Nawaandikia wapinzani, yaani vyama vyote vya upinzani hapa Tanzania

Petro E. Mselewa

JF-Expert Member
Dec 27, 2012
10,193
25,504
Nawaandikia wapinzani, yaani vyama vyote vya upinzani hapa Tanzania vikiongozwa na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA). Nawasihi kuwa wasithubutu kususia uchaguzi wowote utakaosimamiwa na kuendeshwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi(NEC). Hata kama hayatatokea ya Rais Maduro wa Venezuela ya kukataza waliosusa kushiriki tena, nasema kwa uwazi na uthabiti kuwa kususia uchaguzi ni kujimaliza kabisa. Hatupendi iwe hivyo!

Dunia nzima, hakuna mahali ambapo vyama vya upinzani vilisusia uchaguzi na uchaguzi husika kutofanyika. Inafahamika kuwa ni kazi pevu, dunia nzima, vyama vya upinzani kupambana uchaguzini na hata siasani na chama tawala. Sababu kuu ni mbili. Mosi, chama tawala ndicho kinachounda Serikali. Hivyo, vyombo vya dola 'huwa karibu' na mtawala.

Pili, chama tawala hakipangi wala kupenda kutoka madarakani. Hufanya kila njia ya kisiasa kubakia madarakani. Siasa, ingawa mimi si mwanasiasa, ni pamoja na mbinu, ubunifu na kuthubutu. Siasa ni mapambano ya kupambania kuongoza Serikali. Harakati zake, tangu zianze hamsini kweusi, hazijawahi kuisha. Harakati za kisiasa za kimapambano hazisusiwi. Huendelezwa.

Wapinzani wapambane kadiri ya uwanja na nafasi iliyopo. Kama mikutano imekatazwa, tumieni media kufikisha ujumbe wenu. Wananchi wakielewa mnachokisimamia watawasaidia kusimamia hoja zenu. Mabadiliko yote ya kisheria na kimfumo yatakuwa rahisi kupatikana. Hakuna ubishi mkubwa kuwa mfumo mzima wa uchaguzi wa Tanzania, ikiwemo Tume ya Uchaguzi, una dosari.

Kwa mfano, uchaguzi ngazi ya Majimbo na Kata kusimamiwa na wateule wa Mkuu wa Serikali ambaye pia ni Mwenyekiti wa chama tawala ni dosari kubwa. Ushindi kwa wapinzani, katika mazingira hayo, ni kama ngamia kupenya kwenye tundu ya sindano. Wapinzani husambaratishwa hata kwa mapingamizi na vigisu za kuchelewa kurejeshwa kwa fomu za wagombea.Hatahivyo, wapinzani hushinda.

Hakika, kuna hoja za kidemokrasia za kuzifanyia kazi katika kufanya siasa na wakati wa uchaguzi. Lakini, kususia si njia sahihi. Njia itakiwayo ni kuendeleza mapambano uchaguzini huku changamoto zikibebwa na kuelezwa kila uchao kwa namna mbalimbali. Hatimaye, mambo yatakuwa na nafuu. Lakini, kwa nchi nyingi za dunia hii, upinzani haukuwahi kucheza fair game na chama tawala. Ingawa wapo wapinzani walioibuka washindi.
 
Nawaandikia wapinzani, yaani vyama vyote vya upinzani hapa Tanzania vikiongozwa na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA). Nawasihi kuwa wasithubutu kususia uchaguzi wowote utakaosimamiwa na kuendeshwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi(NEC). Hata kama hayatatokea ya Rais Maduro wa Venezuela ya kukataza waliosusa kushiriki tena, nasema kwa uwazi na uthabiti kuwa kususia uchaguzi ni kujimaliza kabisa. Hatupendi iwe hivyo!

