Naumbuka mchana kweupee! Naomba nisaidieni jamani

mwambunnyara

JF-Expert Member
Sep 25, 2013
518
206
Nakaa na mtoto wa kaka yangu hapa kwangu, ghafla kaniuliza swali, hivi Baba eti kwanini mtoto akizaliwa na miezi Saba anaishi lakini akizaliwa na miezi nane anakufa? Naomba sababu za kisayansi, kwa kuwa sijawahi kufuatilia sababu za jambo hilo, nikamwambia nitakujibu baadaye kidogo, kwa sasa Nina haraka, nikaondoka.

Naombeni mnisaidie wataalamu niondokane na kaaibu kanakoninyemelea.
 
Kipo iko hivi. wakati mtoto akiwa na miezi minane rate ya metabolism inakuwa kubwa sana hivyo akizaliwa mwili wake unashindwa kuhimili
 
Kipo iko hivi. wakati mtoto akiwa na miezi minane rate ya metabolism inakuwa kubwa sana hivyo akizaliwa mwili wake unashindwa kuhimili

Mtihani unabaki kwny maana ya metabolism....ila namshauri a-google atapata majibu unless km ingilishi inapiga chenga
 
Nakaa na mtoto wa kaka yangu hapa kwangu, ghafla kaniuliza swali, hivi Baba eti kwanini mtoto akizaliwa na miezi Saba anaishi lakini akizaliwa na miezi nane anakufa? Naomba sababu za kisayansi, kwa kuwa sijawahi kufuatilia sababu za jambo hilo, nikamwambia nitakujibu baadaye kidogo, kwa sasa Nina haraka, nikaondoka.

Naombeni mnisaidie wataalamu niondokane na kaaibu kanakoninyemelea.
Mwambie kuwa huo ni uongo mkubwa. Si kweli, hakuna sababu ya kisayansi zinazosupport hiyo kitu. Naongea hivyo kama daktari ambae nina uzoefu wa kutibu na kuwahudumia watoto njiti. By any means na kwa experience yangu binafsi njiti wanaozaliwa na miezi nane wana survival rate kubwa kuliko wa miezi saba.
 
Kuna kinga ambayo mtoto miezi saba anakuwa nayo...anapoingia miezi nane kinga hiyo hutoweka na kuanza kujitengeneza tena anapokaribia kuzaliwa..so akizaliwa na miezi saba anazaliwa na kinga hiyo ila miezi nane anakuwa hana hiyo kinga hivo ni rahisi sana kufa....
 
Nakaa na mtoto wa kaka yangu hapa kwangu, ghafla kaniuliza swali, hivi Baba eti kwanini mtoto akizaliwa na miezi Saba anaishi lakini akizaliwa na miezi nane anakufa? Naomba sababu za kisayansi, kwa kuwa sijawahi kufuatilia sababu za jambo hilo, nikamwambia nitakujibu baadaye kidogo, kwa sasa Nina haraka, nikaondoka.

Naombeni mnisaidie wataalamu niondokane na kaaibu kanakoninyemelea.

Je huyo mtoto ni wakike au kiume? Na ana umri gani? Unaweza kutengeneza aina ya jibu kutokana na kategori hizi. Pia muulize yeye kasikia hayo wapi naana kama ni shule ni ngumu kumbadilisha kwa maana watoto wadogo wanaamini sana wanacho sikia kutoka kwa waalim wao.
 
Sababu kubwa za msingi zipo mbili
1.akiwa mwez wa saba metabolism rate inakuwa higher so akizaliwa mwili wake unaweza kusavaivu
2.mwezi wa saba mtoto anakuwa kichwa kinatazama mlango au uke so inakuwa rahis kutoka, mwez wa nane anakuwa kichwa kipo juu
 
Back
Top Bottom