MUSIGAJI
JF-Expert Member
- Dec 26, 2014
- 2,187
- 2,460
Wanajukwaa amani iwe nanyi,Leo tarehe 22/8/2018,bila kushurutishwa na yeyote,wala kushawishiwa na yeyote nimeamua kuweka wazi kuwa nimeamua kuushinda wivu wa kipinzani dhidi ya utendaji wa Mh Rais John Pombe Magufuli (JPM).
Ukifuatilia michango yangu yote,Tangu nimejiunga na jukwaa hili nimekuwa mpinzani kwelikweli wa jambo lolote bila kujali linamasilahi kwa Taifa kwa kiwango gani.Nimekuwa na roho ya kipinzani haswaa.Baada ya kujipa muda wa kutafakari nimegundua roho hii ya kipinzani (WIVU) dhidi ya serikali yetu ambayo kimsingi imejitahidi ili Taifa letu lipige hatua si sahii hata kidogo.
Binafsi nimekuwa sijisikii vizuri nilipokuwa ninaona serikali inafanya jambo lolote zuri na hususani sifa zilipokuwa zinaenda kwa serikali kwa kuona kuwa uoinzani hasa CHADEMA itazidiwa sifa.Mfano wa mambo machache mazuri yaliyofanywa na serikali ambayo sikufurahia na ninauhakika wapinzani pia hawakuyafurahia ni haya
I)Ufufuaji wa shirika letu la ndege.Serikali ya awamu ya tano chini ya uongozi wa Mh Rais Magufuli,kwa hakika imejitahidi na imefanya vizuri sana katika kufufua shirika letu la ndege,kwa kufanya hili,serikali imenunua ndege kadhaa ili kuboresha huduma za usafiri wa anga.Ki ukweli ilikua ni aibu sana serikali kutomiliki ndege huku taifa likiwa na Uhuru zaidi ya miaka 50.Sasa kwa sababu ya roho (WIVU) wa kipinzani niliokuwa nayo hakuna siku nilikuwa napata wakati mgumu kama siku za mapokezi ya ndege hizi.Watu nyumbani kwangu waikua wanaangalia kupitia TV na lengo langu nilikuwa sitaki waone mambo hayo lakini dhamira ilikua ikinishitaki sana.
Hongera Mh Raid kwa uthubutu.
II)Uboreshaji wa miundo mbinu.Mh Rais amekuwa akijitahidi sana kuhakikisha anaboresha miundo mbinu,serikali ipo katika hatua za mwisho kukamilisha flyover ya Tazara,Ujenzi wa reli ya kutumia umeme na miundo mbinu mingine. Katika miradi yote hii nilijawa na wivu wa kipinzani sana.Ile flyover tuliibeza ni daraja,lakini ukweli unabaki palepale kwamba litakuwa ni msaada mkubwa kwa wanaotumia barabara ya kutoka gongo la mboto,buguruni,temeke na wanaotoka mjini kupitia barabara ya Nyerere.Nawasihi wapinzani wenye roho ya kipinzani tuunge mkono juhudi hizi,Taifa hili ni letu sote.
iii) Uboreshaji wa Huduma za afya.Serikali katika awamu hii imejitahidi kila Mara kuboresha huduma za afya.Kwa kuongeza upatikanaji wa dawa muhimu,Uboreshaji wa vituo vya afya na hospitali lakini pia kwa kuhakikisha hospital ya Mloganzira inajengwa na kutoa Huduma.Nakumbuka siku ya ufunguzi wa hospital hii nikiwa na roho(wivu wa kipinzani)kama nilivyo na hakika kuwa wapinzani kote nchini walikua na roho hiyo kwa hakika sikujisikia vizuri,hata kidogo tuliponda sana hata hapa jukwaani.Lakini baada ya kutafakari sana nimegundua hii ni hujuma kwa nchi yangu.Nimeamua kumuunga mkono Mh Rais Magufuri katika juhudi hizi.
iv)Kuboresha uchumi wa nchi.Serikali ya awamu ya tano imejidhatiti sana katika kuboresha uchumi.Hatua mbalimbali zimechukuliwa ikiwa ni pamoja na kupitia taratibu mbalimbali za uchimbaji wa madini,ulinzi wa madini ya Tanzanite,udhibiti ya mianya ya upigaji bandarini na mambo kadha wa kadha.
v)Vita dhidi ya rushwa kuimarika.Bila shaka sote ni mashuhuda,zamani rushwa ilikuwa ni kama imealalishwa,lilikuwa ni kama jambo lisilowezekana kupata Huduma katika ofisi za umma bila kitu kidogo.Sasa hivi unapata Huduma kwa haraka na bila kuombwa rushwa.
vi)Uwajibikaji wa viongozi na watumishi wa umma kuimarika.
Ili kuwa ni suala la kawaida kupigwa kalenda na watumishi wa umma,habari njoo wiki au mwezi ujao lilikua jambo la kawaida,Leo hii tunashudia mambo haya yakifutika katika kipindi kifupi tu.
Mwisho,Yapo mengi mazuri ambayo sikuyataja hapa yaliyonigisa na kimsingi yalikuwa yananigusa sema tu nilitawaliwa na roho ya kipinzani ,ambayo Leo yamenifanya niushinde wivu wa kipinzani.Ieleweke Mimi ni mtu huru wala si mwanasiasa (japo nina shahada ya sayansi ya siasa) Nimeandika haya kwa utashi wangu mwenyewe maana dhamira yangu nimekuwa ikinisuta sana,ninapokuwa napinga mambo mema yanayofanyika kwa ajili ya nchi yangu.Niwaombe wapinzani wenye roho za kipinzani (kama nilivyokuwa) ebu tuungane na serikali yetu kwa ajili ya nchi yetu.
