Webabu
JF-Expert Member
- Apr 29, 2010
- 7,149
- 10,854
Waswahili husema mtu ajuwa atokako hajuwi endako.Mwenzenu nina safari ya kwenda mwezini.Uzuri wa safari ni kuaga,na wa mwanzo kuagwa ni nyumbani kwako.Kwa maana hiyo ndio maana nimeamua nianze kuwaageni nyinyi hapa nyumbani.
Baadae nitasafiri kupitia nchi kadhaa za ulaya kuaga ndugu na marafiki.Nitakaa zaidi nchini Uiengereza.Halafu nitaelekea America kwa madhumuni hayo hayo.Huko nitakuwa na shughuli maalum ya maandalizi ya safari kabla kwenda Urusi eneo la Kazakhstan ambako nitakaa kwa muda mfupi.Nikitoka huko nitakuwepo nchi za Ghuba kwa muda kiasi kabla kurudi nyumbani tayari kwa safari.
Nawaombeni ushauri ili kufanikisha safari hii.Nini nichukue na nini niwache.Namna gani nitaweza kushinda upweke kwenye chombo cha usafiri na huko niendako.