Natamani simu kali zisiwekwe kioo mbele na nyuma

TheChoji

JF-Expert Member
Apr 14, 2009
4,974
15,310
Siku hizi simu zote za ghali utakuta zina material ya kioo nyuma (battery cover). Hii ni kwa simu zote kuanzia iphone 8, samsung s8 kwenda mbele zote mfuniko wa nyuma ni kioo. Kwangu mimi naona kuweka kioo nyuma ya simu ni wazo la hovyo kwa sababu zifuatazo;
1. Kioo kinateleza. Simu yenye kioo mbele na nyuma haishikiki, yaani mda wowote inaponyoka na ikianguka lazima ipasuke ama kioo cha mbele au cha nyuma.
2. Kioo huvunjika na kukibadilisha ni gharama. Pamoja na kudai wanatumia sijui gorilla glass lakini binafsi sijawahi kuangusha simu ikaacha kupasuka.
3. Kioo hushika uchafu kirahisi sana hasa fingerprint na vumbi.

Mimi nafikiri hawa watengenezaji wa simu lengo lao ni simu ipasuke ili ununue nyingine sijaona kama wana hoja yoyote ya msingi, hasa ukizingatia miaka ya nyuma tulikua na simu za plastic na aluminium na hazikua na shida yoyote.

Mwenye hoja kinzani namkaribisha anitoe tongotongo.
 
SmartSelect_20211024-170613_Chrome.jpg

Hii ndo sababu ya kitaalamu kwa wao kutumia glass mgongoni mwa smartphone
 
Dunia inakwenda kwenye wireless technologies..
Mf
Wireless Charging
Wireless Earbud/ Earphones na ndo maana hizo flagship phones hazina earphone jack..
Wireless na automation au kujiendesha ndo uelekeo wa dunia kwa sasa.
Nimewahi kusoma sehemu kuwa wireless haina ubora kama kutumia wire yenyewe.

Mfano ukiunganisha spika na simu kwa kutumia wire, nyimbo inakuwa vizuri zaidi kuliku ukiunganisha kwa wireless.

Mimi siyo mtaalamu pande hizo nimegusa tu nilichosoma sehemu.

Chief-Mkwawa
 
Nimewahi kusoma sehemu kuwa wireless haina ubora kama kutumia wire yenyewe.

Mfano ukiunganisha spika na simu kwa kutumia wire, nyimbo inakuwa vizuri zaidi kuliku ukiunganisha kwa wireless.

Mimi siyo mtaalamu pande hizo nimegusa tu nilichosoma sehemu.

Chief-Mkwawa
Ni kweli mkuu hata Charger wireless hazifikii waya na umeme mwingi unapotea. Mfano charger ya waya asilimia 98 inaweza ingia kwenye simu na 2 ukapoteza, wakati Wireless tunaongelea 30 mpaka 80, hivyo umeme wa kuchaji simu 3 unaweza tumika kuchaji simu moja.

Same kwa earphone bluetooth ina bandwidth ndogo ili usikilize mziki quality inabidi compression ifanyike na compression inapunguza Quality. Hizi True Wireless Earbuds haziplay Lossless Audio unatoa Laki kadhaa hadi millioni wakati Earphone kali za waya pengine ukatoa laki ama chini ya hapo ukapata quality kali sana, na wired zipo simu nyingi zinakuja na DaC ya maana.
 
Nakubaliana na nyie wakuu
Lakini tukubali au tukatae wakuu
Wataalamu wa technology duniani huko ndiko wanakotupeleka, nadhani hizi changamoto mnazoziona zitapatiwa uvumbuzi ndani ya miaka michache..
 
Hivi wireless charging ni kitu cha maana kiasi icho kweli..?
Katika technology wireless ni jambo la maana sana.
Kumbuka lengo ni kurahisisha matumizi ya vitu sambamba na kuvifanya vivutie.

Mfano saiv ukinunua radio ni vema ununue radio wireless ambayo unaweza connect speakers zake bila nyaya.

Weka cover kuepusha simu zako kupasuka back cover na kioo
 
So why watumie gharama kutumia glass?
Ambapo pia ni gharama kwa mtumiaji endapo ataidondosha ikapasuka na akahitaji ku repair
Ndio maana mimi nimekuja na hoja kwamba huenda jamaa waligundua ukitumia material zisizopasuka kama aluminium au plastic, simu hazichakai haraka na hivyo mtu anakaa nayo miaka nenda rudi, ambapo ni hasara kwa kampuni.

Mfano ukijaribu kuangalia watu wengi sana mpaka leo bado wana iphone 7plus. Ile simu ni ngumu sana maana ni aluminium na mtu anaweza kukaa nayo hata miaka 10, tufauti na iphone 8.
 
Back
Top Bottom