Sent using Jamii Forums mobile app
Ukifuatilia michango yangu yote,Tangu nimejiunga na jukwaa hili nimekuwa mpinzani kwelikweli wa jambo lolote bila kujali linamasilahi kwa Taifa kwa kiwango gani.Nimekuwa na roho ya kipinzani haswaa.Baada ya kujipa muda wa kutafakari nimegundua roho hii ya kipinzani (WIVU) dhidi ya serikali yetu ambayo kimsingi imejitahidi ili Taifa letu lipige hatua si sahii hata kidogo.
Binafsi nimekuwa sijisikii vizuri nilipokuwa ninaona serikali inafanya jambo lolote zuri na hususani sifa zilipokuwa zinaenda kwa serikali kwa kuona kuwa uoinzani hasa CHADEMA itazidiwa sifa.Mfano wa mambo machache mazuri yaliyofanywa na serikali ambayo sikufurahia na ninauhakika wapinzani pia hawakuyafurahia ni haya
I)Ufufuaji wa shirika letu la ndege.Serikali ya awamu ya tano chini ya uongozi wa Mh Rais Magufuli,kwa hakika imejitahidi na imefanya vizuri sana katika kufufua shirika letu la ndege,kwa kufanya hili,serikali imenunua ndege kadhaa ili kuboresha huduma za usafiri wa anga.Ki ukweli ilikua ni aibu sana serikali kutomiliki ndege huku taifa likiwa na Uhuru zaidi ya miaka 50.Sasa kwa sababu ya roho (WIVU) wa kipinzani niliokuwa nayo hakuna siku nilikuwa napata wakati mgumu kama siku za mapokezi ya ndege hizi.Watu nyumbani kwangu waikua wanaangalia kupitia TV na lengo langu nilikuwa sitaki waone mambo hayo lakini dhamira ilikua ikinishitaki sana.
Hongera Mh Raid kwa uthubutu.
II)Uboreshaji wa miundo mbinu.Mh Rais amekuwa akijitahidi sana kuhakikisha anaboresha miundo mbinu,serikali ipo katika hatua za mwisho kukamilisha flyover ya Tazara,Ujenzi wa reli ya kutumia umeme na miundo mbinu mingine. Katika miradi yote hii nilijawa na wivu wa kipinzani sana.Ile flyover tuliibeza ni daraja,lakini ukweli unabaki palepale kwamba litakuwa ni msaada mkubwa kwa wanaotumia barabara ya kutoka gongo la mboto,buguruni,temeke na wanaotoka mjini kupitia barabara ya Nyerere.Nawasihi wapinzani wenye roho ya kipinzani tuunge mkono juhudi hizi,Taifa hili ni letu sote.
iii) Uboreshaji wa Huduma za afya.Serikali katika awamu hii imejitahidi kila Mara kuboresha huduma za afya.Kwa kuongeza upatikanaji wa dawa muhimu,Uboreshaji wa vituo vya afya na hospitali lakini pia kwa kuhakikisha hospital ya Mloganzira inajengwa na kutoa Huduma.Nakumbuka siku ya ufunguzi wa hospital hii nikiwa na roho(wivu wa kipinzani)kama nilivyo na hakika kuwa wapinzani kote nchini walikua na roho hiyo kwa hakika sikujisikia vizuri,hata kidogo tuliponda sana hata hapa jukwaani.Lakini baada ya kutafakari sana nimegundua hii ni hujuma kwa nchi yangu.Nimeamua kumuunga mkono Mh Rais Magufuri katika juhudi hizi.
iv)Kuboresha uchumi wa nchi.Serikali ya awamu ya tano imejidhatiti sana katika kuboresha uchumi.Hatua mbalimbali zimechukuliwa ikiwa ni pamoja na kupitia taratibu mbalimbali za uchimbaji wa madini,ulinzi wa madini ya Tanzanite,udhibiti ya mianya ya upigaji bandarini na mambo kadha wa kadha.
v)Vita dhidi ya rushwa kuimarika.Bila shaka sote ni mashuhuda,zamani rushwa ilikuwa ni kama imealalishwa,lilikuwa ni kama jambo lisilowezekana kupata Huduma katika ofisi za umma bila kitu kidogo.Sasa hivi unapata Huduma kwa haraka na bila kuombwa rushwa.
vi)Uwajibikaji wa viongozi na watumishi wa umma kuimarika.
Ili kuwa ni suala la kawaida kupigwa kalenda na watumishi wa umma,habari njoo wiki au mwezi ujao lilikua jambo la kawaida,Leo hii tunashudia mambo haya yakifutika katika kipindi kifupi tu.
Mwisho,Yapo mengi mazuri ambayo sikuyataja hapa yaliyonigisa na kimsingi yalikuwa yananigusa sema tu nilitawaliwa na roho ya kipinzani ,ambayo Leo yamenifanya niushinde wivu wa kipinzani.Ieleweke Mimi ni mtu huru wala si mwanasiasa (japo nina shahada ya sayansi ya siasa) Nimeandika haya kwa utashi wangu mwenyewe maana dhamira yangu nimekuwa ikinisuta sana,ninapokuwa napinga mambo mema yanayofanyika kwa ajili ya nchi yangu.Niwaombe wapinzani wenye roho za kipinzani (kama nilivyokuwa) ebu tuungane na serikali yetu kwa ajili ya nchi yetu.
Sent using Jamii Forums mobile app