Natamani nikiolewa nimruhusu mume wangu aoe mke mwingine tuwe wawili

Habari zenu wakuu,

Sijui ni kawaida? I'm 27 yrs lakini katika kuishi kwangu kote mpaka leo, mekua nkitamani siku nkiolewa baada ya muda kadhaa nimruhusu mume wangu aoe mke mwingine...yaan naona kama tukiwa wawili ndoa itakua na Raha.

Sitaki kua bi mdogo au mke wa pili nop natamani tuwe niwe mke mkubwa afu mme wangu nimruhusu aoe mwingine ambae natamani tuwe na amani. nawaona wake za baba angu mkubwa yaani wanapendana huwezi Dhani ni wake wenza.

Japo kwa dini yetu ya kikristo wanaamini ni dhambi but.

Personally nimeyatamani sana haya maisha.
Kwenye kikao kijacho tutakubaliana yafuatayo:

Mosi, ujengewe sanamu tatu- moja katikati ya Jiji la DSM pale mnara wa saa ama Askari monument, na nyingine pale Dodoma sambamba na sanamu ya sanamu ya Nyerere pale Nyerere Square.

Na nyingine ndogo pale mnara wa saa Arusha jiji kubwa la Utalii nchini.

Halafu, utapewa ulinzi wa kudumu maisha yako yote.

Then, utapewa phD ya heshima ya masuala ya mahusiano.

Na mwisho kabisa utapewa ubalozi wa kudumu wa wife material Duniani.

Hayo ndio yatakuwa maadhimio ya kikao chetu kijacho
 
Mwenyewe huwa nawaza ka wewe mleta mada mume awe hata na wake sita hivi ili kunipa na mimi mda wa kutimiza ndoto nikiwa busy na kazi zangu pia maana kikubwa mimi kwa mwanaume ni kutaka watoto sasa nikiwa nao tayari furaha yangu yeye ahangaike na hao wake wengine tena ubusy huo hata kugombana na kusumbuana inakuwa kidogo mno.
 
Duuh inaelekea:
1.Una wivu sana ndio maana unataka aoe mke mwingine umuonyeshe upendo wa kweli uko wapi

2.Unapenda kushindana na mwenzio tu katika mahaba mkomeshane

3. Umezoea threesome sex, au unaitamani walau uone ikoje

4. Hujui maana halisi ya Upendo

Yani Kuna mtazamo mingi kiasi kwamba nashangaa mnoo, maana hata wanaoolewa Mathna(mke mwenza) wanasikia maumivu moyoni ila watakubali sababu ni Dini
Haya ndio yaliyopo kichwani mwako Ila unajaribu kumpandikizia mtoa mada.
 
Mwenyewe huwa nawaza ka wewe mleta mada mume awe hata na wake sita hivi ili kunipa na mimi mda wa kutimiza ndoto nikiwa busy na kazi zangu pia maana kikubwa mimi kwa mwanaume ni kutaka watoto sasa nikiwa nao tayari furaha yangu yeye ahangaike na hao wake wengine tena ubusy huo hata kugombana na kusumbuana inakuwa kidogo mno.
Kama kwa mumeo unataka watoto tu Bora usiolewe
 
Habari zenu wakuu,

Sijui ni kawaida? I'm 27 yrs lakini katika kuishi kwangu kote mpaka leo, nimekua nkitamani siku nikiolewa baada ya muda kadhaa nimruhusu mume wangu aoe mke mwingine...yaani naona kama tukiwa wawili ndoa itakua na Raha.

Sitaki kuwa bi mdogo au mke wa pili nop natamani tu niwe mke mkubwa afu mme wangu nimruhusu aoe mwingine ambae natamani tuwe na amani.
Hii ni gia ya kutafuta mchumba humu
 
Mwenyewe huwa nawaza ka wewe mleta mada mume awe hata na wake sita hivi ili kunipa na mimi mda wa kutimiza ndoto nikiwa busy na kazi zangu pia maana kikubwa mimi kwa mwanaume ni kutaka watoto sasa nikiwa nao tayari furaha yangu yeye ahangaike na hao wake wengine tena ubusy huo hata kugombana na kusumbuana inakuwa kidogo mno.
Shida yako watoto tu? Mbona sperm donors wamejaa hapa duniani.
 
Back
Top Bottom