Natangaza nia ya kumuoa yule mama ambaye roli lake lilizama mto wami kama hana mme: Bila mume makini mama atapata tabu

dmkali

JF-Expert Member
Nov 17, 2014
11,252
21,345
Wanawake wenye uthubutu wako wengi Sana! Ni Jambo jema; Na yote hayo yamepelekewa na sisi wanaume kutowatimizia mahitaji yao ipasavyo!

Huyo mama anaonekana Ni miongoni mwa wapambanaji
Biashara Ni VITA ya kiuchumi! Hupaswi kuingia mzimamzima kizembe Utapigwa KNO moja (noki Auti) na usirudi tena uringoni.

Upambanaji hususani wa kuwa mfanyabiashara mkubwa, Kuna msukosuko mingi Sana ambayo inaonekana na isiyoonekana!
Hisia,Maono,Uvumilivu, na Kinga vyote hufanya kazi sambamba

Huyu mama anahitaji kuwa na mme makini Ili awe KICHWA

Ikumbukwe Mwanaume Ni kichwa Cha familia ( hayo Ni maneno kwenye maandiko)
Ukichambua maana ya kichwa; Hata Kama hakina nywele Kama wasemavyo wahenga "akili Ni nywele"

Bado kichwa kipara kinauwezo wa kupasua, kuteleza hata kupenya pembamba ili kiwili wili kipite!
kwahiyo sifa ya kichwa kuongoza Ni wajibu!

Kwa maneno yake mwenyewe yule mama alipohojiwa alisema Hana mme!

Angekuwa na mme;

Isingekuwa rahisi kabisa Ile gari ya biashara kuikatia bima ndogo namna Ile (third party).
Wanaume tunaujinga wetu lakini katu hakuna mwanamme hata awe mme bwege angekubali kukata third party Gari la biadhara tena masafa, huyo mme wa hivyo hata Kama awepo angepewa ushauri hata vijiwe vya kahawa, maana kijiweni huwa tunanyooshana!

Kwenye biashara hususani ya usafilishaji, Ni Kama kucheza draft, lazima akili ichanganye vinginevyo unapigwa kingi mapema!

Mtazunguka sana lakini UKWELI ni kwamba yule mama anahitaji Mme!

La sivyo huko mbeleni akirudi kwenye gemu basi itabidi konda, dreva au Fundi gereji wajitolee!!!

Mnaotoa misaada endeleeni kuchangia!

Mimi najitolea kumuoa yule mama!
Maana imeandikwa Mtu mwanamke atazaa kwa uchungu, na Mtu mwanamme atakula kwa jasho!

Ukipindua haya maandiko, Ewe mwanamke ukaamua kubeba zege leo ni sawa utabeba, Lakini itabidi awepo Mwanaume wa kukutwisha kichwani Hilo zege! Na huyo anaekutwisha ndo kichwa mwenyewe!

............Asili Itabaki Asilia..........
 
Picha ya mwajuma
hqdefault(0).jpg
 
Kwa habari ya mwanaume kuwa kichwa uko sahihi. Imeandikwa:

"Lakini nataka mjue ya kuwa kichwa cha kila mwanamume ni Kristo, na kichwa cha kila mwanamke ni mwanamume, na kichwa cha Kristo ni Mungu" 1KOR 11:3.

Kwa habari ya kumuoa huyo dada: ndugu, wewe si ni una mke wewe????
 
9 Reactions
Reply
Back
Top Bottom