changu ni changu
Senior Member
- Dec 21, 2013
- 111
- 28
Wana Jamiiforum habarini za asubuhi!!Ndugu zangu nilikuwa naomba ufafanuzi. Mimi niliajiriwa Bukoba na shirika moja la ubelgiji. Katikati ya mkataba wakanihamishia Dar, lakini kabla mkataba haujaisha nikiwa hapa dar wakanipa notice kwamba hawataniongeza mkataba, mkataba wangu umeisha tarehe 30 Septemba. Niliwaomba nauli za kunisafirisha Mimi na vitu vyangu lakini wakakataa, Je kwa mujibu wa sheria ninapaswa nilipwe aje kwa ajili ya safari na je wanapaswa kunilipa posho za kujikimu tangu mkataba wangu ulipoisha mpaka siku ya kusafiri?. Na kisheria posho ni shilingi ngapi kama mshahara wangu ulikuwa 1,100,000/=