Natamani Rais Magufuli aige muundo wa siasa Israel

Yericko Nyerere

JF-Expert Member
Dec 22, 2010
16,987
20,271
Natamani Rais Magufuli kama mwenyekiti wa Chama Tawala Tanzania afuatilie na kuyachukua haya yanayotokea Israel katika uchaguzi mkuu wa Waziri Mkuu wa Nchi hiyo.

Fikiria kwa nchi kama Israel ambayo imezungukwa na unyeti wa kila kitu kuanzia nchi yenyewe, siasa na utawala, ulinzi na usalama, na pia jicho kali la mahasimu wake. Lakini linapokuja suala la siasa za vyama nchi husimama kama nchi ya kidemokrasia inayoruhusu vyama vyote kufanya siasa bila vyombo vya dola kuingilia vyama pinzania kama ilivyo Tanzania ambayo ni nchi masikini kuanzia kichwani hadi miguuni.

Kinachovutia Uchaguzi huu wa Israel na kinachonisukuma nitamani Rais wangu mpendwa John Pombe Magufuli afuatilie uchaguzi huu, ni aina ya Wagombea kwa upande mmoja Jasusi Benjamin Netanyahu wa Chama cha Likud toka katika kikosi cha siri cha shirika la Ujasusi la nchi hiyo cha MOSSAD kiitwacho Kidon, na Jeneral wa Kijeshi kutoka katika kikosi imara cha jeshi la Israel kiitwacho Unit 269 – Sayeret Matkal bwanana Benny Gantz wa chama cha Nixes.

Licha ya Waziri Mkuu Benjamini Netanyahu kwamba angekuwa na nguvu zote za kufifisha ndoto za Jenerali huyu wa kijeshi kutumia haki ya kikatiba ya nchi hiyo kugombea urais lakini hakuthubutu kumtisha wala kumwingilia wala kumtaka ahamie chama chake kwahiyari ama kwa nguvu, Benny Gantz amekuwa ni mwenye nguvu na ushawishi kwa kiwango cha juu na kutishia uimara wa Netanyahu.

Uchaguzi umepita bila kupata mshindi jambo linalomlazimu Netanyahu kuunda serikali ya mseto, na kinachofurahisha nikuwa wakati wajumbe wa chama cha Nixes wakielekea kwenye kikao cha majadiliano leo, Netanyahu akapinga kuunda serikali ya mseto, huku mwanasheria wa Serikali akiwasilisha mahakamani kesi ya kula nyama na kukosa uaminifu, mashitaka haya yanamlenga Netanyahu kupokea rushwa. Na kwakiasi kikubwa yanaweza kumbomoa ikiwa uchaguzi utarudiwa.

Navuta picha uhuru na uimara wa mihimili na taasisi za kiserikali ulipo Israel ungekuwa uko Tanzania, Fikiria idadi ya misururu ya wagombea wa CCM ambao wangechukua fomu wakiongozwa na Bernard Membe 2020, Fikiria vyama vya upinzani vingekuwa na uwanja sawa wakufanya siasa bila kuingiliwa na chama tawala kupitia dola, nchi ingekuwa mbali sana.
 
Huyo Yericko ni muongo sana! Na pia ana upeo mdogo.

Netanyahu hajawahi kuwa jasusi wa Mossad ila aliwahi kuwa mwanajeshi wa IDF kwenye kikosi cha Sayeret Matkal, ni special forces hawa sio Mossad. Hata kaka yake, Jonathan, ali serve kwenye IDF na ni commando pekee aliyekufa Entebbe.

Benny Gantz alikuwa mkuu wa majeshi, IDF, nafikiri kule wanaita chief of defence staff. Halafu hao watu hawagombei urais! Israel inafuata parliamentary system na rais wao ni ceremonial figure. Mnaosoma upupu wa Yericko nawashangaa sana.
 
Wale ni educated civilived,wanaangalia maslai ya nchi.

Ni watumishi na si watawala.Pia mfumo wa dola kwao uangalia maslai ya nchi na si maslai ya chama.

Wale ni educated civilived,wanaangalia maslai ya nchi.

Ni watumishi na si watawala. Pia mfumo wa dola kwao uangalia maslai ya nchi na si maslai ya chama.
 
Sasa umepinga nini hapo? Mbona Umeandika yaleyale alioandika Jasusi wa kujitegemea Yericko.
Huyo Yericko ni muongo sana! Na pia ana upeo mdogo. Netanyahu hajawahi kuwa jasusi wa Mossad ila aliwahi kuwa mwanajeshi wa IDF kwenye kikosi cha Sayeret Matkal, ni special forces hawa sio Mossad. Hata kaka yake, Jonathan,ali serve kwenye IDF na ni commando pekee aliyekufa Entebbe. Benny Gantz alikuwa mkuu wa majeshi, IDF, nafikiri kule wanaita chief of defence staff. Halafu hao watu hawagombei urais! Israel inafuata parliamentary system na rais wao ni ceremonial figure. Mnaosoma upupu wa Yericko nawashangaa sana.
 