Dunia nzima, hakuna mahali ambapo vyama vya upinzani vilisusia uchaguzi na uchaguzi husika kutofanyika. Inafahamika kuwa ni kazi pevu, dunia nzima, vyama vya upinzani kupambana uchaguzini na hata siasani na chama tawala. Sababu kuu ni mbili. Mosi, chama tawala ndicho kinachounda Serikali. Hivyo, vyombo vya dola 'huwa karibu' na mtawala.

Pili, chama tawala hakipangi wala kupenda kutoka madarakani. Hufanya kila njia ya kisiasa kubakia madarakani. Siasa, ingawa mimi si mwanasiasa, ni pamoja na mbinu, ubunifu na kuthubutu. Siasa ni mapambano ya kupambania kuongoza Serikali. Harakati zake, tangu zianze hamsini kweusi, hazijawahi kuisha. Harakati za kisiasa za kimapambano hazisusiwi. Huendelezwa.

Wapinzani wapambane kadiri ya uwanja na nafasi iliyopo. Kama mikutano imekatazwa, tumieni media kufikisha ujumbe wenu. Wananchi wakielewa mnachokisimamia watawasaidia kusimamia hoja zenu. Mabadiliko yote ya kisheria na kimfumo yatakuwa rahisi kupatikana. Hakuna ubishi mkubwa kuwa mfumo mzima wa uchaguzi wa Tanzania, ikiwemo Tume ya Uchaguzi, una dosari.

Kwa mfano, uchaguzi ngazi ya Majimbo na Kata kusimamiwa na wateule wa Mkuu wa Serikali ambaye pia ni Mwenyekiti wa chama tawala ni dosari kubwa. Ushindi kwa wapinzani, katika mazingira hayo, ni kama ngamia kupenya kwenye tundu ya sindano. Wapinzani husambaratishwa hata kwa mapingamizi na vigisu za kuchelewa kurejeshwa kwa fomu za wagombea.Hatahivyo, wapinzani hushinda.

Hakika, kuna hoja za kidemokrasia za kuzifanyia kazi katika kufanya siasa na wakati wa uchaguzi. Lakini, kususia zi njia sahihi. Njia itakiwayo ni kuendeleza mapambano uchaguzini huku changamoto zikibebwa na kuelezwa kila uchao kwa namna mbalimbali. Hatimaye, mambo yatakuwa na nafuu. Lakini, kwa nchi nyingi za dunia hii, upinzani haukuwahi kucheza fair game na chama tawala. Ingawa wapo wapinzani walioibuka washindi.
sawa wakala wa Lukaku tumekusikia
 
Mimi nitaendelea kusisitiza ni bora kususia maana kiukweli kuendelea na uchaguzi ni kuharalisha uhuni tuliofanyiwa. Chaguzi ni gharama ya nafsi za watu na fedha. Sasa kama watu wanacharangwa mapanga na polisi haisemi lolote zaidi ya yenyewe kutuadhibu.
 
Nawaandikia wapinzani, yaani vyama vyote vya upinzani hapa Tanzania vikiongozwa na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA). Nawasihi kuwa wasithubutu kususia uchaguzi wowote utakaosimamiwa na kuendeshwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi(NEC). Hata kama hayatatokea ya Rais Maduro wa Venezuela ya kukataza waliosusa kushiriki tena, nasema kwa uwazi na uthabiti kuwa kususia uchaguzi ni kujimaliza kabisa. Hatupendi iwe hivyo!

Dunia nzima, hakuna mahali ambapo vyama vya upinzani vilisusia uchaguzi na uchaguzi husika kutofanyika. Inafahamika kuwa ni kazi pevu, dunia nzima, vyama vya upinzani kupambana uchaguzini na hata siasani na chama tawala. Sababu kuu ni mbili. Mosi, chama tawala ndicho kinachounda Serikali. Hivyo, vyombo vya dola 'huwa karibu' na mtawala.

