Naulizia Shule nzuri kwa watoto inayofundisha michezo pia

Abuu Kauthar

JF-Expert Member
Jul 10, 2011
3,950
5,692
Habari za jioni Kamarada,

Waswahili tuna msemo wetu "mtoto umleavyo ndivyo akuavyo". Mimi nina kijana wangu ana about 5yrs, nataka nimtafutie shule ambayo inafundisha michezo na elimu nyingine hizi za darasani za kawaida.

Dhumuni langu ni kumuandaa huyu mtoto aje awe mwanamichezo hasa football maana naona danadana anapiga vizuri.

Kwa nini nataka awe mwana michezo, kwa sababu michezo hasa mpira wa miguu unalipa sana kuliko kuvaa tai na kuwa afisa mahala fulani.

Ushauri wenu ni muhimu sana,

Asanteni.
 
Mpeleke alliance schools mwanza,ni shule ya michezo na wanatimu ya wanafunzi ambayo ipo daraja la kwanza kidogo tu iingie ligi kuu ikafanyiwa figisu figisu na mwamuz kwenye mechi yao ya mwisho na singida united,wakafungwa singida ikaingia ligi kuu....!!!!ni shule nzuri sana
 
Mpeleke alliance schools mwanza,ni shule ya michezo na wanatimu ya wanafunzi ambayo ipo daraja la kwanza kidogo tu iingie ligi kuu ikafanyiwa figisu figisu na mwamuz kwenye mechi yao ya mwisho na singida united,wakafungwa singida ikaingia ligi kuu....!!!!ni shule nzuri sana

Sawa mkuu, je inapokea watoto wa umri wa miaka 5?
 
Back
Top Bottom