buzitata
JF-Expert Member
- Apr 11, 2017
- 1,997
- 7,067
Kwa sisi ambao tumepitia ujasusi wa saikolojia tunajua lengo la Uzi wako ni kuitambulisha hiyo LGBT ili mapunga wasikate tamaa wakijua wanawatetezi wengi.View attachment 2036928
Abuu Kauthar
Nianze kwa kuelezea uzoefu wangu katika maisha wa kukutana na kuwajua mashoga. Nianze kwa kuomba msamaha kwa jina hilo kwani sina hakika kama ni rasmi na linakubalika kwao.
Nimepata kujuana na mashoga watano. Najua kuna makundi mengi katika hao wanaojitambulisha kama jamii ya LGBT, lakini nikizungumzia mashoga ninakusudia wanaume wanaofanyiwa mapenzi kupitia tundu la nyuma, ambalo limezoeleka kama ni kwa ajili ya kutolea mavi.
Watu hao watano ninaowajua wana jambo moja linalofanana. Wote waliingia kwenye tabia hiyo utotoni baada ya kunyanyaswa kwa muda mrefu, kingono. Mmoja wapo, nilimjua katika taasisi moja ya elimu, alinambia alifanyiwa mambo hayo na baba yake mdogo, mwingine ambaye ni mdogo wangu wa mama mdogo alinyanyaswa utotoni na jirani.
Mwingine ni kijana wa Kiarabu kule Dodoma ambaye alikuwa rafiki wa mjomba angu, akisoma shule ya Mazengo. Mara kadhaa alimfuata mjomba kumuomba amuombee dua aache tabia hiyo na kukiri kuwa ina uraibu mkubwa, kama wa sigara kwa liayezoea kufanyiwa. Kijana huyo naye alianzishwa mambo hayo utotoni na watu wazima katika familia yake. Katika hao watano, kila mmoja alikuwa na hadithi yake.
Sina sababu ya kutowaamini kwa sababu hayakuwa mazungumzo ya kipolisi au ya kuwahukumu bali ya kirafiki kabisa.
Kule Zanzibar na hata baadhi ya maeneo mengine, tunaambiwa, vitendo vya ulawiti wa watoto ni vingi mno. Baadhi vinang’amuliwa maopema, baadhi ya vitendo hivyo havijulikani na vinaendelea na kutengeneza mashoga.
Swali langu kwa watetezi wa LGBT, hawa nao waliingia huku kwa hiari?
Sina tatizo na mtu mzima, walau kwa uchache miaka 18 na zaidi, anayejitambua tayari, kuamua kuingiliwa kinyume akaifanya ni starehe yake lakini kuingizwa huko kupitia unyanyasaji haikubaliki.
Kwa hiyo, wakati wakina Mishy Singano, Fatma Karume na wenzao wanaowatetea mashoga wakiendeleza harakati zao, wachungulie takwimu na kuona hali mbaya ya ongezeko la vitendo vya ulawiti kwa watoto wa kiume na kike, wachunguze mchango wake katika kuzalisha mashoga (bila hiari) na wajishughulishe na mapambano hayo.
Katika habari moja niliyoiona imechapwa katika tovuti ya Shirika la Habari la Ujerumani, Deutche Welle (DW) Jeshi la Polisi limenukuliwa kuwa visa vya ukatili na dhuluma ya kingono dhidi ya watoto mwaka wa 2020 ilifikia 7263 ikiwa ni ongezeko la asilimia 26 ikilinganishwa na mwaka 2015 ambapo vilirikodiwa visa 5803, hii ikiwa ni sawa na visa 615 kwa mwezi jambo ambalo linatajwa kuwa linahatarisha mustakabali wa ustawi kwa watoto nchini humo. Dhuluma hizi za kingono ndio zinazalisha uraibu wa kupenda kuingiliwa kinyume.
Hawa vijana walioingizwa katika ushoga bila kutaka kwa kubakwa mfululizo utotoni wanapitia mateso makubwa mno. Wakienda kufanyiwa vipimo, hukutwa na hali mbaya ya kiafya, wameharibika. Starehe gani hii ya kuvunja haki za watu wengine ya kuwa na afya nzuri, eti kwa kizingizio kuwa ameridhia wakati kumbe wengi wanalazimishwa kwa kuanza kubakwa?
Jambo la pili ambalo nataka kuligusia kidogo ni hii tabia ya kutumia nguvu nyingi kupromote ushoga, jambo ambalo kusema ukweli linaathiri jamii ya LGBT kuliko kuwasaidia.
Jamii ya LGBT ilikuwepo miaka na miaka na ndio maana jambo la kuingiliana kinyume wanaume kwa wanaume au hata kwa wanaume kwa wanawake limetajwa kama dhambi kwenye dini nyingi kubwa. Zamani, hasa huku Afrika, walikuwepo walivumiliwa, kama walivyovumiliwa wengine wenye tabia zisizokubalika katika jamii.
Siku hizi upinzani dhidi yao umekuwa mkubwa kwa sababu wajiitao wanaharakati (ambao wenyewe wanapambana watoto wao wa kuwazaa wasiingie huko) wanatumia nguvu nyingi kulazimisha jamii ipende na ikumbatia tabia hizi.
Mi nadhani kwanza, wanaharakati wa LGBT waanze kuchunguza vijana wengi waliingiaje huko na wana maoni gani kwa hivi sasa? Je wangependa kusaidiwa kutoka (naamini hivyo) kwa sababu wengi wanafanya kwa uraibu, kama ilivyo kwa dawa za kulevya, sio kupenda?
Lakini, nina hakika wanaharakati wa LGBT hawawezi kufanya jambo lolote litakalopunguza idadi ya mashoga, ambao wamewafanya mradi wao wakichuma mabilioni kutoka kwa wafadhili. Wanaharakati wanapenda kutuaminisha kuwa mashoga wote wamekuwa hivyo kwa sababu ya kimaumbil.e.. sijui homoni na kadhalika.
Jamani! hivi ukiwa na homoni za kike ndio uingiliwe kinyume? Kwani kwa hao wanawake huko nyuma ni rasmi kama eneo la starehe? Mi nina hakika wanaharakati nguli wa LGBT, wakina nanihii hawajawahi kutoa ‘tigo’ kwani wanajua madhara yake ila wanahimiza watoto wa kiume wa wanawake wenzao wafyokolewe nyuma! Disgusting!
Wazazi wenzangu nawashauri tuwe waangalifu. Sibishi kuwa huenda homoni fulani huchangia kumsukuma mtu kwenye ushoga, lakini tusisahau sababu kubwa ya watoto wetu kuingia huko ni unyanyasaji wa kingono.
Wazazi, tuwachunge watoto sio tu dhidi ya manyang’au watu wazima wanaowamendea kutaka kuwabaka, lakini tuwalinde watoto wasifanyiane wao kwa wao na kuzoesha na tabia hiyo chafu.
Mwenyezi Mungu atuhifadhi na tabia asizoziridhia! Aaamiin
Unatumia njia Kama Ile ya freemason walivokua wanajivumisha kwamba wanatoana kafara at the end of the day wakafanikiwa kuwa maarufu Kama walivopanga