Natarajia kuiona Tanzania aliyoiacha Mwalimu Julius Nyerere inarudi tena

Chagu wa Malunde

JF-Expert Member
Jul 11, 2015
8,708
5,711
Kwa tuliobahatika kuushudia utawala wa mwl JKN ni wazi kabisa kuwa ni mashuhuda kuwa tuliishi maisha yasiyo na stress

Kuanzia shule ya msingi mpaka Chuo Kikuu ilikuwa ni bure, huduma za afya bure. Kulikuwa hakuna matabaka maana hakuna cha mtoto wa kigogo au kibopa kusoma shule tofauti na watanzania wenzako, kwa ujumla maisha yalikuwa ya raha. Tuachilie mbali setbacks zilizoukumba utawala wa Mwl JKN kwa ujumla alijitahidi sana

Lakini hii ni kwa sababu utawala wa mwl ulitumia vizuri mapato ya serikali ndio maana aliweza kuhakikisha huduma za jamii kama elimu, afya, zinamfikia kila mtanzania.

Kitendo cha serikali ya awamu ya tano kukusanya tril 2 huku matumizi ni tril 1.8+ ni ushahidi tosha kuwa sasa tunaweza kurudi kule alipotuacha Mwl JKN.

Ni wazi kuwa tutaweza kulipia huduma za msingi kama afya na elimu bure kwa watanzania wote. Tunaweza kuanza na elimu bure mpaka kidato cha sita, pia huduma za afya ziwe bure kwa wananchi wote.

Kisingizio kuwa pato la taifa ni dogo na hivyo cost sharing kwenye afya na elimu iwepo hakipo. Hivyo huu ndio wakati wa kuirudisha Tanzania aliyotuachia Mwl JKN.
 
Maisha ni vita! Wanaojua hilo ndio huishi kifalme duniani

Usipofanya vita kupigania maisha, hata kile chako utanyang'anywa Kwa wanaoelewa kuwa maisha ni vita

Kiongozi yoyote anaeendekeza kucheka na waliokalili huo msemo Kodi zote wataingiza mifukoni mwao na bado watamwambia hicho kiti alichokalia hakimfai

Usawa kwenye Kodi na kodi Rafiki, hiyo tr2. Ni kidogo Sana!

Tz inawatu zaidi ya m60, inatakiwa iwe na walipa Kodi nusu ya hao, hata wakiwa wanalipa 1,5000/ Kwa mwezi unaona kabisa Kwa haraka zinachungulia hapo tr 4.5
 
Kwahiyo unaamini tumekusanya 2t? Nyerere alituachia Tanzania yenye neema? Wakati amelazimika kutoka madarakani tulikuwa tunavaa viraka. Sema Tanzania iliyowahi wakati fulani kuwa na neema kipindi cha Nyerere.

Yeye alituachia nchi uchumi ukiwa umekufa ndio maana akatoka. Hakutoka kwa kupenda, bali baada ya uchumi kuharibika akawa hana jinsi.

Sema turudi kwenye nchi ya chama kimoja aliyotuachia Nyerere, ambapo wananchi wote wanashurutushwa kumsujudia rais, ambayo ndio hali tuliyonayo sasa.
 
Kwahiyo unaamini tumekusanya 2t? Nyerere alituachia Tanzania yenye neema? Wakati amelazimika kutoka madarakani tulikuwa tunavaa viraka. Sema Tanzania iliyowahi wakati fulani kuwa na neema kipindi cha Nyerere. Yeye alituachia nchi uchumi ukiwa umekufa ndio maana akatoka. Hakutoka kwa kupenda, bali baada ya uchumi kuharibika akawa hana jinsi. Sema turudi kwenye nchi ya chama kimoja aliyotuachia Nyerere, ambapo wananchi wote wanashurutushwa kumsujudia rais, ambayo ndio hali tuliyonayo sasa.
Kwa nini nisiamini juu ya tril 2? Mamlaka husika ndio imetoa taarifa, unataka nimuamini nani?

Nyerere hakupenda kuiacha nchi ikiwa na uchumi kama ule ndio maana nimeandika alijitahidi,vita vya Kagera na fitina za mabeberu zilimuangusha.

Ukweli utabaki wazi kuwa alijitahidi kudhibiti matumizi ya mapato na kutoa huduma za kijamii bure,jambo ambalo hata sasa linawezekana. Habari za kusurutisha watu ili rais aabudiwe sio kweli.
 