Sasa umepinga nini hapo? Mbona Umeandika yaleyale alioandika Jasusi wa kujitegemea Yericko.
Hapana, soma tena maelezo yake na yangu. Kwa mfano kuna sehemu ametaja urais. Urais wa Israel haogembewi kwa popular vote.

Anyways Jiwe sio mtu wa kujifunza chochote kwa sasa. Anajua kila kitu.
 
Hapana, soma tena maelezo yake na yangu. Kwa mfano kuna sehemu ametaja urais. Urais wa Israel haogembewi kwa popular vote.

Anyways Jiwe sio mtu wa kujifunza chochote kwa sasa. Anajua kila kitu.
Kwamba hajaiga mambo flani toka Rwanda?
 
Umesahau mfumo wetu wa utawala Africa. Kuna ncihi kama South Africa, Botswana, Namibia na Ghana ambazo angalau wapinzani hawabugudhiwi wakati wa uchaguzi na wanajaribu kuwa na fair election. Katiba zao ziko vizuri na viongozi wanazifuata.

Itachukua muda kwa kutengeneza upeo mwingine wa siasa katika nchi zetu hizi na kufikia hapo walipo waisrael. Kwa sasa hatuwezi kutokana na njaa zetu, ukosefu wa elimu na umasikini. Pia Rais ndiye mwenye mamlaka yote na si katiba. Kuna mambo yanafanyika katika nchi zetu hizi yangefanyika kwa mabeberu mtu angejiuzulu haraka sana. Ubabaishaji wa sasa wa viongozi wa Afrika huu wa kulindana hautusaidii bali unaangamiza nchi zetu hizi.

Kinachosikitisha zaidi hata hao wanaoitwa wapinzani wakipewa nchi leo watakuwa kama wenzao tu na ndiyo maana ukiwa mtawala lazima upiganie kwa njia yoyote ile iwe ya kuiba kura alimradi ubakie madarakani.

Hii ni Afrika ambapo hata raisi akikosea hawezi kuulizwa na mtu yeyote maana yuko juu ya sheria. Safari yetu bado ndefu. Sipendi huu msemo wa kusema Afrika ni bara la giza lakini kuna ka ukweli fulani.
 
Unapoongozwa na kiongozi ambaye haikuwahi kufundishwa tofauti ya haki na dhuluma tegemea kukuta dhaluma imekaa palipo na haki na haki ameiweka palipo na dhuluma.
Umemuelezea vizuri kwa maneno machache. Hajui nini maana ya haki, hata haki ya kuishi.
 
Daaah! Nimesoma hii post nimejisikia vbaya Sana and I MEAN IT. Nimeikumbuka 2010 Jenerali Shimbo alivyotoka hadharani kutisha watu wasiingie barabarani kudai matokeo yatangazwe nilikuwa Mwanza nakumbuka kilichokutoa Mkurugenzi wa Ilemela.

Cha ajabu huyu Jenerali na mnadhimu mkuu we Jeshi ndugu Shimbo ilikuja kubainika ana kiasi Cha tillion nne kwenye akaunti huko Africa kusini...baba Yale Riz one akamzawadia ubalozi wa China.
 
Daaah! Nimesoma hii post nimejisikia vbaya Sana and I MEAN IT. Nimeikumbuka 2010 Jenerali Shimbo alivyotoka hadharani kutisha watu wasiingie barabarani kudai matokeo yatangazwe nilikuwa Mwanza nakumbuka kilichokutoa Mkurugenzi wa Ilemela. Cha ajabu huyu Jenerali na mnadhimu mkuu we Jeshi ndugu Shimbo ilikuja kubainika ana kiasi Cha tillion nne kwenye akaunti huko Africa kusini...baba Yale Riz one akamzawadia ubalozi wa China.
sawa Comrade, nafikiri unakumbuka mradi feki wa matrekta ya "POWER TILLER"
Manji naye alikuwako ndani ya huo mradi kupitia kampuni ya Quality Motors.
 
Huyo Yericko ni muongo sana! Na pia ana upeo mdogo. Netanyahu hajawahi kuwa jasusi wa Mossad ila aliwahi kuwa mwanajeshi wa IDF kwenye kikosi cha Sayeret Matkal, ni special forces hawa sio Mossad. Hata kaka yake, Jonathan,ali serve kwenye IDF na ni commando pekee aliyekufa Entebbe. Benny Gantz alikuwa mkuu wa majeshi, IDF, nafikiri kule wanaita chief of defence staff. Halafu hao watu hawagombei urais! Israel inafuata parliamentary system na rais wao ni ceremonial figure. Mnaosoma upupu wa Yericko nawashangaa sana.
senior member Wewe umetisha ni tofauti na senior member wengine! Hongera sana! YERICO YUPO NA AJE AJIBU UONGO WAKE!💪💪💪
 
Back
Top Bottom