Nauli hizi za SGR nani atapanda? Kutoka Dar - Moro Tsh 24,000?

TODAYS

JF-Expert Member
Apr 30, 2014
13,731
21,133
Hata kama ni mapendekezo sidhani kama mlifikiria au kuwaza kwa kinagaubaga, huko Anatorglo mnaenda kupaka mafuta ili kung'arisha hiyo nauli na si vinginevyo.

Ukute mmeshaandaa wazungumzaji wenu wa kutetea hiyo nauli na hapo ndiyo watakuwa wengi ukumbini.

--

Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA) imepokea maombi kutoka Shirika la Reli Tanzania (TRC) kuhusu nauli za abiria kwa treni ya njia ya Reli ya Kisasa – ‘Standard Gauge Railway’ (SGR) zitakavyotumika kwa huduma ya usafiri wa treni za abiria.

Kwa mujibu wa Kifungu Na. 21 cha Sheria Na. 3 ya LATRA, 2019 Mamlaka inapaswa kukusanya maoni ya wadau kabla ya kufikia uamuzi wa kuridhia viwango vya nauli kwa huduma zinazodhibitiwa na Mamlaka ikiwemo nauli za treni.

Katika kulitekeleza hilo, Mamlaka imeandaa mkutano wa kupokea maoni ya wadau wa usafirishaji, ikiwa ni pamoja na watoa huduma, watumiaji wa huduma na wananchi kwa ujumla. Mkutano utafanyika tarehe 19 Disemba 2022 jijini Dar es salaam katika Ukumbi wa Anatorglo.

Nauli zinazopendekezwa na TRC ni Kama ifatavyo:

s1.PNG


s2.PNG


Kutokana na umuhimu wa mkutano huo, LATRA inawaalika wadau wa sekta ya reli na wananchi kwa ujumla kushiriki katika mkutano huo wa kukusanya maoni ya wadau.

Vilevile, wadau wanaweza kuwasilisha maoni yao kwa Mkurugenzi Mkuu kwa maandishi kupitia LATRA Makao Makuu, Mtaa wa Tambuka Reli, Dodoma au ofisi za LATRA zilizopo Makao Makuu ya kila mkoa Tanzania Bara kabla ya tarehe 3 Januari 2023.

Aidha, maoni ya wadau yanaweza kutumwa kwa barua pepe kupitia anuani hizi: info@latra.go.tz na dg@latra.go.tz

Imetolewa na:
Kitengo cha Uhusiano na Mawasiliano – LATRA
06 Disemba, 2022​
 
Hapa au hii ni kutaka kuwaonyesha wananchi kwamba kuendesha huu mradi ni garama kubwa au wananchi kutumia treni ni anasa.

Yaani kwenda Dodoma -60,000/-!.

Treni kwa waliostaarabika huko ni usafiri wa garama nafuu sana sisi unaenda kuonekana ni anasa.
 
View attachment 2440365
Hata kama ni mapendekezo sidhani kama mlifikilia au kuwanza kwa kinagaubaga, huko Anatorglo mnaenda kupaka mafuta ili kung'arisha hiyo nauli na si vinginevyo.

Ukute mmesha andaa wazungumzaji wenu wa kutetea hiyo nauli na hap ndiyo watakuwa wengi ukumbini.
Hizo bei sio kubwa endapo muda utazingatiwa
Maaan kama una haraka n nzur sana sasa hzo naul znafkia za ndege?
 

Hata kama ni mapendekezo sidhani kama mlifikilia au kuwanza kwa kinagaubaga, huko Anatorglo mnaenda kupaka mafuta ili kung'arisha hiyo nauli na si vinginevyo...

Nauli inakwenda na services gani? Je treni inachukua muda gani kwenda Morogoro mpaka Dodoma na maeneo mengine?

Naamini watumiaji watakuwepo kama kuna sababu za kiutendaji na kibiashara
 
View attachment 2440365
Hata kama ni mapendekezo sidhani kama mlifikiria au kuwaza kwa kinagaubaga, huko Anatorglo mnaenda kupaka mafuta ili kung'arisha hiyo nauli na si vinginevyo.

Ukute mmeshaandaa wazungumzaji wenu wa kutetea hiyo nauli na hapo ndiyo watakuwa wengi ukumbini.
Dsm Dodoma naweza kulipa hiyo 59,000 iwapo itatumia saa 1 sawa na ndege vinginevyo hata 35,000 sitoi
 
Back
Top Bottom