nngu007
JF-Expert Member
- Aug 2, 2010
- 15,862
- 5,797
[h=3][/h]
ETI wanachama 700 wa Yanga walikutana Jumapili makao makuu ya klabu, makutano ya mitaa ya Twiga na Jangwani, Dar es Salaam na kufikia uamuzi wa kumngoa madarakani Mwenyekiti, Wakili Lloyd Bahargu Nchunga.
Mapinduzi haya yaliongozwa na Mzee Ibrahim Akilimali, ambaye kihistoria nilishasema siku nyingi ni mzee kinara wa migogoro na mvuruga amani klabuni.
Kweli, Nchunga ameshindwa kuongoza Yanga na sababu kubwa ni uelewa wake mdogo katika masuala ya michezo na kukosa ushirikiano kutoka kwa Wajumbe wenzake wa Kamati ya Utendaji na wadau wengine wa klabu, wakiwemo hao wanaojiita wazee.
Lakini ukirejea uchaguzi uliomuweka madarakani Nchunga Jumapili ya Mei 18, mwaka 2010, alishinda Uenyekiti baada ya kupata kura 1,437, akiwaangusha wapinzani wake wanne, Francis Kifukwe aliyepata kura 370, Mbaraka Igangula aliyepata kura 305, Abeid Falcon aliyepata kura 301 na Edgar Chibura aliyeambulia kura 65 katika kura 2,220 zilizopigwa, wakati kura 23 kati ya hizo ziliharibika.
Kura 370 za Kifukwe na 305 za Igangula kwa pamoja wakichanganya, bado hawawezi kufikia kura za Nchunga- ina maana alishinda kwa kishindo. Inakuwa rahisi kuhisi watu hawa 700 waliokutana Jumapili ni wale wale 700 waliomnyima kura Nchunga PTA Mei 18, 2010.
Sitaki kuzama ndani sana- kwa sababu nimeshapitisha sera ya kutoandika habari za migogoro- lakini kwa pamoja na wasomaji wangu napenda tujadili, kiongozi aliyeshinda kwa kura 1,437 anaweza kungolewa madarakani na watu 700?
Tena watu ambao hakuna aliyewahakiki kama kweli ni 700 na hakuna aliyehakikisha kama kweli ni wanachama wa Yanga? Tujadili.
LLOYD NCHUNGA
MWENYEKITI WA KAMATI YA UCHAGUZI YA YANGA, RIDHIWAN KIKWETE AKITANGAZA MATOKEO MEI 19, 2010, KULIA NI MFADHILI WA KLABU HIYO, YUSUF MANJI
MAKAMU MWENYEKITI, DAVIS MOSHA AKITOA SHUKURANI KWA WANACHAMA
SARAH RAMADHAN ALIYESHINDA UJUMBE WA KAMATI YA UTENDAJI
ALLY MAYAI TEMBELE ALIYESHINDA UJUMBE
CHARLES MUGONDO ALIYESHINDA UJUMBE
THEOFRID RUTASHOBORWA (SASA MAREHEMU) ALIYESHINDA UJUMBE
SALIM RUPIA ALIYESHINDA UJUMBE
MZEE YUSSUF ALIYESHINDA UJUMBE
MOHAMMED BHINDA ALIYESHINDA UJUMBE
ETI wanachama 700 wa Yanga walikutana Jumapili makao makuu ya klabu, makutano ya mitaa ya Twiga na Jangwani, Dar es Salaam na kufikia uamuzi wa kumngoa madarakani Mwenyekiti, Wakili Lloyd Bahargu Nchunga.
Mapinduzi haya yaliongozwa na Mzee Ibrahim Akilimali, ambaye kihistoria nilishasema siku nyingi ni mzee kinara wa migogoro na mvuruga amani klabuni.
Kweli, Nchunga ameshindwa kuongoza Yanga na sababu kubwa ni uelewa wake mdogo katika masuala ya michezo na kukosa ushirikiano kutoka kwa Wajumbe wenzake wa Kamati ya Utendaji na wadau wengine wa klabu, wakiwemo hao wanaojiita wazee.
Lakini ukirejea uchaguzi uliomuweka madarakani Nchunga Jumapili ya Mei 18, mwaka 2010, alishinda Uenyekiti baada ya kupata kura 1,437, akiwaangusha wapinzani wake wanne, Francis Kifukwe aliyepata kura 370, Mbaraka Igangula aliyepata kura 305, Abeid Falcon aliyepata kura 301 na Edgar Chibura aliyeambulia kura 65 katika kura 2,220 zilizopigwa, wakati kura 23 kati ya hizo ziliharibika.
Kura 370 za Kifukwe na 305 za Igangula kwa pamoja wakichanganya, bado hawawezi kufikia kura za Nchunga- ina maana alishinda kwa kishindo. Inakuwa rahisi kuhisi watu hawa 700 waliokutana Jumapili ni wale wale 700 waliomnyima kura Nchunga PTA Mei 18, 2010.
Sitaki kuzama ndani sana- kwa sababu nimeshapitisha sera ya kutoandika habari za migogoro- lakini kwa pamoja na wasomaji wangu napenda tujadili, kiongozi aliyeshinda kwa kura 1,437 anaweza kungolewa madarakani na watu 700?
Tena watu ambao hakuna aliyewahakiki kama kweli ni 700 na hakuna aliyehakikisha kama kweli ni wanachama wa Yanga? Tujadili.
LLOYD NCHUNGA
MWENYEKITI WA KAMATI YA UCHAGUZI YA YANGA, RIDHIWAN KIKWETE AKITANGAZA MATOKEO MEI 19, 2010, KULIA NI MFADHILI WA KLABU HIYO, YUSUF MANJI
MAKAMU MWENYEKITI, DAVIS MOSHA AKITOA SHUKURANI KWA WANACHAMA
SARAH RAMADHAN ALIYESHINDA UJUMBE WA KAMATI YA UTENDAJI
ALLY MAYAI TEMBELE ALIYESHINDA UJUMBE
CHARLES MUGONDO ALIYESHINDA UJUMBE
THEOFRID RUTASHOBORWA (SASA MAREHEMU) ALIYESHINDA UJUMBE
SALIM RUPIA ALIYESHINDA UJUMBE
MZEE YUSSUF ALIYESHINDA UJUMBE
MOHAMMED BHINDA ALIYESHINDA UJUMBE