NATO wanatishia, Urusi hatishii atavamia kweli na inaweza kutokea Vita kweli

lee Vladimir cleef

JF-Expert Member
Feb 5, 2013
9,147
33,302
Mgogoro Kati ya Ukraine upo kweli na Vita kubwa sana yaweza Kutokea baina ya Urusi na Ukraine wakisaidiwa na NATO.

Chokochoko hapo ni Marekani tu ndio ambae anampa kiburi na kumdanganya Ukraine.

Nia ovu ya Marekani Ni kuwa na wanachama wengi wa NATO walio karibu na Urusi na hasa wale walikua wasoviet walionitenga. Lengo kuu Ni kumzunguka Urusi.

NATO wanatishia kumuonya Urusi asijaribu kuingia/kuvamia Ukraine. Wanaonya kuwa Urusi akiingiza majeshi Ukraine atakiona.
Hapa wanatishia tu.hakuna watakachokifanya Kama Urusi akiamua kuingiza,na hajaamua. Zaidi watakachokifanya Ni kujaribu kumpa silaha Ukraine,na ambazo zinaweza kuishia mikononi mwa Urusi.

Kwa Nini nasema NATO wanatishia tuu,Ni kwa sababu Ukraine sio mwanachama wa NATO,na NATO akiingiza jeshi lake hata kwa kurusha risasi moja tu kuelekea Urusi basi hiyo itakua Vita kamili,amabapo Urusi itatoa jibu kamili kabisa kwa NATO,au kwa lugha nyingine Risasi hiyo itajibiwa kikamilifu na Urusi.

Sasa hapo kitakachochotokea Ni Vita kamaili. Na Vita Kati ya Urusi na NATO itakua sio viita ya Risasi na Bunduki,Wala ndege,Bali Vita vya Makombora. Wote tunajua Hawa mahasimu wawili yaani Urusi na NATO uwezo wao kwenye Makombora.

Je, Ni Nani Yuko tayari kwa upande wa NATO kukubali Makombora mapya na ya zamani ya Urusi yatue kwenye nchi zao kwa ajili ya Ukraine ambae hata sio mwanachama wa NATO?

Tena kwa mgogoro amabo hata yeye Ukraine Ana ukorofi wake?

Urusi hatishii, atavamia kweli na hakuna wa kumfanya kitu.

Katika mgogoro wa Ukraine na Urusi Ni Ukraine na Urusi kweli ndio Zina maslahi sio NATO,NATO lengo la Ni kujitanua tu.

Ukraine yeye anataka kujiunga na Magharibi kweli lakini ndani yake Kuna majimbo yanataka kuwa upande wa Msahariki (Urusi).
Haya majimbo yakijitenga Ukraine inabaki Nusu,hivyo haiko tayari kwa Hilo.

Urusi in Maslahi makubwa kuliko NATO na hata Ukraine,Urusi bado inaipenda Ukraine,lakini Ukraine haiipendi Urusi. Urusi inaogopa Ukraine ikijiunga na NATO kwa sababu NATO itakua kubwa Sana na itakua mlangoni pa Urusi.

Ukraine inawapiga waasi amabao Ni Warusi wa asili. Ukraine ikijiunga na NATO Crimea inaweza kuchukuliwa Tena na Ukraine kwa msaada wa NATO. Hizo Ni sababu chache tu za kwangu kuonesha jinsi Urusi ilivyo na maslahi makubwa na Ukraine.

Kwa maslahi hayo ndio maana nasema Urusi hatishii atavamia kweli na hajali matokeo yoyote Yale tofauti na nchi Kama Ufaransa Ujerumani Italy na wanachama wengine wa NATO labda kidogo Marekani atajitutumua kuonesha Yuko pamoja na Ukraine, lakini ki ukweli wale NATO hawana maslahi makubwa kwao zaidi ya kutanua huo umoja ambao Marekani ndio anafaidika zaidi.

Kwa Ni I Naamini Kuwa Urusi hatishii na atavamia kweli.

