/inatia uvivu
4. '' '' Kupanda daladala kunachosha (kwa asiye na gari)
5. Acha mtindo wa kutafutiana viwanja jirani na unapoishi Sio lazima wote muishi kimara nk
6. Unapoishi mbali heshima na upendo vinaongezeka
7. Ukifuata hayo utapendana na hao ndugu japo kwa hizo 61%
 
Upendo hauna kikomo
Furaha na upendo ni vitu tofauti
Mvuta sigara anapenda kuvuta sigara au anafurahia tendo la kuvuta sigara?

mmmh! Hata sijui. Kama kuna mvutaji humu atatujibu.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom