Natamani maisha ya JamiiForums yawe wazi siku moja!

josephwaara

JF-Expert Member
Jun 18, 2016
304
637
Watu wa jamiiforums tunatishiana mno buana!

Majigambo mengi, dharau kedekede na ujuaji usio na kikomo.

Naona nyuzi kibao sasa za majivuno na mashambulizi kwa watu wengine au kundi fulani la watu.

Utakuta mdau wa JF anajisifu kwamba ana IQ kubwa, anamiliki fedha, mchacharikaji, ni mjanja wa kuvaa, anamiliki gari, alipata ufaulu wa juu darasani n.k huku akiunganisha hayo mambo na dis kwa wengine.

Hivi kweli ikitokea dharura identity zetu zikawa wazi ghafla wangapi tutasalia humu JF?

Hizi tabia za kupangiana maisha au kudharau wengine zina tija gani?
Una maisha mazuri sawa, una akili kubwa sawa mshukuru Mungu maana hukujiamlia ni neema na rehema zake tu, tumia hiyo akili yako kusaidia wengine au jamii yako.

Na wengi wanaofanya haya ni vijana, tena wanaojisifu wamesoma vyuo vyetu pendwa Udsm n.k na faculties za sayansi n.k wakati hatuoni hata impact ya elimu zao kwa taifa zaidi ya kuzunguka na laptops tu.
 
Na kuna wale wajuaji wanaojua kila kitu.

Hao huwa nawapenda sana kwa sababu najua namna ya kushughulika nao vizuri.

Ukishawaelewa hawa vinyamkera wa mtandaoni hawakupi shida.

Unaenda nao kwa staili ya uchizi.
Kuna uzi nmesoma punde umejaa dharau, udhalilishaji na chuki kwa kundi fulani la watu,.
Unajiuliza huyu mwandishi ana busara kweli? Yaani mtu hufikiri kabla ya kuandika????
 
Ndo maana ya fake Id. Kama ilivyo kwenye nyumba za ibada ukikutana na waumini wote ni wana nyuso za watu watakatifu humu JF Mtu anakuwa kitu ambacho sicho. Fake id inakufanya Uwe na ujasiri ambao huna, Uwe na identity isiyaathiriwa na maisha yako halisi....

Hapa kondakta anaweza kuwa waziri
Mtanzania kuwa Mrusi
Raisi kuwa machinga
Darasa la pili kuwa Phd n.k

Hata wewe ulipojipa jina lisilo lako ilikuwa ni hatua ya kwanza ya kuwa kitu kingine ambacho si wewe.

Huu mfumo unasaidia mtu kupokea ushauri bila kutizama anayeutoa, mfano drs la pili anaweza kuongea point kubwa na mtu aliyesoma akaichukua bila kujali aliyeitoa maana hajui kiwango chake cha elimu, pia inasaidia kuwa huru maana mabaya utakayofanya huku, matusi utakayotukana au kutukanwa, vituko, majigambo na yooote utakayoyatenda humu yatabaki humu hayataenda na wewe katika identinty yako halisi.

Jambo la msingi ni kuchukua zuri na kuachana na baya na siku zote kukumbuka kuwa upo mtandaoni.
 
Watu wa jamiiforums tunatishiana mno buana!

Majigambo mengi, dharau kedekede na ujuaji usio na kikomo.

Naona nyuzi kibao sasa za majivuno na mashambulizi kwa watu wengine au kundi fulani la watu.

Utakuta mdau wa JF anajisifu kwamba ana IQ kubwa, anamiliki fedha, mchacharikaji, ni mjanja wa kuvaa, anamiliki gari, alipata ufaulu wa juu darasani n.k huku akiunganisha hayo mambo na dis kwa wengine.

Hivi kweli ikitokea dharura identity zetu zikawa wazi ghafla wangapi tutasalia humu JF?

Hizi tabia za kupangiana maisha au kudharau wengine zina tija gani?
Una maisha mazuri sawa, una akili kubwa sawa mshukuru Mungu maana hukujiamlia ni neema na rehema zake tu, tumia hiyo akili yako kusaidia wengine au jamii yako.

Na wengi wanaofanya haya ni vijana, tena wanaojisifu wamesoma vyuo vyetu pendwa Udsm n.k na faculties za sayansi n.k wakati hatuoni hata impact ya elimu zao kwa taifa zaidi ya kuzunguka na laptops tu.
FB_IMG_1656226864791.jpg
 
Sio wote ni majigambo, wengine kweli ni maisha yetu halisi….. tofauti unazoziona mtaani na hata mtandaoni ni hivyo.

To each their own.
 
Hivi kweli ikitokea dharura identity zetu zikawa wazi ghafla wangapi tutasalia humu JF?
Ikitokea hivyo itakuwa ndio mwisho wa Jf tunayoifahamu.
Huu mfumo wa Jf umejengwa juu ya mwamba wa barafu, (Id bandia) ukifanya kosa ukawasha moto juu yake(kuweka uhalisia wa wahusika) ndio itakuwa mwisho wa jf.
Kuna member mmoja (Wangari Maathai) yalimkuta ya kumkuta.
 
Acha watu waishi hapa wanavyotaka wao, hilo halibadilishi uhalisia wa namna walivyo katika maisha yao tusioyaona...
 
Ikitokea hivyo itakuwa ndio mwisho wa Jf tunayoifahamu.
Huu mfumo wa Jf umejengwa juu ya mwamba wa barafu, (Id bandia) ukifanya kosa ukawasha moto juu yake(kuweka uhalisia wa wahusika) ndio itakuwa mwisho wa jf.
Kuna member mmoja (Wangari Maathai) yalimkuta ya kumkuta.
Hv yule alipataga shida gani!!?
kweli sioni I'd yake sikuhizi
 
Back
Top Bottom