Urusi aliwahi kuivamia Georgia kwa ujinga Kama huu wa Georgia kuwapiga waasi wanaotaka kujitenga wa Southern Ossetia na Abkhazia. Urusi alikuja juu na kushusha kipigo kwa Georgia na NATO wakibaki kupiga kelele bila kufanya chochote ingawa walikua wakimpa kiburi Georgia.

Urusi ilikwenda mbali zaidi kwa kumpinga Georgia Hadi ndani na Urusi kuyapa Uhuru majimbo hayo mawili ya Southern Ossetia na Abkhazia kibabe tu. NATO walipiga kelele na UN walipiga kelele Urusi walitia pamba masikioni.

Baada ya mgogoro wa Ukraine kuanza kipindi kile kupelekea Rais aliekuwepo Ukraine wakati ule kupinduliwa na kukimbilia Urusi,baada ya Majimbo ya Luhansk na Donesk kutaka kujitenga Urusi iliingia Ukraine kiana na kujitwalia Jimbo la Crimea iliyokua sehemu ya Ukraine NATO na UN waliishia kupiga kelele huku wakiwa Kama watazamaji wa nyumba inayoungua bila msaada.Urusi hapa hakutishia alifanya kweli.

Mgogoro wa Waasi wa Syria waliokua wakiungwa mkono na Marekani Uingereza,Ufaranza,Uturuki,baadhi ya nchi za Ulaya, Sehemu kubwa ya Waarabu na Israel ili kumtoa Assad.

Urusi peke yake ilipinga Assad kuondolewa na kwa jeuri kabisa katikati ya hao wote ikapeleka majeshi yake na kupigana na yoyote aliekua anataka kumtoa Assad na hatimae leo Assad yupo madarakani zaidi ya miaka nane.

Urusi Tena ikapeleka vifaa vya kijeshi nchini Venezuela kumuunga mkono Raisi Nikolas Maduro ambae Marekani Uingereza na nchi nyingi za Amerika ya KUSINI kufanya kila hila kutaka Maduro aondoke madarakani kisiasa ama kijeshi.Urusi alipeleka vifaa vya kijeshi na wataalamu wa kijeshi nchini Venezuela kumlinda Maduro na Hadi leo yupo miaka kadhaa Sasa. Hii ya Venezuela sio maslahi muhimu Sana kwa Urusi ila kuweka heshima tu.

Kwa Urusi kule Ukraine Ana maslahi makubwa ya muhimu na ya kweli kabisa. Hivyo nchi yoyote duniani huwa inaingia vitani kupigania maslahi yake.

Urusi hapa iko tayari kupigana Vita kabisa na haijali matokeo ya Vita Bali maslahi kwanza. Lakini NATO hasa wa upande wa Ulaya Hawa hata Vita ikianza wao hawoni umuhimu wa Vita. Kwa hiyo NATO wanatishia tu lakini Urusi Hatishii Bali ataingia kweli Kama akiona ujinga unaendelea. Nimeonesha mifano hapo juu ya Georgia, Crimea, na Syria. Urusi hakutishia Bali aliingiza majeshi kweli na Hali halisi tumeiona. Kama mnadhani utani subirini mtaona Kama Urusi ataogopa kuivamia Uraine.
 
Hivi unafikiri Nani hapa Ulaya Yuko tayari kuingia vitani na URUSI kwa ajili ya Ukraine? Kwa sababu zipi hasa?

Kwanza sio mwanachama wa NATO

Pili sioni sababu za NATO kuruhusu kuingiza majeshi yake uwanjani kutokana na mkataba wa Kuanzishwa umoja wa NATO.

Namaana sababu za NATO kuingia vitani Ni zile zilizokubaliwa wakati wanaanzisha umoja?
 
