Natamani sana kila member humu wa JamiiForums atumie jina na pamoja na picha yake halisi

Kama ukificha jina halisi, halafu ukaikashifu serikali, wakiamua kufuatilia hutapatikana?. Ulipojiunga JF ulitumia no yako ya simu! Ni sawa na bata kuficha kichwa chake ardhini akifikiria yupo salama.
 
Leo nimetafakari sana juu ya hili jambo, kwa maana wanachama wa humu wa JF wakitumia majina pamoja na picha zao halisi kutaleta faida zifuatazo:

1. Kutaongeza kuheshimiana, endapo kila member humu atatumia jina pamoja na picha yake halisi kutapelekea kuheshimiana kwa kuwa member wengi humu wanachukuliana poa kwa kuwa ID sio halisi kwahiyo unaweza kuta katoto ka mwaka 2000 kanamtimulia vumbi mtu mzima tena wa miaka 70 huko.

2. Kutapunguza idadi ya watu kutumia ID zaidi ya moja , kama mjuavyo wengi humu wana ID's hata 10 kwa ajiri ya maslai yao binafsi hivyo kama mtu ili afungue account lazima atumie jina pamoja na picha yake original itakua ngumu mtu huyo kuwa na ID's zaid ya moja.

3.Kutarahisisha upanikanaji wa mchumba, mpenzi humu jukwaani, Hii naisema kwa kuwa wanawake wengi humu jukwaani wanachukulia sana poa wanaume wa humu jukwaani kwa kuwa awajawaona wanavyofanania, hivyo kama members humu wakitumia utambulisho wao halisi itakua ni rahisi kumpata mchumba tena ata mke humu jukwaani.

4. Kutapunguza utapeli, wengi humu wanatumia ID ambazo hazima taarifa za ukweli kwa ajiri ya kufanya utapeli hivyo endapo kama members humu watatumia majina na picha zao itakua rahisi ata kuwapata kwani picha na jina ni halisi.

Ni hayo tu wakuu kama kuna sehemu nimesahau kugusia unaweza kuongezea nyama

NAWASILISHA.
Yaani wewe ungekuwa mfano ingekuwa vyema nakuzidi hadi Mimi ambae sikuleta hoja ila nipo real kuanzia jina na picha.
 
Kama ukificha jina halisi, halafu ukaikashifu serikali, wakiamua kufuatilia hutapatikana?. Ulipojiunga JF ulitumia no yako ya simu! Ni sawa na bata kuficha kichwa chake ardhini akifikiria yupo salama.
Hahaha sawa mkuu umeeleweka acha tuendelee kujificha humu maana kuna faida zake pia
 
Mengine tuwaachie tu "facebook". Hapa tubakie "huru" tu. Kuna faidi nyingi zaidi kwa JF kuwa kama ilivyo.

Napita tu.
 
Leo nimetafakari sana juu ya hili jambo, kwa maana wanachama wa humu wa JF wakitumia majina pamoja na picha zao halisi kutaleta faida zifuatazo:

1. Kutaongeza kuheshimiana, endapo kila member humu atatumia jina pamoja na picha yake halisi kutapelekea kuheshimiana kwa kuwa member wengi humu wanachukuliana poa kwa kuwa ID sio halisi kwahiyo unaweza kuta katoto ka mwaka 2000 kanamtimulia vumbi mtu mzima tena wa miaka 70 huko.

2. Kutapunguza idadi ya watu kutumia ID zaidi ya moja , kama mjuavyo wengi humu wana ID's hata 10 kwa ajiri ya maslai yao binafsi hivyo kama mtu ili afungue account lazima atumie jina pamoja na picha yake original itakua ngumu mtu huyo kuwa na ID's zaid ya moja.

3.Kutarahisisha upanikanaji wa mchumba, mpenzi humu jukwaani, Hii naisema kwa kuwa wanawake wengi humu jukwaani wanachukulia sana poa wanaume wa humu jukwaani kwa kuwa awajawaona wanavyofanania, hivyo kama members humu wakitumia utambulisho wao halisi itakua ni rahisi kumpata mchumba tena ata mke humu jukwaani.

4. Kutapunguza utapeli, wengi humu wanatumia ID ambazo hazima taarifa za ukweli kwa ajiri ya kufanya utapeli hivyo endapo kama members humu watatumia majina na picha zao itakua rahisi ata kuwapata kwani picha na jina ni halisi.

Ni hayo tu wakuu kama kuna sehemu nimesahau kugusia unaweza kuongezea nyama

NAWASILISHA.
Umetisha firmino

Sent from my SM-J500H using JamiiForums mobile app
 
Hhahaha jf ni hatari kwahiyo watu wakamtimulia vumbii
sio kuchimbika tu Ile ilikua ni vita ya pili ya Tanzania ukitoa Ile ya Uganda maana jamaa alitupiwa makombora ya Nyukilia nikiwa na maana nyuki Hawa Hawa watengeneza asali maana bongo hatuna Nuclear power!
Alikoma bwana
Mwiguluiza Nchembazimana Mwakatozo
Mzee wa tuhamie Burundi!
😁😁😁😁
 
Mengine tuwaachie tu "facebook". Hapa tubakie "huru" tu. Kuna faidi nyingi zaidi kwa JF kuwa kama ilivyo.

Napita tu.
Yeap umesomeka mkuu acha tuenjoy hivi hivi tu
 
sio kuchimbika tu Ile ilikua ni vita ya pili ya Tanzania ukitoa Ile ya Uganda maana jamaa alitupiwa makombora ya Nyukilia nikiwa na maana nyuki Hawa Hawa watengeneza asali maana bongo hatuna Nuclear power!
Alikoma bwana
Mwiguluiza Nchembazimana Mwakatozo
Mzee wa tuhamie Burundi!
😁😁😁😁
Hahaha inawezekna alifungua account nyingine kwa jina jingine tu maisha yakaendelea mkuu
 
Back
Top Bottom