Naunga mkono hoja Madereva DRC wasindikizwe na askari

N'yadikwa

JF-Expert Member
Aug 10, 2014
6,824
9,521
Mhariri wa gazeti la Mwananchi leo Septemba 17 2016 anasema madereva wanaosafiri nchi zenye machafuko kama huko DRC wasindikizwe kwa sababu hali huko si salama, na visa vinavyosimuliwa ni vichache.
  • Anasema madereva wengi wanaosaforosha mizigo kwenda DRC husimulia kuporwa, kupigwa na mizigo wanayosafirisha kuibiwa.
  • Wanasema pamoja na kusafiri kwa misururu bado wanatendewa jinai
  • Haya yanajiri wakati kukiwa na kongamano la kuboresha biashara baina ya nchi ya Tanzania na DRC, sasa suala la usalama kuwa nyuma kama ajenda kiongozi hakutawezesha kukuza biashara.
  • MHARIRI anamalizia kwa kushauri kuwa uwekwe utaratibu kwa serikali ya DRC na Tanzania zikubaliane kuwe na utaratibu wa askari wa DRC kuwasindikiza madereva wetu mara wanapoingiza matairi ya malori yao DRC ili ukuaji wa biashara usizorote.
MIMI NYADIKWA: Namuunga Mkono huyu ndugu mhariri kwa maslahi mapana ya uchumi wa Tanzania na huko DRC. Serikali ya Tanzania liangalieni hili na mlifanyie kazi. OVER. N'yadikwa UR
 
Kazi sio mdogo hiyo ya usindikizaji.
1.Magari yanyokwenda Kongo nimengi naona kama kuna ugumu ,
2.waasi wanapodhamilia hata wangesindikizwa ni bure
3.kiserikali escott ni pesa hiyo,

Kikubwa ni kujengwa reli tu ndio zuruhisho wakongo wanapesa sana
 
Ukizungumzia watekaji huko Kongo unazungumzia WANAJESHI waasi ambao tayari wako vitani, wameshachora ramani ya mapambano ikiwemo utekaji huo, sio majambazi hao mkuu!!
Hilo wazo mimi naona halitakuwa Na tija sana!
 
Mhariri wa gazeti la Mwananchi leo Septemba 17 2016 anasema madereva wanaosafiri nchi zenye machafuko kama huko DRC wasindikizwe kwa sababu hali huko si salama, na visa vinavyosimuliwa ni vichache.
  • Anasema madereva wengi wanaosaforosha mizigo kwenda DRC husimulia kuporwa, kupigwa na mizigo wanayosafirisha kuibiwa.
  • Wanasema pamoja na kusafiri kwa misururu bado wanatendewa jinai
  • Haya yanajiri wakati kukiwa na kongamano la kuboresha biashara baina ya nchi ya Tanzania na DRC, sasa suala la usalama kuwa nyuma kama ajenda kiongozi hakutawezesha kukuza biashara.
  • MHARIRI anamalizia kwa kushauri kuwa uwekwe utaratibu kwa serikali ya DRC na Tanzania zikubaliane kuwe na utaratibu wa askari wa DRC kuwasindikiza madereva wetu mara wanapoingiza matairi ya malori yao DRC ili ukuaji wa biashara usizorote.
MIMI NYADIKWA: Namuunga Mkono huyu ndugu mhariri kwa maslahi mapana ya uchumi wa Tanzania na huko DRC. Serikali ya Tanzania liangalieni hili na mlifanyie kazi. OVER. N'yadikwa UR
Wako busy kulinda ukuta usijengwe
 
Mie nafikiria kwamba Drivers wawe trained tu.
Maana Nchi zenye kuingiza magari kule ni Nchi nyingi sana,almost Nchi zote za Africa Mashariki.

Wangeweka base tu kwenye njia kuu,ambazo ni hatarishi
Wale ni waasi ambao ni dhaifu sana,maana hawavamii na silaha kubwa,maana itakuwa ni hatari kwao na wanajua njia hiyo pia inatumika kijeshi.Na ndio maana wamestukia mchezo wa kuwauwa,maana show ingeyofanywa na Tanzania ingekuwa sio ya kitoto.
Hivi vikundi vya waasi ni miradi ya Nchi za Magharibi
 
Sio akili hii,hoja nyingine kabisa,na usiharibu uzi kwa ujinga wa Siasa.
Yaani unashindwa kujenga hoja kwenye hoja hapo juu?sio kila kitu siasa
hii nchi kila kitu siasa toka lini makada wanakuwa maDED post ambayo very sensitive maendeleo yote yapo halmashauri.
 