Wewe tangu lini umekuwa msemaji wa nchi za Ulaya Mkuu!?
Hivi unafikiri Nani hapa Ulaya Yuko tayari kuingia vitani na URUSI kwa ajili ya Ukraine? Kwa sababu zipi hasa?
Kwanza sio mwanachama wa NATO

Pili sioni sababu za NATO kuruhusu kuingiza majeshi yake uwanjani kutokana na mkataba wa Kuanzishwa umoja wa NATO.
Namaana sababu za NATO kuingia vitani Ni zile zilizokubaliwa wakati wanaanzisha umoja?
 
Jamaa umeandka kshabk sana as if we ndo putin yan unaamin urusi hatishii ila nato ndo wanatishia sjui we ni kiongoz wa urus au wa nato.

Kuhusu makombora unadhan urus ye haogopi makombora ya nato au hayana madhara naona unaizungumzia nato as if unaizungumzia ukraine.

Unaleta reference ya georgia kwan uko nato walsema watapeleka jesh kama wanavyosema sasa.

Nashangaa unaona ni sahihi urusi kutaka kuigawa ukraine kwa maslahi yake wkt lile n taifa huru linajchagulia rafk wamtakaye umeonyesha ushabk kupta maelezo kuongea krusi kwa hayo majmbo si sbb ya urus kutaka chukua ardhi ya taifa lingne hao waongea krus si wahamie urus huko kwan lazma wawe kwny ardhi ya ukraine.

Unasema ukraine anadanganywa na marekan lakn hujasema hao waongea krus nao wanadanganywa na urusi.

Unasema ukraine ana maslahi makubwa na ukraine huku uksema nato hana maslah na ukraine cha ajabu unashndwa kuwa muwaz tu maslah ya urus kwa ukraine ni usalama lakn pia unashndwa kuwa mkwel maslah ya nato pia kwa ukraine n usalama na si kwel urus na nato wanaipenda ukraine hapana hapo n maslah yao tu ya kiusalama.

Karibu unikosoe na uache ushabk mkuu ukraine n taifa huru lischaguliwe rafk na urus kwaiyo leo kenya waichukue shrati kule kwa wajaluo wadai wanawalinda wajalauo sbb kenya wanaongea kjalauo waweke na jesh mpakan eti watshie kuvamia we utafkria nn hapo mkuu?

Asante
 
Jamaa umeandka kshabk sana as if we ndo putin yan unaamin urusi hatishii ila nato ndo wanatishia sjui we ni kiongoz wa urus au wa nato.

Kuhusu makombora unadhan urus ye haogopi makombora ya nato au hayana madhara naona unaizungumzia nato as if unaizungumzia ukraine.

Unaleta reference ya georgia kwan uko nato walsema watapeleka jesh kama wanavyosema sasa.

Nashangaa unaona ni sahihi urusi kutaka kuigawa ukraine kwa maslahi yake wkt lile n taifa huru linajchagulia rafk wamtakaye umeonyesha ushabk kupta maelezo kuongea krusi kwa hayo majmbo si sbb ya urus kutaka chukua ardhi ya taifa lingne hao waongea krus si wahamie urus huko kwan lazma wawe kwny ardhi ya ukraine.

Unasema ukraine anadanganywa na marekan lakn hujasema hao waongea krus nao wanadanganywa na urusi.

Unasema ukraine ana maslahi makubwa na ukraine huku uksema nato hana maslah na ukraine cha ajabu unashndwa kuwa muwaz tu maslah ya urus kwa ukraine ni usalama lakn pia unashndwa kuwa mkwel maslah ya nato pia kwa ukraine n usalama na si kwel urus na nato wanaipenda ukraine hapana hapo n maslah yao tu ya kiusalama.

Karibu unikosoe na uache ushabk mkuu ukraine n taifa huru lischaguliwe rafk na urus kwaiyo leo kenya waichukue shrati kule kwa wajaluo wadai wanawalinda wajalauo sbb kenya wanaongea kjalauo waweke na jesh mpakan eti watshie kuvamia we utafkria nn hapo mkuu?

