Kigarama
JF-Expert Member
- Apr 23, 2007
- 2,492
- 1,230
Katika Tanzania nauogopa na kuuchukia sana ufisadi kuliko ninavyoichukia CCM na Serikali yake. Na kiukweli kabisa chuki yangu kwa CCM ilikuja baada ya kugundua kwamba chama hicho kimeugeuza ufisadi kama ndiyo mfumo wake rasmi wa kuendesha mambo. Lakini ukweli wa mambo unaoonyesha kwa kukaa kwake muda mrefu kwenye madaraka, CCM imeambukiza ufisadi kwa watz wengi sana.
Niliwahi kumsaidia mama mmoja kuhudhuria semina pale Giraffe Hotel. Alipotoka kwenye semina na laki tano zake za posho (Per diem) aling'ang'aniza anipe "asante" hata baada ya kumwambia kwamba kuhudhuria kwake kwenye semina ile kulitokana na yeye kuwa na sifa za kuhudhuria semina na wala si upendeleo kutoka kwangu. Niliikataa asante yake!!
Huo ni mfano mmoja tu wa hali halisi kwenye jamii yetu. Tuna watu wangapi tunaowajua wanatumia vyeti vya kughushi kupata ajira, tumetoa taarifa polisi? Ndugu zetu ambao ni Traffic Police na wanamiliki mali tofauti na mishahara yao tumewahi kuwakemea? Ni wangapi kati yetu tunafanya biashara au kupangisha nyumba bila ya kulipa kodi, huo nao siyo ufisadi?
Kwenye NGOs tunazofanyia kazi tumeghushi risiti ngapi na ni fedha kiasi gani tulizokwapua na kwenda kujengea nyumba au kununulia magari badala kufanya kazi zilizokusudiwa. Ufisadi kama huu ni lazima ufanywe na Lowassa ndiyo tuupige kelele?
Ili kuirekebisha nchi yetu ni lazima tuupige vita ufisadi hata bila ya kujali kama umo CCM, CUF, CHADEMA, msikitini ,kanisani, kwa jirani au ndani ya nyumba zetu. Kwa maana kuna watu humu jamvini wanataka tuamini ufisadi ni matendo mabaya ya wanasiasa peke yao ila matendo hayo hayo yakifanywa na watu wa kawaida tunatafuta sababu za kuyatetea na kuyahalalisha maovu hayo. Ufisadi ni ufisadi tuu hata kama unatendwa na baba yako mzazi au mkweo.
Ufisadi Tanzania umo madarasani, umejaa kwenye mabweni, umejikita kwenye mithani, umeota mzizi kwenye matokeo, haushikiki kwenye usaili, umetamalaki kwenye ajira, upo kwenye mishahara, ndiyo alama ya mafanikio,na ni chanzo cha mbwembwe kwenye maisha yetu ya kila siku mtaani. Kwa hakika UFISADI ndiyo NGUZO ya MAISHA ya kila SIKU kwa WATANZANIA wengi.
Wewe ukifumba macho haimaanishi wenzio wote nao pia hawaoni.
Niliwahi kumsaidia mama mmoja kuhudhuria semina pale Giraffe Hotel. Alipotoka kwenye semina na laki tano zake za posho (Per diem) aling'ang'aniza anipe "asante" hata baada ya kumwambia kwamba kuhudhuria kwake kwenye semina ile kulitokana na yeye kuwa na sifa za kuhudhuria semina na wala si upendeleo kutoka kwangu. Niliikataa asante yake!!
Huo ni mfano mmoja tu wa hali halisi kwenye jamii yetu. Tuna watu wangapi tunaowajua wanatumia vyeti vya kughushi kupata ajira, tumetoa taarifa polisi? Ndugu zetu ambao ni Traffic Police na wanamiliki mali tofauti na mishahara yao tumewahi kuwakemea? Ni wangapi kati yetu tunafanya biashara au kupangisha nyumba bila ya kulipa kodi, huo nao siyo ufisadi?
Kwenye NGOs tunazofanyia kazi tumeghushi risiti ngapi na ni fedha kiasi gani tulizokwapua na kwenda kujengea nyumba au kununulia magari badala kufanya kazi zilizokusudiwa. Ufisadi kama huu ni lazima ufanywe na Lowassa ndiyo tuupige kelele?
Ili kuirekebisha nchi yetu ni lazima tuupige vita ufisadi hata bila ya kujali kama umo CCM, CUF, CHADEMA, msikitini ,kanisani, kwa jirani au ndani ya nyumba zetu. Kwa maana kuna watu humu jamvini wanataka tuamini ufisadi ni matendo mabaya ya wanasiasa peke yao ila matendo hayo hayo yakifanywa na watu wa kawaida tunatafuta sababu za kuyatetea na kuyahalalisha maovu hayo. Ufisadi ni ufisadi tuu hata kama unatendwa na baba yako mzazi au mkweo.
Ufisadi Tanzania umo madarasani, umejaa kwenye mabweni, umejikita kwenye mithani, umeota mzizi kwenye matokeo, haushikiki kwenye usaili, umetamalaki kwenye ajira, upo kwenye mishahara, ndiyo alama ya mafanikio,na ni chanzo cha mbwembwe kwenye maisha yetu ya kila siku mtaani. Kwa hakika UFISADI ndiyo NGUZO ya MAISHA ya kila SIKU kwa WATANZANIA wengi.
Wewe ukifumba macho haimaanishi wenzio wote nao pia hawaoni.