thebogo055
Member
- Jun 22, 2020
- 19
- 176
Hivi kwanini nyumba za kupanga ambazo wenye nyumba nao wanaishi humo zinakuwa na usumbufu sana. Wenye nyumba wanasumbua kinoma noma yani.
Mfano nyumba ninayokaa nimehamia mwezi wa tano, lakini dah natamani kuhama sema ninmeshalipa miezi sita. Yaani kuna vigharama vya ajab ajabu mpaka najiuliza huyu mzee ana shughul gan na hizi pesa.
Maana nimehamia tu nikaambiwa chemba imejaa wapangaji tujichange 36k tuite gari livute maji taka. Mimi nikagoma kwasababu hata mwezi sina nikasema chemba ikijaa tena nitatoa hii ya sasa sihusiki. Mwenye nyumba akanijia juu kinoma kuwa mimi mkorofi.
Kingine kila tarehe 1 na tar 15 kuna watu wanakuja kusafisha hapo nje kwenye vitofali vya chini sijui wanaviitaje jina lake inabid kila mpangaji achangie elf tatu ili hao mabwana walipwe.
Yaani nyumba hii ina mambo kibao yaani.
Bili ya maji jana imekuja elf 12 kila mmoja achangie na mimi hata sina mazoezi ya maji maana sifui wala kupika kwasababu sio mtu wa kushinda home kazi zangu ni za porini huko, utalii.
Nikirud nakaa week nasepa tena. Nguo huwa napeleka sehem zinafuliwa then nazifuata matumizi yangu ya maji ni kuoga tu na usafi wa ndan basi.
Je, huko kwenu jaman hali ikoje?
Wenye nyumba wenu wana habari gan huko maana dah.
Mfano nyumba ninayokaa nimehamia mwezi wa tano, lakini dah natamani kuhama sema ninmeshalipa miezi sita. Yaani kuna vigharama vya ajab ajabu mpaka najiuliza huyu mzee ana shughul gan na hizi pesa.
Maana nimehamia tu nikaambiwa chemba imejaa wapangaji tujichange 36k tuite gari livute maji taka. Mimi nikagoma kwasababu hata mwezi sina nikasema chemba ikijaa tena nitatoa hii ya sasa sihusiki. Mwenye nyumba akanijia juu kinoma kuwa mimi mkorofi.
Kingine kila tarehe 1 na tar 15 kuna watu wanakuja kusafisha hapo nje kwenye vitofali vya chini sijui wanaviitaje jina lake inabid kila mpangaji achangie elf tatu ili hao mabwana walipwe.
Yaani nyumba hii ina mambo kibao yaani.
Bili ya maji jana imekuja elf 12 kila mmoja achangie na mimi hata sina mazoezi ya maji maana sifui wala kupika kwasababu sio mtu wa kushinda home kazi zangu ni za porini huko, utalii.
Nikirud nakaa week nasepa tena. Nguo huwa napeleka sehem zinafuliwa then nazifuata matumizi yangu ya maji ni kuoga tu na usafi wa ndan basi.
Je, huko kwenu jaman hali ikoje?
Wenye nyumba wenu wana habari gan huko maana dah.