Boss la DP World
JF-Expert Member
- Dec 12, 2021
- 1,997
- 7,551
Wakuu heshima kwenu, nahudumu katika kitengo cha manunuzi katika taasisi moja ya umma (sita itaja). Kila mara ninapokuwa nikitekeleza majukumu yangu kuna roho ya ufisadi inanijia, ukweli nikwamba huwa naiba ila sijawahi kuiba zaidi ya laki 5 hata kama manunuzi ni makubwa vipi.
Tamanio langu ni siku moja kutokea katika vichwa vya habari kama fisadi aliyeficha mabilioni nje ya nchi, fisadi ambaye anaheshimika na hakamatiki kirahisi.
Siipendi hii hali lakini sijui kwanini nashawishika na nafasi ya kufanya hivyo ninayo maana najua kupanga mahesabu yangu vyema, napata cha juu na chenchi inabaki.
Naaminika kuliko wenzangu wote, kuna siku wenzangu walinishawishi tuibe laki 1 nanusu kila mmoja kwenye manunuzi ya vifaa vya ofisi, nikakataa walichokuwa hawajui nikwamba niliiba laki 4 na point kwa upole na unyenyekevu.
Naombeni mnielekeze jinsi ya kuishinda hali hii vinginevyo mtaniona kwenye viunga vya mahakama nikiwa nimezungukwa na mawakili wangu tukijaribu kuishinda jamhuri ili baada ya kesi tukatumie fedha zetu.
Tamanio langu ni siku moja kutokea katika vichwa vya habari kama fisadi aliyeficha mabilioni nje ya nchi, fisadi ambaye anaheshimika na hakamatiki kirahisi.
Siipendi hii hali lakini sijui kwanini nashawishika na nafasi ya kufanya hivyo ninayo maana najua kupanga mahesabu yangu vyema, napata cha juu na chenchi inabaki.
Naaminika kuliko wenzangu wote, kuna siku wenzangu walinishawishi tuibe laki 1 nanusu kila mmoja kwenye manunuzi ya vifaa vya ofisi, nikakataa walichokuwa hawajui nikwamba niliiba laki 4 na point kwa upole na unyenyekevu.
Naombeni mnielekeze jinsi ya kuishinda hali hii vinginevyo mtaniona kwenye viunga vya mahakama nikiwa nimezungukwa na mawakili wangu tukijaribu kuishinda jamhuri ili baada ya kesi tukatumie fedha zetu.