Naunga mkono Serikali kutaka Watoto wapumzike wakati wa likizo lakini....

May Day

JF-Expert Member
May 18, 2018
6,162
8,818
Mimi ni miongozi wa Wazazi nisiyefurahishwa kabisa na namna tunavyowachosha Watoto wetu kwa ratiba ngumu wakati mwingine kuliko hata tulizonazo sisi Watu wazima.

Kuhusu likizo nadhani twaweza kuja na namna nyingine ya kwenda na Watoto wetu hawa bila kuendelea kuwaumiza...maana pia kama lengo kuu ni kuwapa Watoto muda wa kukaa na Wazazi tujiulize ni Wazazi wangapi wanapatikana nyumbani zama hizi? sanasana Watoto hawa huishia kushinda tu na kina Dada wa Kazi au Kaka wa kazi.

Au la watashinda kutwa nzima wakiangalia TV hapo kwao au kushinda kwa majirani...au kutumia simu zitakazopatikana kwenye maeneo yao bila Msimamizi...hivyo bila ya shaka shuleni bado kutabaki kama sehemu salama zaidi kwa uangalizi kuliko hata nyumbani.

Kwa kipindi hiki cha likizo Watoto waruhusiwe kwenda hata shule zilizopo jirani na wanapoishi, ila kwa wale ambao bado watamudu kutumia usafiri kuzifikia shule zao ni sawa. Watoto watoke nymbani saa nne na warudi saa tisa. kwangu ni kheri kuliko wakishinda nyumbani siku nzima.

Kwa namna ile ile wanavyolipia tuition Watoto wahudhurie mashuleni na wafundishwe stadi za maisha za kawaida tu zisizowapa stress, mafundisho kama ya kiimani, michezo, kuimba n.k. kabla ya kurudi nyumbani na kushiriki kazi ndogondogo za nyumbani.
 
Ni sahihi kwa unachokizungumzia mzazi mwenzetu,ila kwa waalimu itakuwa ngumu tena kupatikana mashuleni wakati wa likizo kwani walio wengi huenda makwao na wengine ni mikoani kuwatembelea ndugu,jamaa na marafiki zao,ingepaswa waalimu watakaobaki mashuleni wapewe motisha fulani ili wanafunzi waweze kupata hizo stadi za maisha,elimu ya imani zao n.k naungana nawe kwa 100%
 
Tatizo ni Wazazi kukwepa majukumu yao kwenye malezi ya watoto wao. Kwa nini shuleni pawe salama kuliko nyumbani? Jibu ni udhaifu wa wazazi kwenye malezi. Tujirekebishe.
 
Ni sahihi kwa unachokizungumzia mzazi mwenzetu,ila kwa waalimu itakuwa ngumu tena kupatikana mashuleni wakati wa likizo kwani walio wengi huenda makwao na wengine ni mikoani kuwatembelea ndugu,jamaa na marafiki zao,ingepaswa waalimu watakaobaki mashuleni wapewe motisha fulani ili wanafunzi waweze kupata hizo stadi za maisha,elimu ya imani zao n.k naungana nawe kwa 100%
Watumike Walimu wale wale wafundishao tuition..kama wamekuwa wanapatikana kwa kazi hiyo sioni kwa nini kwa hili wasipatikane.
 
Hivi ni kweli mzazi hataki kuona mtoto nyumbani?Jukumu la kumfinyanga mtoto wako unamwachia nani???
Hapo juu si nimeeleza nikihoji kama kweli kuna hao Wazazi Majumbani.

Tofauti itakuwa tu ni Mzazi kuondoka akimuacha Mtoto nyumbani tofauti na siku nyingine ambazo hutoka wote.

Na hiyo saa kumi na mbili au saa mojaMzazi anayorudi si atamkuta tu huyo Mwanaye?.
 
Mimi ni miongozi wa Wazazi nisiyefurahishwa kabisa na namna tunavyowachosha Watoto wetu kwa ratiba ngumu wakati mwingine kuliko hata tulizonazo sisi Watu wazima.

Kuhusu likizo nadhani twaweza kuja na namna nyingine ya kwenda na Watoto wetu hawa bila kuendelea kuwaumiza...maana pia kama lengo kuu ni kuwapa Watoto muda wa kukaa na Wazazi tujiulize ni Wazazi wangapi wanapatikana nyumbani zama hizi? sanasana Watoto hawa huishia kushinda tu na kina Dada wa Kazi au Kaka wa kazi.

Au la watashinda kutwa nzima wakiangalia TV hapo kwao au kushinda kwa majirani...au kutumia simu zitakazopatikana kwenye maeneo yao bila Msimamizi...hivyo bila ya shaka shuleni bado kutabaki kama sehemu salama zaidi kwa uangalizi kuliko hata nyumbani.

Kwa kipindi hiki cha likizo Watoto waruhusiwe kwenda hata shule zilizopo jirani na wanapoishi, ila kwa wale ambao bado watamudu kutumia usafiri kuzifikia shule zao ni sawa. Watoto watoke nymbani saa nne na warudi saa tisa. kwangu ni kheri kuliko wakishinda nyumbani siku nzima.

Kwa namna ile ile wanavyolipia tuition Watoto wahudhurie mashuleni na wafundishwe stadi za maisha za kawaida tu zisizowapa stress, mafundisho kama ya kiimani, michezo, kuimba n.k. kabla ya kurudi nyumbani na kushiriki kazi ndogondogo za nyumbani.
Hata mimi naunga mkono kwa vitendo,marufuku mtoto wangu kwenda tuition,likizo ni mapumziko na kusaidia wazazi Kazi ndogo ndogo na wao kujifunza.

Hii ya kila mda kushinda madarasani watoto wanaishia kuwa mazezeta.
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom