Nauliza kuhusu mahusiano ya wanawake wa Bongo Movie kutoolewa

ryana fan

JF-Expert Member
Apr 27, 2018
2,632
3,051
Habari za asubuhi wana JF?

Baada ya salamu nijikite kwenye mada husika.

Naombeni kuuliza pia kama wahusika wapo humu wanisaidie.

Nimejiuliza maswali mengi sana kuhusu hawa ndugu zangu na si kwa ubaya bali kwa mema tu.

Maswali niliyojiuliza yanahusu maswala ya ndoa na mapenzi ya dhati kati ya hawa mastar wetu wa tanzania au waigiza muvi wa bongo na wasanii wa music.

1. Je, ni kwanini hawa wasanii hususani wa kike hawaolewi? Mfano. Wema sepetu, Irine Uwoya, Jackline Wolper, Blandina chamila, anti ezekiel, Lulu Michael, Diva, Lulu, Hamisa Mobeto, Gigy money, Mdee, Jenifer Odama, yule aliyeigiza na kanumba Dengerous Desire nimemsahau kwa jina na wengine wengi unaweza kuwataja.

2. Je, ni kweli hawa ndiyo wanaosalitiwa katika mapenzi? Na kwanini wao tu ndiyo wasalitiwe? Kila siku wao ndiyo husalitiwa katika mapenzi why?

Nb. Hawa baadhi ya wasanii niliyowataja wanajiita kio cha jamii je, kio chao ni nini kwa jamii kama hawaoneshi mfano wa kuigwa na jamii?

3. Au ukiwa msanii huruhusiwi kuolewa ?

Haya ndiyo maswali yanayoumiza kichwa changu.

Nawasilisha.
 
Pole sana kwa kuumiza kichwa kwa kuyawazia maisha ya wenzio. Sina nia mbaya, ila ningekushauri kubadilika kuanzia sasa na hivyo uanze kuumiza kichwa zaidi kwenye kuyawazia maisha yako! Anza kuwaza unataka uwe mtu wa aina gani baada ya miaka kadhaa, uwe na hela kiasi gani, watoto wako wasome shule gani, uwe na cheo gani kazini/kwenye jamii, nk.

Usijiumize kabisa kichwa chako kuwawazia hao wasanii ambao hawajaolewa! Maana unaweza ukakuta wenyewe wameridhika na hayo maisha waliyojichagulia na huku wakiingiza mkwanja wa kutosha kupitia huo umaarufu wao, lakini wewe mwenzangu ukiendelea tu kutaabika na maisha yako.
 
Maswali mazuri na fikirishi kwa wasanii wetu.

Wapo wachache wanaojua kutofautisha usanii na maisha halisi, nao ni wale ambao wapo na waume zao na wametulia.
Ila hata wa kiumeni ni hali moja tu.
 
Pole sana kwa kuumiza kichwa kwa kuyawazia maisha ya wenzio. Sina nia mbaya, ila ningekushauri kubadilika kuanzia sasa na hivyo uanze kuumiza kichwa zaidi kwenye kuyawazia maisha yako! Anza kuwaza unataka uwe mtu wa aina gani baada ya miaka kadhaa, uwe na hela kiasi gani, watoto wako wasome shule gani, uwe na cheo gani kazini/kwenye jamii, nk.

Usijiumize kabisa kichwa chako kuwawazia hao wasanii ambao hawajaolewa! Maana unaweza ukakuta wenyewe wameridhika na hayo maisha waliyojichagulia na huku wakiingiza mkwanja wa kutosha kupitia huo umaarufu wao, lakini wewe mwenzangu ukiendelea tu kutaabika na maisha yako.

Sawa sawa
 
Ukiowa msanii ni sawa na kuficha embe kwenye mfuko wa shati. Lambda aamue kuacha tu, kazi zao zimekaa kistarehe sana na hivyo huwafanya waingiwe na tamaa. Ukipwa na pesa ya maana oa angalau utamficha vizuri,
 
Uwoya alishaolewa na Janjaro
Aunt ezekiel ashaolewaga na Jack pemba
Lulu ashavalishwa Pete na majizo

Na kwanini hawa hawaoi usihukumu upande mmoja
1;Ray kigosi
2;Dully syks
3;Jay moe
4;TID
5;Joh makini
6;
 
Back
Top Bottom