Pili, chama tawala hakipangi wala kupenda kutoka madarakani. Hufanya kila njia ya kisiasa kubakia madarakani. Siasa, ingawa mimi si mwanasiasa, ni pamoja na mbinu, ubunifu na kuthubutu. Siasa ni mapambano ya kupambania kuongoza Serikali. Harakati zake, tangu zianze hamsini kweusi, hazijawahi kuisha. Harakati za kisiasa za kimapambano hazisusiwi. Huendelezwa.

Wapinzani wapambane kadiri ya uwanja na nafasi iliyopo. Kama mikutano imekatazwa, tumieni media kufikisha ujumbe wenu. Wananchi wakielewa mnachokisimamia watawasaidia kusimamia hoja zenu. Mabadiliko yote ya kisheria na kimfumo yatakuwa rahisi kupatikana. Hakuna ubishi mkubwa kuwa mfumo mzima wa uchaguzi wa Tanzania, ikiwemo Tume ya Uchaguzi, una dosari.

Kwa mfano, uchaguzi ngazi ya Majimbo na Kata kusimamiwa na wateule wa Mkuu wa Serikali ambaye pia ni Mwenyekiti wa chama tawala ni dosari kubwa. Ushindi kwa wapinzani, katika mazingira hayo, ni kama ngamia kupenya kwenye tundu ya sindano. Wapinzani husambaratishwa hata kwa mapingamizi na vigisu za kuchelewa kurejeshwa kwa fomu za wagombea.Hatahivyo, wapinzani hushinda.

Hakika, kuna hoja za kidemokrasia za kuzifanyia kazi katika kufanya siasa na wakati wa uchaguzi. Lakini, kususia si njia sahihi. Njia itakiwayo ni kuendeleza mapambano uchaguzini huku changamoto zikibebwa na kuelezwa kila uchao kwa namna mbalimbali. Hatimaye, mambo yatakuwa na nafuu. Lakini, kwa nchi nyingi za dunia hii, upinzani haukuwahi kucheza fair game na chama tawala. Ingawa wapo wapinzani walioibuka washindi.
Anzisha chama na ushiriki, kuandikia wapinzani nikupoteza muda. Unafiki tupa kule
 
Ha ha ha ha ha kwanza sijawahi kuwa mshabiki wa Ligi nzima ya Rugby ya Uingereza. Mimi nashabikia Barcelona na AC Milan ingawa kwasasa tunasuasua.
hAHAHAHA Eti RUGBY ya Uingereza.....kwanini RUGBY Mkuu?
kwani Mpira si magoli?Mpira si ushindi tuu...mpira si furaha?huenda watu wa EPL Ndo wanavyopenda hivyo Au kwasababau hawajaonjeshwa ligi nyingine,Au wameanza kujua mpira tuu wakaonyeshwa EPL Hakuna nyingine.Au pia matangazo Mkuu yanasaidia kujulikana sana,ila na Takwimu za Dunia zinaipa EPL Kuwa na washabaiki sana sana.
yote 9,ila Mchezaji bora wa Dunia au Ulaya kamwe hawezi kuja kutoka EPL Zaidi ya ule mwaka 2009 alipotoka Christiano ronaldo...mmoja tuu by that time wakati Spain na Italy wanatoa kila kukicha.
 
Sikubaliani na hoja. Unapokerwa na jambo ni uungwana kuonesha dhahiri kukerwa kwako. Unaweza kununa, kukataa, kususia hata kuongea kwa ukali tu. Kuendelea kufanya jambo lililo kukera ni kukubaliana nalo.
 
Kuna watu huwa wanajifanya wanawatakia mema upinzani kumbe sivyo, wanajifafanya kama washauri wema wenye lengo jema kumbe siyo,mioyoni mwao wanapenda upinzani ubaki kiendelea kuwa upinzani milele.
Watu walipigwa, waliumizwa, waliswekwa lupango, kubambikwa kesi za ajabuajabu hadi wengine kupoteza maisha. Upande mmoja unatoa rai wakae wachambue na kumaizi nini kilijiri ili kutorudia mabalaa, upande mwingine unajitia upofu na ukiziwi. Maana yake nini? Ningeshangaa sana iwapo upinzani ungeshiriki huo ujinga. Ningeona wanapenda yawakute.
 
