Natangaza maandamano ya amani ya wiki moja nchi nzima kuanzia kesho (11 - 17/08/2011)

President Elect

JF-Expert Member
Aug 9, 2011
693
212
Kwa mujibu wa katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ndugu wananchi, tunawajibika kuandamana kwa amani nchi nzima kupinga adha tunazopata kutokana na ugumu wa maisha uliokithiri.

Kuanzia kesho saa nne asubuhi wananchì wa mkoa wa Dsm tutaandamana kwa amani tukiwa tumeshika vitambaa vyeupe kuanzia Manzese darajani hadi viwanja vya Jangwani. Nitaendelea kutoa ratiba kwa maandamano kama haya kwa mikoa yote nchi nzima kwa muda wa siku saba kuanzia kesho.

Inshallah, kwa pamoja tutaweza kubadilisha na kuboresha mustakabali wa nchi yetu. Hakutakuwa na haja ya mabango, kitambaa cheupe kinatosha, pamoja kwa amani tutapita pembezoni mwa barabara bila kubugudhi magari ambayo maskini wala hayana mafuta, na bila kuharibu mali au kuleta uvunjifu wa amani.

Asanteni kwa ushirikiano wenu.
 
moshi yanaanzia wapi? Na asubuh ya saa ngapi?mtaani kwangu kn zaid ya watu 200 watakaoshiriki
 
Kitambaa cheupe ndio tiketi yako ya kushiriki maandamano haya ya siku saba nchi nzima. Ukiwa na uwezo wa kuja na chupa yako ya maji ya kunywa pia itakuwa vizuri kwa wale wasio kwenye swaum. Mwendo wa mguu kutoka Manzese darajani hadi viwanja vya Jangwani ni hatua ndefu hivyo nawaomba wananchi tuwe wavumilivu, natoa ruhusa kwa watakaopenda kujichomeka njiani waje tuandamane pamoja. Muhimu sana kitambaa cheupe, ishara ya amani. Asanteni sana, pamoja kwa amani nchi yetu itakombolewa kutoka makucha ya mafisadi papa.
 
arachuggah je tuanzie wapi???,,,, nadhani clock tower mpaka NMC will do, ili kutumia the major road ya pale city centre (uhuru road), so that no business takes place, hawa wakubwa wasikie vilio vyetu
 
Nitatoroka kazini nije kuhudhuria hayo maandamano ya amani....
 
arachuggah je tuanzie wapi???,,,, nadhani clock tower mpaka NMC will do, ili kutumia the major road ya pale city centre (uhuru road), so that no business takes place, hawa wakubwa wasikie vilio vyetu
Afu huku shamra shamra za mkutano wa kesho zishaanza. Wanatangaza sasahivi.. Full raha!
 
Naunga mkono hoja 100% nipo Dom hapa ngoja niulize wadau wangu tupige huo mzigo
 
Ratiba ya awali ni kama ifuatavyo: DSM 11/08; Morogoro, Kibaha, Lindi na Mtwara 12/08; Arusha, Moshi, Manyara, Mwanza, Shinyanga, Unguja na Pemba 13/08; Musoma, Tarime, Geita, Mererani, Mafia, Manyara, Tanga, Singida, Tabora na Dodoma 14/08. Nitaendelea kuainisha vituo vya kuanzia maandamano haya ya amani kwa mikoa iliyotajwa hapo juu, na ratiba kwa mikoa iliyosalia. Tafadhali sana ndugu wananchi, tuzingatie kuwa haya ni maandamano ya amani. Muda wa kuanza ni saa nne asubuhi, na tiketi yako ya kushiriki ni kitambaa cheupe, hakutakuwa na haja ya kubeba mabango. Amani kwa wote, sote pamoja tunaweza kuikomboa nchi yetu na kuiondoa kutoka kwenye lindi la umaskini uliokithiri. Inshallah, Mwenyezi Mungu atatusaidia Watanzania.
 
Ratiba ya awali ni kama ifuatavyo: DSM 11/08; Morogoro, Kibaha, Lindi na Mtwara 12/08; Arusha, Moshi, Manyara, Mwanza, Shinyanga, Unguja na Pemba 13/08; Musoma, Tarime, Geita, Mererani, Mafia, Manyara, Tanga, Singida, Tabora na Dodoma 14/08. Nitaendelea kuainisha vituo vya kuanzia maandamano haya ya amani kwa mikoa iliyotajwa hapo juu, na ratiba kwa mikoa iliyosalia. Tafadhali sana ndugu wananchi, tuzingatie kuwa haya ni maandamano ya amani. Muda wa kuanza ni saa nne asubuhi, na tiketi yako ya kushiriki ni kitambaa cheupe, hakutakuwa na haja ya kubeba mabango. Amani kwa wote, sote pamoja tunaweza kuikomboa nchi yetu na kuiondoa kutoka kwenye lindi la umaskini uliokithiri. Inshallah, Mwenyezi Mungu atatusaidia Watanzania.
Inshallah!
 
kila siku maandamano...nahis serikali kiziwi ya CCM kama imeanza kuyazoea naona kuna haya ya kuja kivingine kupinga maovu ya viongozi wa CCM....bado natafakari
 
Wako wananchi wengi wanapenda kujua mimi ni nani, je nina CV au Profile? Ndugu wananchi, mimi ni Mtanzania mzalendo mwenye upeo na utashi wa kuwakomboa Watanzania wenzangu kwa njia ya amani. Watanzania tumenyanyaswa na kudhalilishwa vya kutosha, na wakati wa ukombozi wa kweli kwa mwananchi mnyonge wa nchi hii ni sasa, kama si sasa, basi ni sasa hivi. Pamoja kwa amani tuungane kufikisha ujumbe kwa watawala kwamba 'imetosha'. Amani kwenu nyote, nawashukuru sana kwa usirikiano wenu.
 
Back
Top Bottom