Natamani Tundu Lissu angekuwa ndiye Katibu Mkuu CHADEMA

TAWA

JF-Expert Member
Jun 23, 2013
3,664
1,565
Wanabodi salamu,
Kwangu mimi chaguo langu la nafasi ya ukatibu ndani ya chama pendwa CHADEMA ilikuwa ni mbunge wa singida mashariki mh. Tundu A Lissu.

Huyu jamaa anajua sana kuwabana maccm kiasi kwamba wanamtafutia kila zengwe ili mradi komdhoofisha.

Anakubalika sana na jamii na wafuasi wa chama kwa ujumla.

Ni mwanasheria kitaaluma hivyo chama kitaendeshwa kiweredi tofauti na mashinji.

Udhaifu uliopo kwa sasa ndani ya chama anaujua na anaweza kupambana nao tofauti na mashinji.

Alipambana ndani ya chama hivyo alifanikiwa kukifikisha chama hapa kilipo tofauti na ndugu mashinji sijui kipindi hicho alikuwa wapi.

Pia Tundu lissu tofauti na katibu w sasa, hana makundi kwa maana anakubalika na watu wote ndani na nje ya chama.
 
Wanabodi salamu,
Kwangu mimi chaguo langu la nafasi ya ukatibu ndani ya chama pendwa CHADEMA ilikuwa ni mbunge wa singida mashariki mh. Tundu A Lissu.

Huyu jamaa anajua sana kuwabana maccm kiasi kwamba wanamtafutia kila zengwe ili mradi komdhoofisha.

Anakubalika sana na jamii na wafuasi wa chama kwa ujumla.

Ni mwanasheria kitaaluma hivyo chama kitaendeshwa kiweredi tofauti na mashinji.

Udhaifu uliopo kwa sasa ndani ya chama anaujua na anaweza kupambana nao tofauti na mashinji.

Alipambana ndani ya chama hivyo alifanikiwa kukifikisha chama hapa kilipo tofauti na ndugu mashinji sijui kipindi hicho alikuwa wapi.

Pia Tundu lissu tofauti na katibu w sasa, hana makundi kwa maana anakubalika na watu wote ndani na nje ya chama.
Acha uchambuzi uchwara
 
Huyu Katibu mara msomi, mara muoga. Me kwa mtazamo wangu naona anafanya mambo yake kisomi. Hana jazba
 
ww kibaraka wa lumumba huwezi kutuchagulia sisi chadema katbu mkuu, #twende na mashinji#
 
Kama ninyi wanademocrasia kweli andamaneni kumpinga....

Vinginevyo ni hamna kitu
 
kwakwel sijawah kuona kaz ya mashinji kama katibu mkuuu....
kiukwel hata mm mwanachama nimemkatia tamaa
... hatoi tamko lolote. ... hajitokez hadharan kukemea jambo
nafas imempwaya
 
Nakumbuka baada ya Mashinji kuteuliwa Kigwangala alinukuliwa akisema,"hana uhakika na hilo la Dr.Mashinji kuwa mtu asiyeteteleka sababu wakati ule wa mgomo wa madaktari wao waliacha kumshirikisha kwenye mipango maanake alikuwa ameshaanza kuufyata".(nukuu siyo rasmi)

Basi Makene akaandika makala ndeefu kumjibu Kigwangala sasa naona mmeanza kuungana na Kigwangala kimya kimya.

BTW:Lowassa kasema anaibadilisha CDM kutoka kwenye uanaharakati kiwe chama cha siasa so Mashinji yuko na mtazamo wa Edo.
 
Kwa katibu mkuu tumechemka mkuu..Tukubali tu..haiwezekani haya yote yanatokea katibu mkuu kanyamaza tuuuuu
si mlisema huyu wa sasa ni msomi, tena ni daktari, ninavyojua mm wasomi wazuri huwaga si wanasiasa wazuri, na mbowe aliliona hilo thats why akamleta mashinji ili apwaye na yy mbowe awe juu, hakutaka kufanya kosa alilolifanya kwa dr slaa, katbu kuwa maaruf kuliko mwenyekiti. any way ni mawazo ya mwenyekiti lazma yaheshmiwe.
 
Nakumbuka baada ya Mashinji kuteuliwa Kigwangala alinukuliwa akisema,"hana uhakika na hilo la Dr.Mashinji kuwa mtu asiyeteteleka sababu wakati ule wa mgomo wa madaktari wao waliacha kumshirikisha kwenye mipango maanake alikuwa ameshaanza kuufyata".(nukuu siyo rasmi)

Basi Makene akaandika makala ndeefu kumjibu Kigwangala sasa naona mmeanza kuungana na Kigwangala kimya kimya.

BTW:Lowassa kasema anaibadilisha CDM kutoka kwenye uanaharakati kiwe chama cha siasa so Mashinji yuko na mtazamo wa Edo.
Makene naye aondoke,idara ya habari imekufa kabisa na haina mikakati
 
4 Reactions
Reply
Back
Top Bottom