Chadema/upinzani ukifanikiwa kususia uchaguzi na kufanikiwa kuwashawishi wapiga kura kususia uchaguzi pia hapo ndipo akili itawarudia ccm na serikali.
 
Nawaandikia wapinzani, yaani vyama vyote vya upinzani hapa Tanzania vikiongozwa na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA). Nawasihi kuwa wasithubutu kususia uchaguzi wowote utakaosimamiwa na kuendeshwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi(NEC). Hata kama hayatatokea ya Rais Maduro wa Venezuela ya kukataza waliosusa kushiriki tena, nasema kwa uwazi na uthabiti kuwa kususia uchaguzi ni kujimaliza kabisa. Hatupendi iwe hivyo!

Dunia nzima, hakuna mahali ambapo vyama vya upinzani vilisusia uchaguzi na uchaguzi husika kutofanyika. Inafahamika kuwa ni kazi pevu, dunia nzima, vyama vya upinzani kupambana uchaguzini na hata siasani na chama tawala. Sababu kuu ni mbili. Mosi, chama tawala ndicho kinachounda Serikali. Hivyo, vyombo vya dola 'huwa karibu' na mtawala.

Pili, chama tawala hakipangi wala kupenda kutoka madarakani. Hufanya kila njia ya kisiasa kubakia madarakani. Siasa, ingawa mimi si mwanasiasa, ni pamoja na mbinu, ubunifu na kuthubutu. Siasa ni mapambano ya kupambania kuongoza Serikali. Harakati zake, tangu zianze hamsini kweusi, hazijawahi kuisha. Harakati za kisiasa za kimapambano hazisusiwi. Huendelezwa.

Wapinzani wapambane kadiri ya uwanja na nafasi iliyopo. Kama mikutano imekatazwa, tumieni media kufikisha ujumbe wenu. Wananchi wakielewa mnachokisimamia watawasaidia kusimamia hoja zenu. Mabadiliko yote ya kisheria na kimfumo yatakuwa rahisi kupatikana. Hakuna ubishi mkubwa kuwa mfumo mzima wa uchaguzi wa Tanzania, ikiwemo Tume ya Uchaguzi, una dosari.

Kwa mfano, uchaguzi ngazi ya Majimbo na Kata kusimamiwa na wateule wa Mkuu wa Serikali ambaye pia ni Mwenyekiti wa chama tawala ni dosari kubwa. Ushindi kwa wapinzani, katika mazingira hayo, ni kama ngamia kupenya kwenye tundu ya sindano. Wapinzani husambaratishwa hata kwa mapingamizi na vigisu za kuchelewa kurejeshwa kwa fomu za wagombea.Hatahivyo, wapinzani hushinda.

Hakika, kuna hoja za kidemokrasia za kuzifanyia kazi katika kufanya siasa na wakati wa uchaguzi. Lakini, kususia si njia sahihi. Njia itakiwayo ni kuendeleza mapambano uchaguzini huku changamoto zikibebwa na kuelezwa kila uchao kwa namna mbalimbali. Hatimaye, mambo yatakuwa na nafuu. Lakini, kwa nchi nyingi za dunia hii, upinzani haukuwahi kucheza fair game na chama tawala. Ingawa wapo wapinzani walioibuka washindi.
Mnataka washiriki ili muwauwe tena na kuwateka na kuwakata mapanga , hapana ili watanzania wenye mtazamo tofauti na chama cha mapinduzi wabaki salama basi upinzan wasishiriki uchaguzi huo na ikiwezekana msajili wa vyama avifute kabisa vyama vyote vya upinzani tanzani maana naona watanzania wengi wana tiwa vilema na polisi kwa sababu ya huo uchuguzi na upinzani wao serikali hii haiutambui upinzani kama ni sehemu ya watanzania inaonekana wapinzani kwa serikali hii ni maadui kuliko wala rushwa . vifutwe tu ili polisi wasiendelee kubebeshwa dhabi za mauaji na damu za watu maan wao ni kutii tuu

