Mimi ni mwanafunzi wa mwaka wa mwisho hapa muhimbili, nalitamani na ninatamani sana kuwatumikia wananchi wenzangu wa kahama. Kilichonisukuma sana ni kuona rasilimali nyingi tulizonazo wana wa Kahama ni aibu maisha tunayoishi tukiendelea kutembelea barabara za vumbi ,ugumu wa maisha ukituandama kiasi cha kutishia amani ya wananchi na migodi pia kwa sababu naona ujambazi na matukio ya ajabu yamezidi.
Lakini pia kama kijana nimefikia uamuzi huu kwa kundi la vijana wenzangu likihangaika bila ajira .Pia kilimo chetu maarufu cha pamba na mpunga vinazidi kufifia kwa sababu ya sera mbovu za viongozi wetu walioamua kutufanya maskini kwa makusudi.
nitaendelea kutoa maelezo mengi sana kuhusiana na huu uamuzi ,Pia Wana KHM wenzangu mliomo jamvini endeleeni kunishauri kadri muwezavyo
NAWASILISHA
Lakini pia kama kijana nimefikia uamuzi huu kwa kundi la vijana wenzangu likihangaika bila ajira .Pia kilimo chetu maarufu cha pamba na mpunga vinazidi kufifia kwa sababu ya sera mbovu za viongozi wetu walioamua kutufanya maskini kwa makusudi.
nitaendelea kutoa maelezo mengi sana kuhusiana na huu uamuzi ,Pia Wana KHM wenzangu mliomo jamvini endeleeni kunishauri kadri muwezavyo
NAWASILISHA