story ya kweli kabisa
kumbe madrerva wengi wanalawitiwa na hao waasi,kuna dereva alikuwa na msaidizi wake wanaenda huko congo njiani wakakutana na waasi wakamfanya dereva wakawaachia waende walisema tumfanyie tu dereva.wakati wa kurudi dereva akamwambia aendeshe gari ,walipofika lile eneo tena wakawakuta jamaa wakasema hii gari tulimfumua dereva marinda leo tumfumue msaidizi .dereva aakadakwa akawa anajitetea jamani mimi tayari leo tumebadilishana na mwenzangu akaambiwa sisi hatuwezi kukumbuka maana tumeshapitia madereva wengi .wakamla tena. kwa sasa ameacha kazi maskini
 
Mhariri wa gazeti la Mwananchi leo Septemba 17 2016 anasema madereva wanaosafiri nchi zenye machafuko kama huko DRC wasindikizwe kwa sababu hali huko si salama, na visa vinavyosimuliwa ni vichache.
  • Anasema madereva wengi wanaosaforosha mizigo kwenda DRC husimulia kuporwa, kupigwa na mizigo wanayosafirisha kuibiwa.
  • Wanasema pamoja na kusafiri kwa misururu bado wanatendewa jinai
  • Haya yanajiri wakati kukiwa na kongamano la kuboresha biashara baina ya nchi ya Tanzania na DRC, sasa suala la usalama kuwa nyuma kama ajenda kiongozi hakutawezesha kukuza biashara.
  • MHARIRI anamalizia kwa kushauri kuwa uwekwe utaratibu kwa serikali ya DRC na Tanzania zikubaliane kuwe na utaratibu wa askari wa DRC kuwasindikiza madereva wetu mara wanapoingiza matairi ya malori yao DRC ili ukuaji wa biashara usizorote.
MIMI NYADIKWA: Namuunga Mkono huyu ndugu mhariri kwa maslahi mapana ya uchumi wa Tanzania na huko DRC. Serikali ya Tanzania liangalieni hili na mlifanyie kazi. OVER. N'yadikwa UR

Hiyo kitu unayoomba ndio mbaya kuliko maelezo, hayo Magari yangekuwa na Askari humo ndani, basi tungepokea mabox ya maiti hapa Tanzania
Hao jamaa hata siku moja hawajawahi kuua wanaiwateka kama magari wanayoyateka hayana Askari, ukisia wameua basi walikutana na watu wenye silahaama askari

Mara nyingi hata Askari wakiomba lift kwenye hayo Magari, huwa Makini sana wakisikia risasi tu basi wao ndio wanakuwa wa kwanza kutupa magwanda yao pamoja na bunduki na kukimbilia porini

Naongea kutokana na Experience
 
Hiyo kitu unayoomba ndio mbaya kuliko maelezo, hayo Magari yangekuwa na Askari humo ndani, basi tungepokea mabox ya maiti hapa Tanzania
Hao jamaa hata siku moja hawajawahi kuua wanaiwateka kama magari wanayoyateka hayana Askari, ukisia wameua basi walikutana na watu wenye silahaama askari

Mara nyingi hata Askari wakiomba lift kwenye hayo Magari, huwa Makini sana wakisikia risasi tu basi wao ndio wanakuwa wa kwanza kutupa magwanda yao pamoja na bunduki na kukimbilia porini

Naongea kutokana na Experience
Sasa nini kifanyike kumaliza hujuma hizi mkuu.
 
Sasa nini kifanyike kumaliza hujuma hizi mkuu.
Hakuna cha kufanya hapo kaka, Watu kutekwa hapo hata Watanzania sio mara ya kwanza kwa hilo tukio, hilo tukio limepata kujulikana kwa sababu ya hizo gari kuchomwa moto, otherwise hakuna mtu angejua ingekuwa kama matukio mengine yaliyowahi kutokea, Watanzania washatekwa sana hapo, lakini jamaa wakishajua wewe ni mbongo wala hawana habari na wewe na passport wanakurudishia, au wanaweza kukunyanganyeni mabegi na wakenda nayo milimani kusachi, unaweza shangaa baada ya wiki anakuja mtu sehemu uliyofikia say 50km akiwa na passport yako na anakwambia kabisa nyie wabongo ni ndugu zetu

Hakuna cha kufanya kaka hapo, hapo ni siasa za Congo wenyewe kwa wenyewe na kisha Congo na Rwanda
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom