Mag3
Platinum Member
- May 31, 2008
- 13,060
- 22,755
Wakati mwingine tuwe tunatumia akili kidogo, Mohamed Dewji kawashukuru waliomteka kwa kuamua kumuachia usiku wa manane wakati tuliokuwa tukisikitika, tuliokuwa tukiomba, tuliokuwa tukiliaa na tuliokuwa tukipiga makelele tumelala. Mohamed Dewji hana muda wa kuwashukuru binadamu wanyonge kama sisi tulioumbwa kwa udongo.
Sala zetu, vilio vyetu na makelele yetu hayakuweza kufanikisha kupatikana kwa Ben Saanane, Azory na ndugu zetu lukuki waliopotea...iweje kwa Mohamed Dewji? Maombi yetu, masikitiko yetu na vilio vyetu havikuwezesha kupatikana kwa wauaji waliommiminia risasi zisizo na hesabu Mbunge wa Singida Mh. Tundu Antiphas Lissu kwa nia ya kumuua.
Mohamed Dewji hana haja ya kutushukuru wala asithubutu kutushukuru, awashukuru watekaji wenye roho nzuri waliomuonea huruma hadi kapatikana mzima wa afya bila hata kuhitaji uchunguzi wa afya yake, nashauri familia yake iwape hao watekaji zile trilioni kama asante...Kweli Tanzania ni zaidi ya tunavyoijua, pole sana Mohamed Dewji!
Sala zetu, vilio vyetu na makelele yetu hayakuweza kufanikisha kupatikana kwa Ben Saanane, Azory na ndugu zetu lukuki waliopotea...iweje kwa Mohamed Dewji? Maombi yetu, masikitiko yetu na vilio vyetu havikuwezesha kupatikana kwa wauaji waliommiminia risasi zisizo na hesabu Mbunge wa Singida Mh. Tundu Antiphas Lissu kwa nia ya kumuua.
Mohamed Dewji hana haja ya kutushukuru wala asithubutu kutushukuru, awashukuru watekaji wenye roho nzuri waliomuonea huruma hadi kapatikana mzima wa afya bila hata kuhitaji uchunguzi wa afya yake, nashauri familia yake iwape hao watekaji zile trilioni kama asante...Kweli Tanzania ni zaidi ya tunavyoijua, pole sana Mohamed Dewji!