Natokwa na makohozi na mate ya utelezo mara kwa mara. Nini chanzo na tiba yake?

Lizaboni

JF-Expert Member
Feb 21, 2013
33,894
20,372
Wadau, kwa muda mrefu nimekuwa nikisumbukiwa na tatizo la kutokwa na makohozi na mate ya utelezi. Tatizo hilo limedumu kwa muda wa miaka 3. Nimeenda hospitali kadhaa lakini sijapata matibabu ya kumaliza tatizo hilo. Kuna daktari mmoja alinieleza kuwa ugonjwa huo unatibika kwa dawa za asili na unajulikana kama Ndimi Mbili. Sina hakika kama jina hilo ni la kitaalam au ni majina yetu ya uswahilini.

Naamini kuwa JF ina watu wanaojua mambo mengi na ninaamini kuwa hata tatizo hili wanalifahamu na wanafahamu tuba yake. Mwenye uelewa mpana juu ya ugonjwa huu atuwekee maelezo ya kutosha na ni vema pia akaainisha na tiba ili isaidie na wengine wanaoteseka pasi na mafanikio

Ahsante

CC. ZEMARCOPOLO
 
Wadau, amani iwe nanyi!!!!

Mdogo wangu anatatizo la kutoa makohozi kutoka kwenye koo lake! amekua akilalamika kua njia ya koo yaani kwenye kuta za koo huwa makohozi yanakua yamegandiana. Hivyo hulazimika kutoa makohozi mara kwa mara. Makohozi haya huwa mazito sana, na wakati mwingne anasema kuwa huwa mazito sana kama vijinyama nyama.

Msaada jamani, atumie DAWA gani? Anasema hali hiyo humkera sana.
 
Nami nilikuwa na hilo tatizo Ila nilikuja kupona kama bado analo aende pale mwembe chai kuna hospitali inaitwa ekenywa atapona Mimi nilihangaika sana mwisho nikaponea hapo
 
Dawa yake ndogo sana aache kujipendekeza na kutumiwa km pulizo la kiume na Ccm na aache matusi kwa wazee wa upinzani bila hivyo huponi kabisa
 
Leo naona mmembamba Lizaboni lazima aufute huu uzi au audit na kusema kuna rafiki yangu ameniomba nimuandikie humu jf kama anaweza pata msaada...

Jamaa Cheche kweli kumbe anatype huku anarusha makohozi kwenye keyboard it means kila mwezi ananunua new keyboard.. Ila Tusicheke Magonjwa.. Mkuu Lizaboni ushapona makohozi?

Dawa uwe unasukutua na maji chumvi kila asubuhi usiyameze ila kichwa unakuwa unatizama juu kila siku hadi upone ila ndio uache kula vitu vya baridi kama lamba lamba za Azam na local na pia Usinywe kabisa Gongo
 
Leo naona mmembamba Lizaboni lazima aufute huu uzi au audit na kusema kuna rafiki yangu ameniomba nimuandikie humu jf kama anaweza pata msaada...

Jamaa Cheche kweli kumbe anatype huku anarusha makohozi kwenye keyboard it means kila mwezi ananunua new keyboard.. Ila Tusicheke Magonjwa.. Mkuu Lizaboni ushapona makohozi? Dawa uwe unasukutua na maji chumvi kila asubuhi usiyameze ila kichwa unakuwa unatizama juu kila siku hadi upone ila ndio uache kula vitu vya baridi kama lamba lamba za Azam na local na pia Usinywe kabisa Gongo
Duh. Ushauri wa masemango huu
 
Dawa yake ndogo sana aache kujipendekeza na kutumiwa km pulizo la kiume na Ccm na aache matusi kwa wazee wa upinzani bila hivyo huponi kabisa
Mkuu, usilete siasa kwenye masuala ya msingi. Hapa tunazungumzia afya na si siasa
 
Nami nilikuwa na hilo tatizo Ila nilikuja kupona kama bado analo aende pale mwembe chai kuna hospitali inaitwa ekenywa atapona Mimi nilihangaika sana mwisho nikaponea hapo
Dawa ipi walikupa?
Hivi madokta hawapo humu kutusaidia?
 
Back
Top Bottom