Eiyer
JF-Expert Member
- Apr 17, 2011
- 28,258
- 20,707
Natoka kazini nafika nyumbani usiku saa 3,mke wangu nae ndo anafika kutoka kazini,nae amechoka,namwambia tukaoge ananiambia nitangulie kwani amechoka.Naenda kuoga narudi HG anaweka chakula mezani,namuangaza mke wangu namkuta amepitiwa na usingizi kwenye kiti sababu za purukushani za kazini,namwamsha kisha wote tunajongea mezani,chakula sio kitam kama kile anachopika mke wangu,siku hizi hapiki,anakua kazini.Tunaingia kulala nimechoka nilitarajia mke wangu anipoze na mahangaiko ya kutwa nzima kumbe nae anahitaji wa kumpoza,hakuna wa kumpoza mwenzake wote usingizi unatupitia,tunalala kama tumezirai,hakuna muda wa kujadiliana kuhusu familia na maisha yetu.Unyumba tunapeana kimazoea tu,hakuna zile hisia na ham kama zamani.Kukicha watoto nao wanalalamika hatuna muda wa kukaa nao,hg hajui kuwalea kama mama yao.Watoto wanatuona kama wapita njia tu.Ee Mungu wanangu hawa watalelewaje?Najikuta nayatamani maisha niliyokulia mimi,natamani ningekuwa na umri wa baba yangu!! . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . Nyote mnaochangia hebu changieni kwa kushauri kulingana na changamoto hizi zinazotukabili,mtoa mada anaweza kuwa amewawakilisha wenye maisha yenye changamoto hiyo,sio lazima ahusike!