Unajilisha upepo bure! Hiyo Dunia ya Mwl.Nyerere haipo na hata Mwl.Nyerere angefufuka leo basi angeshangaa namna elimu mliyopata katika karne ya 21 imeshindwa kuwakomboa Watanzania kama wewe.
" when income rises, expenditure also tend to rise to meet that income"!

Watanzania tunatakiwa tutoke ndani ya box na tuache kabisa kufikiria kwamba Serikali itatufanyia kila kitu! Hii ndiyo nguzo ya umasikini wetu.

Tupambane kuhakikisha kuwa mazingira yanajengwa mazuri kila mtu ajenge uchumi wa Nchi na wake binafsi.

Hivi vitawezekana kupitia " the rule of law" and "democracy" where minority are listened to and not eliminated and majority are left to decide.
 
Unajilisha upepo bure! Hiyo Dunia ya Mwl.Nyerere haipo na hata Mwl.Nyerere angefufuka leo basi angeshangaa namna elimu mliyopata katika karne ya 21 imeshindwa kuwakomboa Watanzania kama wewe....
When income rises expenditure also rises. Kwani kuna tatizo kwa sasa kukusanya tri 2huku expenditure ni 1.8 tril? Huoni kuwa income ni kubwa kuliko expenditure? Au umekurupuka kamanda.
 
" when income rises, expenditure also tend to rise to meet that income"!
It's dependent on what your priorities are. Kama tumeamua kuwekeza kwenye kuwajengea mahekalu viongozi wastaafu, kuwalipa posho za vikao na pesa ya kununua magari ya kifahari wabunge nk, ni dhahiri huduma zingine muhimu kwa mwananchi zitakosekana.
 
Wewe ndo unakurupuka na analysis za kitoto.

Hivi mtu ukiwa na Tshs.2,000/= na ukaamua kula ugali dagaa kwa Tshs.1,500/=, maji ya kiroba 300/= basi utajitapa kuwa wewe una mafanikio makubwa kwa kuwa pesa yako haijaisha na umebakiza Tshs.200/=?

Ebu jaribu kuagiza pilau ya Tshs.3,000/= na Maji ya kunywa (Kilimanjaro) Tshs.1,000/= ili ujue umaskini wako!

Hizo Trilioni 2 ambazo unataka "wajinga" washangilie zimekusanywa at the expense of kuuwa biashara za watu, ku- freeze accounts na wakati huo huo hakuna malipo ya wastaafu kwa miezi kadhaa,hakuna nyongeza za mishahara kwa watumishi na mengineyo mengi!
 
Kwa tuliobahatika kuushudia utawala wa mwl JKN ni wazi kabisa kuwa ni mashuhuda kuwa tuliishi maisha yasiyo na stress...
Hivi huwa mnawaza vitu gani jamaaniii? Yaani unaitaka Tanzania ya kipindi hicho?? Unafaham mahangaiko yaliyokuwepo hususani kwenye huduma za jamii kama vile elimu, afya miundombinu mibovu n.k? Yaani unataka turudie kipindi cha kuwa na secondary moja mkoa mzima? Hospitali moja mkoa mzima au barabara ya rami dar tuu pekeakeee?

Hivi unadhani mwl.yeeye hakupenda kuona Tanzania iliyosheheni vituo vya afya na secondary kila kata? Unafikiri mwl yeye hakupenda kuona Tanzania ya barabara za juu na barabara za rami Tanzania nzima kama ilivyo kwa sasaa?? Unafikiri mwl yeye hakutamani kuona wasomi na wabobezi wahitimu vya vyuo vikuuu kama ilivyo kwa sasaa??
 
Hivi huwa mnawaza vitu gani jamaaniii?? Yaani unaitaka Tanzania ya kipindi hicho?? Unafaham mahangaiko yaliyokuwepo hususani kwenye huduma za jamii kama vile elimu, afya miundombinu mibovu n.k? Yaani unataka turudie kipindi cha kuwa na secondary moja mkoa mzima? Hospitali moja mkoa mzima au barabara ya rami dar tuu pekeakeee?? Hivi unadhani mwl.yeeye hakupenda kuona Tanzania iliyosheheni vituo vya afya na secondary kila kata? Unafikiri mwl yeye hakupenda kuona Tanzania ya barabara za juu na barabara za rami Tanzania nzima kama ilivyo kwa sasaa?? Unafikiri mwl yeye hakutamani kuona wasomi na wabobezi wahitimu vya vyuo vikuuu kama ilivyo kwa sasaa??
Soma vizuri na uelewe kabla ya kuropoka
 