Asante
Kwa kifupi wewe na huyo mtoa mada ni waandishi wakishabiki ila mnatofautiana upande wa kushabikia
 
Kwa kifupi wewe na huyo mtoa mada ni waandishi wakishabiki ila mnatofautiana upande wa kushabikia
Wewe usiye mshabk hebu toa maoni yako.

Kwa kfupi hata wewe ni mshabk wa urus ndo maana umekmbilia kujbu kuptia nlchoandka ukzngatia umeweka pcha ya putin hapo naiona unadhan mwny ufahamu atashndwa kujua we ni mshbk wa upande upi. Labda mwendawazmu.
 
Hivi unafikiri Nani hapa Ulaya Yuko tayari kuingia vitani na URUSI kwa ajili ya Ukraine? Kwa sababu zipi hasa?
Kwanza sio mwanachama wa NATO

Pili sioni sababu za NATO kuruhusu kuingiza majeshi yake uwanjani kutokana na mkataba wa Kuanzishwa umoja wa NATO.
Namaana sababu za NATO kuingia vitani Ni zile zilizokubaliwa wakati wanaanzisha umoja?
Anachofanya Urusi hata Hitler alianza hivyo hivyo,mwishoe akajitanua na kuota mapembe. Kama hujui kuwa Ulaya wanalichukulia hili jambo seriously subiri uone moto wake. Nchi kama Poland, Romania,Norway na Sweden wanalichukulia kwa uzito mkubwa sana.
 
Anachofanya Urusi hata Hitler alianza hivyo hivyo,mwishoe akajitanua na kuota mapembe. Kama hujui kuwa Ulaya wanalichukulia hili jambo seriously subiri uone moto wake. Nchi kama Poland, Romania,Norway na Sweden wanalichukulia kwa uzito mkubwa sana.
Mrusi anachofanya hasa ni kujihami. Hao NATO wanataka wasogee mlangoni kwake kabisa kitu ambacho mrusi hakubaliani nacho
 
Watakupinga ila muda utaongea! Safari hii kama Ukraine haibebwi yote basi majimbo yake yatabebwa kiulaini kabisa huku wanaompa kiburi wakipigana vita ya maneno.
Vita vya kuchambana anaviweza USA sana na ndiko alikobaki
USA kwa wababe wenzake anaishiaga kubwekabweka na kukimbilia vikwazo, ila akikuta mlevi wa mataputapu anajipigia muda wowote anaoamua.
 
Wewe tangu lini umekuwa msemaji wa nchi za Ulaya Mkuu!?
Hamna Mkuu ni mazungumzo tu Kama tunavyozungumzaga kwa undani mechi za Akina Man U na Liverpool, au akina Barcelona na Akina Real Madrid au Akina Buyen Minich na Akina Buyer Liverkusen au Akina AC Milan na Inter Milan.

Si unajua Marekani akikohoa huku tunapata mafua?
 
USA anapigana vita vya akili. Soma Historia ya vita vya 1 na 2 vya dunia. Kipindi wao wapo vitani Marekani kajifungia ndani. Wanaume wapo vitani, matokeo yake ndiyo haya USA anawawekea vikwazo

Vita vya ubabe, kujiona ww una nguvu sana kuliko wengine. Wamebaki wajinga ndiyo wanapigana. Yeye akiona sehemu kuna mali ndiyo anapigana maana atapata faida.

Wala siyo kuchambana, USA akili kubwa. Sasa hivi Libya ameshanyonya mafuta tayari.

Apigane na China, Urusi au Korea kaskazini atachukua nn? Ni bonge la hasara.

Angalia wanaojifanya wanajua vita, miji yao imebaki magofu. Warabu hawana akili kbsa. Ni wajinga kiwango cha PHD

Watakupinga ila muda utaongea! Safari hii kama Ukraine haibebwi yote basi majimbo yake yatabebwa kiulaini kabisa huku wanaompa kiburi wakipigana vita ya maneno.
Vita vya kuchambana anaviweza USA sana na ndiko alikobaki
 
Back
Top Bottom