Na kama mnasema siasa ni mapambano basi kuwe na ushindani sawa sio mwingine akizidiwa anatafuta vyombo vya dola na silaha za moto na kutumia mamlaka yake aliyo nayo kukandamiza wengine , huwezi kushindana na mtu anaye jivunia jeshi na silaha za moto wakati wewe mwingine hata jiwe tu hunalo mkononi halafu mnataka wasiache waendelee kuumizwa?

Mnafurahia mnapo ona watanzania wenye itikadi tofauti na ccm wanapo pata majeraha wanapo funguliwa mashtaka kila kipindi cha uchaguzi ,wana vamiwa usiku wa manane na kutekwa, hilo kwenu ni faraja? Kila uchaguzi ccm ni vinara wa vurugu kwa mgongo wa jeshi la polisi, hakuna uchaguzi ambao vuruugu zimetokea ccm hawahusiki

Kama si kucheleweshankumtangaza mshindi basi kuingia na kura bandia kama sio kura bandia kutumia jeshi la polisi kusurubu upinzani,

mnacharanga mapanga wenzenu huku mkiamin jeshi lipo nyuma yenu na hakuna kilicho wahi kutokea kwenu baada ya kukamilisha unyama wenu

Halafu mnataka bado waendelee kushiriki ili watanzania waendelee kupewa vilema , waendelee kuuawa hilo kwenu ni faraja.sababu mna jeshi nyuma linawapa ushindi , ni ushindani gan huo mnao wataka wenzenu waendelee kupambana na risasi za moto na mapanga huku nyie mkisherehekea ushind haramu ? kisa tu siasa ni mapambano wasikate tamaa?

Nadhan kama taifa hatukujiadaa kupokea democrasia nadhan vyama hivi vya upinzani vifutwe tu ili tupunguze yatima wa kisiasa , tupunwguze walemavu kutokana na siasa za chuki nk.
 
Petro E. Mselewa.....nimepitia posts na kuona unaitwa wakili msomi....na hapo ndio nataka kujenga hoja yangu...usomi wenu kwa bahati mbaya sana umekuwa ni wa kwenye vyeti na unakosa kabisa mashiko ya hali halisi ya maisha ya mtaani.
NIPE FAIDA MOJA TU YA KUHUDHURIA NA KUSHIRIKI UCHAGUZI AMBAO UNAJUA KABISA KWA KANUNI NA TARATIBU ZINAZOTUMIKA HAKUNA JINSI UTAVYOSHINDA UCHAGUZI HUO?
Mie naamini kuwa kutoshiriki uchaguzi ni hatua ndogo sana...hatua kubwa iliyotakiwa kuchukuliwa na upinzani nchini NI KUVIFUTA VYAMA VYA UPINZANIA KWA HIARI YAO WENYEWE NA KUJIUNGA NA SISIEMU KUENDELEA KUPONGEZA JUHUDI ZA RAIS NA KUMSHAURI KUOKOA GHARAMA NA PESA ZA UCHAGUZI BASI AWE ANATEUA WABUNGE NA VIONGOZI WOOTE ILI HAYO MABILIONI YA UCHAGUZI YAENDE KWENYE MAENDELEO YA WANANCHI.

Nihitimishe kwa kukutakia KILA LA HERI WAKILI MSOMI na pia nikukumbushe kuwa sisi wananchi wa kawaida TUNATILIA SHAKA HUO USOMI WENU USIOKUWA NA TIJA KWA TAIFA NA HATA KWENU NINYI WENYEWE BINAFSI.
 
Back
Top Bottom