Wewe ndo unakurupuka na analysis za kitoto.
Hivi mtu ukiwa na Tshs.2,000/= na ukaamua kula ugali dagaa kwa Tshs.1,500/=, maji ya kiroba 300/= basi utajitapa kuwa wewe una mafanikio makubwa kwa kuwa pesa yako haijaisha na umebakiza Tshs.200/=?
Ebu jaribu kuagiza pilau ya Tshs.3,000/= na Maji ya kunywa (Kilimanjaro) Tshs.1,000/= ili ujue umaskini wako!
Hizo Trilioni 2 ambazo unataka "wajinga" washangilie zimekusanywa at the expense of kuuwa biashara za watu, ku- freeze accounts na wakati huo huo hakuna malipo ya wastaafu kwa miezi kadhaa,hakuna nyongeza za mishahara kwa watumishi na mengineyo mengi!
Daah hi nimeilewa kumbe ukitaka kujua umaskini wako kwaiyo Kama unash 5000 inatakiwa utamani kitu Cha 7000 ndio utajua umaskini wako hahahahahaahha Asante
 
Wewe ndo unakurupuka na analysis za kitoto.
Hivi mtu ukiwa na Tshs.2,000/= na ukaamua kula ugali dagaa kwa Tshs.1,500/=, maji ya kiroba 300/= basi utajitapa kuwa wewe una mafanikio makubwa kwa kuwa pesa yako haijaisha na umebakiza Tshs.200/=?....
Pole sana boss,mfano mfu kabisa. Yaani matumizi ya serikali na kula ugali unalinganisha?
 
Kwa tuliobahatika kuushudia utawala wa mwl JKN ni wazi kabisa kuwa ni mashuhuda kuwa tuliishi maisha yasiyo na stress...
Mwezi Disemba ni mwisho wa mwaka kikodi, kuna oparesheni nyingi za kukusanya kodi, na hata kuna kubambikiza kodi kwingi tu. Sio mwezi wa kusema 2tr. Ndio wastani wa makusanyo kila mwezi . Januari kibiiashara ni mbaya hivyo kodi pia zitashuka sana tu, mpaka April
 
Hivi akili huwa mmapeleka wapi? Mbona upumbavu umekuwa mwingi?
 
Kwa tuliobahatika kuushudia utawala wa mwl JKN ni wazi kabisa kuwa ni mashuhuda kuwa tuliishi maisha yasiyo na stress

Kuanzia shule ya msingi mpaka Chuo Kikuu ilikuwa ni bure, huduma za afya bure. Kulikuwa hakuna matabaka maana hakuna cha mtoto wa kigogo au kibopa kusoma shule tofauti na watanzania wenzako, kwa ujumla maisha yalikuwa ya raha. Tuachilie mbali setbacks zilizoukumba utawala wa Mwl JKN kwa ujumla alijitahidi sana

Lakini hii ni kwa sababu utawala wa mwl ulitumia vizuri mapato ya serikali ndio maana aliweza kuhakikisha huduma za jamii kama elimu, afya, zinamfikia kila mtanzania.

Kitendo cha serikali ya awamu ya tano kukusanya tril 2 huku matumizi ni tril 1.8+ ni ushahidi tosha kuwa sasa tunaweza kurudi kule alipotuacha Mwl JKN.

Ni wazi kuwa tutaweza kulipia huduma za msingi kama afya na elimu bure kwa watanzania wote. Tunaweza kuanza na elimu bure mpaka kidato cha sita, pia huduma za afya ziwe bure kwa wananchi wote.

Kisingizio kuwa pato la taifa ni dogo na hivyo cost sharing kwenye afya na elimu iwepo hakipo. Hivyo huu ndio wakati wa kuirudisha Tanzania aliyotuachia Mwl JKN.
Uko sawa kabisa.
 
Maisha ni vita! Wanaojua hilo ndio huishi kifalme duniani

Usipofanya vita kupigania maisha, hata kile chako utanyang'anywa Kwa wanaoelewa kuwa maisha ni vita

Kiongozi yoyote anaeendekeza kucheka na waliokalili huo msemo Kodi zote wataingiza mifukoni mwao na bado watamwambia hicho kiti alichokalia hakimfai

Usawa kwenye Kodi na kodi Rafiki, hiyo tr2. Ni kidogo Sana!

Tz inawatu zaidi ya m60, inatakiwa iwe na walipa Kodi nusu ya hao, hata wakiwa wanalipa 1,5000/ Kwa mwezi unaona kabisa Kwa haraka zinachungulia hapo tr
Watu km nyie ni mizigo hapa nchini.
 
Back
Top Bottom