ngoshwe
JF-Expert Member
- Mar 31, 2009
- 4,131
- 931
Ni miaka mingi hatujaonana, leo maazimisho ya Kifo cha Mwalimu, nipo katika usafiri wa umma (daladala) nikiwa kituoni, watanzania wenzangu wakiteremka, natizama dirishani, namwona jamaa ninae mfahamu,yeye ni Mmachinga anafanya biashara ya CDs..natamani kumsalimu kumbe nae ameniona anapaza sauti "wee bro, wapi??" Mbele ya huyo rafiki yangu mmachinga kuna mwanamume na mwanake wameongozana, mwanaume anageuka kutizama nilipo, ananiona nikipunga mkono, nae ananipungia, hajui kwa nini nami sijui (hatufahamiani), huyu mwanaume amemkumbatia mtoto mchanga kifuani, ghafla mwanamke aliyeongozana nae nae anageuka, tunagongana macho...anatoa tabasamu dogo na kufumba mdomo kutumia kiganja cha mkono wake, lakini naona kama kakwazika, kama amegusa waya wa umeme, akaduwaa kwa muda, akashindwa kuvuta hatua mbele...ni kama kitu kilikuwa kimemwingia, akajilazimisha kujongea mbele, na akijifanya kama kiatu alichovaa kinamvuka, akainama na kutizama kule nilipo na kutikisa kichwa kwa dalili zote za kuonyesha ana huzuni fulani moyoni baada ya kuniona...hana jinsi, ana hofu fulani!!
Nami nilihisi kitu kimekikamata kooni..nikaachama, nikatamani kuteremka kwenye gari lakini sikuwa na maamuzi ya haraka.. nikahisi sauti ikiniambia "yule aliyekuwa nae ni mumewe na mtoto wao''...mara dereva wa daladala akawa tayari ameondoa gari kwa kasi....akili ikanirejea, nikakumbuka.....duh..huyu mwanamke alikuwa rafiki yangu zamani, tukapotezana..sasa nimemwona lakini sijui anapoishi..nitamwonaje, natamani kumwona tena, nisikie tu hata sauti yake nyororo, inikumbushe zamani .
Nami nilihisi kitu kimekikamata kooni..nikaachama, nikatamani kuteremka kwenye gari lakini sikuwa na maamuzi ya haraka.. nikahisi sauti ikiniambia "yule aliyekuwa nae ni mumewe na mtoto wao''...mara dereva wa daladala akawa tayari ameondoa gari kwa kasi....akili ikanirejea, nikakumbuka.....duh..huyu mwanamke alikuwa rafiki yangu zamani, tukapotezana..sasa nimemwona lakini sijui anapoishi..nitamwonaje, natamani kumwona tena, nisikie tu hata sauti yake nyororo, inikumbushe zamani .